G. 55 rasmi wajitoa Chadema

Na Mwandishi Wetu

Aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Chadema Zanzibar, Salum Mwalimu na wanachama wengine wa chama hicho wametangaza kujitoa katika chama hicho kwa madai ya kutoridhishwa na yanayoendelea.

Wametangaza uamuzi huo leo Mei 7, 2025 jijini Dar es wakati wakizungumza na waandishi wa habari.

Akitangaza uamuzi huo aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu Chadema Bara, Benson Kigaila akiwa pamoja na Salumu Mwalimu, aliyewai kuwa Katibu Mkuu wa Baraza la Wanawake (Bawacha), Catherine Ruge, John Mrema na Julius Mwita, amesema wamejitoa lakini hawaendi CCM.

Kigaila amesema muda ukifika wataeleza ni wapi wanapohamia na sasa wanashauriana na vyamba mbalimbali.

“Sisi tumeamua wote kwa pamoja kujiondoa Chadema ili tuwaachie hicho chama waendeshe wanavyotaka. Hatuwezi kuwa wanachama wa chama ambacho maamuzi yake hayafanywi kwa vikao.

“Hatuwezi kuwa wanachama ambao wanabaguliwa.Katiba haifuatwi, sisi sio chawa, sisi tunajitambua, tuliingia Chadema malengo na tunatoka Chadema kwa sababu malengo yameisha basi tunawaachia chama chao,” ameelaza Kigaila.

Kwa upande wake Mwalimu amesema alikuwepo katika chama hicho kwa muda mrefu na hakufuata vyeo wala fedha bali aliamini kwamba kama mtoto wa Taifa hili ana kila sababu ya kutoa mchango wake nchini.

spot_img

Latest articles

DCEA yakamata Lita 66,048 za kemikali bashirifu

NA MWANDISHI WETU MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ((DCEA), imefanikiwa kukamata...

Chevron yaonesha nia ya kuwekeza Tanzania katika sekta ndogo ya Mafuta na Gesi Asilia

Na Mwandishi Wetu KAMPUNI kubwa ya nishati kutoka Marekani, Chevron Corporation imeeleza utayari wake wa...

Jumba la maajabu laiponza Yanga,  yapigwa faini  milioni 30,  Meneja  matatani

Na Mwandishi Wetu KLABU ya Yanga imetozwa faini ya Sh 30 milioni  kwa kosa la...

Waziri Ndejembi atoa maelekezo mazito utekelezaji wa mradi Malagarasi MW 49.6 KIGOMA

📌Hajaridhishwa na kasi ya utekelezaji wa mkandarasi kwenye mradi 📌Aagiza ukaguzi maalum wa matumizi ya...

More like this

DCEA yakamata Lita 66,048 za kemikali bashirifu

NA MWANDISHI WETU MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ((DCEA), imefanikiwa kukamata...

Chevron yaonesha nia ya kuwekeza Tanzania katika sekta ndogo ya Mafuta na Gesi Asilia

Na Mwandishi Wetu KAMPUNI kubwa ya nishati kutoka Marekani, Chevron Corporation imeeleza utayari wake wa...

Jumba la maajabu laiponza Yanga,  yapigwa faini  milioni 30,  Meneja  matatani

Na Mwandishi Wetu KLABU ya Yanga imetozwa faini ya Sh 30 milioni  kwa kosa la...