Jeshi la Polisi lamkamata kiongozi wa Chadema

Na Mwandishi Wetu

Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam limemkamata Naibu Katibu Mkuu  Bara wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Aman Golugwa kwa uchunguzi wa tuhuma za kusafiri kwa siri kwenda na kurudi nje ya Tanzania.

Taarifa ya Jeshi la Polisi iliyotolewa  leo  Mei 13, 2025 imesema Golugwa amekamatwa saa 6:45 usiku Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, akiwa katika maandalizi ya kusafiri kuelekea Brussels nchini Ubelgiji.

“Jeshi la Polisi lilimkamata Naibu Katibu Mkuu huyo kufuatia taarifa za siri kuwa amekuwa na mienendo ya kuondoka na kurudi nchini bila kufuata taratibu za kisheria hapa nchini,”

“Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linaendelea na uchunguzi wa kina wa taarifa hizi kwa kushirikiana na vyombo vingine vya usalama kuhusu suala hilo.”

Katika taarifa hiyo, Jeshi la Polisi limetoa wito kwa wananchi kuendelea kuwa watulivu wakati uchunguzi ukiendelea na kupuuza taarifa za upotoshaji kuhusu hatua hizi za kisheria zinazomuhusu Golugwa.

spot_img

Latest articles

Kikwete mgeni rasmi kongamano la PBA kesho

Na Mwandishi Wetu RAIS Mstaafu wa awamu ya nne Jakaya Mrisho Kikkwete anatarajiwa kuwa...

Mwanza journos sharpen skills for upcoming elections

By Our Correspondent, Mwanza The Resident Representative of the non-governmental organization Konrad Adenauer Stiftung (KAS)...

Wanahabari Mwanza wafundwa kuhusu Sheria za Uchaguzi, maadili

MWAKILISHI Mkazi wa shirika lisilo la kiserikali la Konrad Adenauer Stiftung nchini, Peter Koch,...

Wanahabari Mwanza wafundwa kuhusu Sheria za Uchaguzi, maadili

Na Mwandishi Wetu, Mwanza MWAKILISHI Mkazi wa shirika lisilo la kiserikali la Konrad Adenauer Stiftung...

More like this

Kikwete mgeni rasmi kongamano la PBA kesho

Na Mwandishi Wetu RAIS Mstaafu wa awamu ya nne Jakaya Mrisho Kikkwete anatarajiwa kuwa...

Mwanza journos sharpen skills for upcoming elections

By Our Correspondent, Mwanza The Resident Representative of the non-governmental organization Konrad Adenauer Stiftung (KAS)...

Wanahabari Mwanza wafundwa kuhusu Sheria za Uchaguzi, maadili

MWAKILISHI Mkazi wa shirika lisilo la kiserikali la Konrad Adenauer Stiftung nchini, Peter Koch,...