Simba azidi kumkimbiza Yanga,  bado pointi 4

Na Mwandishi Wetu

Simba imeibuka na ushindi wa mabao 5-1 dhidi ya Pamba Jiji katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliopigwa leo Mei 8,2025 kwenye Uwanja wa KMC Complex, jijini Dar es Salaam.

Katika mchezo huo mabao ya Simba yamefungwa na Jean Ahoua alifunga matatu ‘Hat trick’ na Lionel Ateba aliyefunga mawili, huku bao la Pamba likifungwa na Mathew Momanyi.

Ushindi huo unaifanya Simba kupunguza ‘gap’ la pointi ambapo imebakisha alama nne kuifikia Yanga iliyopo kileleni na pointi 70.

Simba imefikisha pointi 66 ikiwa imecheza michezo 25, wakati Yanga imecheza mechi 26.

Kwa upande wa Pamba hali inazidi kuwa ngumu kwao, kwani ipo katika hatari ya kushuka daraja ambapo inashika nafasi ya 13 katika msimamo na pointi 27, imecheza michezo 27.
 

spot_img

Latest articles

Kapinga azindua Kituo Mama cha gesi asilia iliyoshindiliwa (CNG) DAR

📌 Ni cha Pili kwa ukubwa barani Afrika, Cha Kwanza kwa ukubwa EAC 📌 Kujaza...

Mapato yasiyo ya kodi yafikia asilimia 67, OMH yadhamiria kufikia lengo la mwaka

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia Ofisi ya Msajili wa Hazina (OMH), imeendelea kuonesha mafanikio...

Dkt. Biteko: Matumizi ya Nishati Safi ya kupikia kufikia asilimia 75 mwaka 2030

Na Mwandishi Wetu 📌 Dkt. Biteko akutana na Balozi wa Japan nchini 📌 Tanzania na...

Twange aanza kazi rasmi Tanesco

📌Aomba ushirikiano ili kuhakikisha wananchi wanaendelea kunufaika na umeme wa uhakika. 📌Aahidi Kuendeleza Mazuri yaliyofanyika...

More like this

Kapinga azindua Kituo Mama cha gesi asilia iliyoshindiliwa (CNG) DAR

📌 Ni cha Pili kwa ukubwa barani Afrika, Cha Kwanza kwa ukubwa EAC 📌 Kujaza...

Mapato yasiyo ya kodi yafikia asilimia 67, OMH yadhamiria kufikia lengo la mwaka

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia Ofisi ya Msajili wa Hazina (OMH), imeendelea kuonesha mafanikio...

Dkt. Biteko: Matumizi ya Nishati Safi ya kupikia kufikia asilimia 75 mwaka 2030

Na Mwandishi Wetu 📌 Dkt. Biteko akutana na Balozi wa Japan nchini 📌 Tanzania na...