Wakulima wa zao la Pamba wilayani Magu watakiwa kuzingatia ubora

Na Mwandishi Wetu

WAKULIMA wa zao la Pamba wilayani Magu wametakiwa kuzingatia sheria na taratibu za kilimo bora ili kupata pamba yenye ubora itakayoendana na thamani ya soko ya zao hilo .

Wito huo umetolewa na Balozi wa pamba nchini, Agrey Mwanri katika ziara yake inayolenga kuhamasisha na kutoa elimu ya usafi na ubora wa pamba kwa wakulima na AMCOS kwa msimu wa pamba wa 2025/2026.

Akizungumza na wakulima wa zao la pamba katika vijiji mbalimbali wilayani Magu, Mwanri amesema Ziara hiyo imetokana na kushuka kwa ubora wa pamba kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo uvunaji mbaya, utunzaji na uchafuaji wa makusudi wa pamba katika baadhi ya vituo vya kununulia pamba.

Akitoa elimu kwa wananchi walioshiriki vikao hivyo msanifu wa pamba kutoka bodi ya pamba Tanzania, Sharifa Salumu amesema ili kilimo kiwe na tija ni lazima kanuni bora zifuatwe ikiwa ni pamoja na kuandaa shamba la pamba kwa kuondoa maotea yote na kuyachoma, kupanda mbegu bora kwa kuzingatia kupanda kwa msitari na kwa vipimo vinavyoelekezwa, kupalilia kwa wakati na kunyunyizia viuwadudu kwa kufuata maelekezo.

Wakulima walioshiriki mafunzo hayo wameishukuru Serikali kwa kuendelea kuwajali wakulima wa zao la pamba kwani hivi karibuni wakulima hao walipewa baskeli kwaajili ya kuwarahisishia usafiri wa kufika shambani na kutembeleana ili kuhamasisha watu wengine kulima zao hilo.

spot_img

Latest articles

DCEA yakamata Lita 66,048 za kemikali bashirifu

NA MWANDISHI WETU MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ((DCEA), imefanikiwa kukamata...

Chevron yaonesha nia ya kuwekeza Tanzania katika sekta ndogo ya Mafuta na Gesi Asilia

Na Mwandishi Wetu KAMPUNI kubwa ya nishati kutoka Marekani, Chevron Corporation imeeleza utayari wake wa...

Jumba la maajabu laiponza Yanga,  yapigwa faini  milioni 30,  Meneja  matatani

Na Mwandishi Wetu KLABU ya Yanga imetozwa faini ya Sh 30 milioni  kwa kosa la...

Waziri Ndejembi atoa maelekezo mazito utekelezaji wa mradi Malagarasi MW 49.6 KIGOMA

📌Hajaridhishwa na kasi ya utekelezaji wa mkandarasi kwenye mradi 📌Aagiza ukaguzi maalum wa matumizi ya...

More like this

DCEA yakamata Lita 66,048 za kemikali bashirifu

NA MWANDISHI WETU MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ((DCEA), imefanikiwa kukamata...

Chevron yaonesha nia ya kuwekeza Tanzania katika sekta ndogo ya Mafuta na Gesi Asilia

Na Mwandishi Wetu KAMPUNI kubwa ya nishati kutoka Marekani, Chevron Corporation imeeleza utayari wake wa...

Jumba la maajabu laiponza Yanga,  yapigwa faini  milioni 30,  Meneja  matatani

Na Mwandishi Wetu KLABU ya Yanga imetozwa faini ya Sh 30 milioni  kwa kosa la...