Wakulima wa zao la Pamba wilayani Magu watakiwa kuzingatia ubora

Na Mwandishi Wetu

WAKULIMA wa zao la Pamba wilayani Magu wametakiwa kuzingatia sheria na taratibu za kilimo bora ili kupata pamba yenye ubora itakayoendana na thamani ya soko ya zao hilo .

Wito huo umetolewa na Balozi wa pamba nchini, Agrey Mwanri katika ziara yake inayolenga kuhamasisha na kutoa elimu ya usafi na ubora wa pamba kwa wakulima na AMCOS kwa msimu wa pamba wa 2025/2026.

Akizungumza na wakulima wa zao la pamba katika vijiji mbalimbali wilayani Magu, Mwanri amesema Ziara hiyo imetokana na kushuka kwa ubora wa pamba kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo uvunaji mbaya, utunzaji na uchafuaji wa makusudi wa pamba katika baadhi ya vituo vya kununulia pamba.

Akitoa elimu kwa wananchi walioshiriki vikao hivyo msanifu wa pamba kutoka bodi ya pamba Tanzania, Sharifa Salumu amesema ili kilimo kiwe na tija ni lazima kanuni bora zifuatwe ikiwa ni pamoja na kuandaa shamba la pamba kwa kuondoa maotea yote na kuyachoma, kupanda mbegu bora kwa kuzingatia kupanda kwa msitari na kwa vipimo vinavyoelekezwa, kupalilia kwa wakati na kunyunyizia viuwadudu kwa kufuata maelekezo.

Wakulima walioshiriki mafunzo hayo wameishukuru Serikali kwa kuendelea kuwajali wakulima wa zao la pamba kwani hivi karibuni wakulima hao walipewa baskeli kwaajili ya kuwarahisishia usafiri wa kufika shambani na kutembeleana ili kuhamasisha watu wengine kulima zao hilo.

spot_img

Latest articles

Yacouba atambulishwa Mbeya City

Na Mwandishi Wetu NYOTA wa zamani wa Yanga, raia wa Burkina Faso, Yacouba Songne, ametambulishwa ...

Waziri Ndejembi: Tanzania ina fursa kubwa ya kuendeleza nishati ya Jotoardhi

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi, amesema kutokana na uwepo wa vyanzo...

‘Guardians of the Peak’ kuinua utangazaji utalii wa Kilimanjaro kupitia filamu

Na Mwandishi Wetu MRADI wa Guardians of the Peak, unaoingia msimu wake wa pili,...

Serikali yazindua Jukwaa la Vijana, yataja vijana kuwa mhimili Mkuu wa Maendeleo ya Taifa

Na Tatu Mohamed SERIKALI imezindua rasmi jukwaa la kitaifa la vijana lijulikanalo kama ‘Vijana...

More like this

Yacouba atambulishwa Mbeya City

Na Mwandishi Wetu NYOTA wa zamani wa Yanga, raia wa Burkina Faso, Yacouba Songne, ametambulishwa ...

Waziri Ndejembi: Tanzania ina fursa kubwa ya kuendeleza nishati ya Jotoardhi

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi, amesema kutokana na uwepo wa vyanzo...

‘Guardians of the Peak’ kuinua utangazaji utalii wa Kilimanjaro kupitia filamu

Na Mwandishi Wetu MRADI wa Guardians of the Peak, unaoingia msimu wake wa pili,...