Serikali yatambua mchango wa Kibanda katika tasnia ya habari, yampa zawadi

Na Mwandishi Wetu, Media Brains

Mwandishi wa Habari Mkongwe,  Absalom Kibanda ambaye pia ni Mkurugenzi Mwenza wa Kampuni ya Media Brains,  amezawadiwa na Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kutokana na mchango wake katika tasnia ya habari nchini.

Zawadi hiyo ya fedha taslimu Sh 10 milioni, imekabidhiwa jana na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Prof. Palamagamba Kabudi mbele ya Rais Samia Suluhu Hassan wakati wa utoaji tuzo za Samia  Kalamu  Awards 2025, jijini Dar es Salaam.

Kibanda amepewa zawadi hiyo pamoja na wakongwe wengine ambao ni Deodatus Balile, Haula Shamte na Baraka Islam  kutokana na uandishi wao mahiri wa habari na uchambuzi hasa katika masuala ya siasa.

Akizungumza wakati wa kutoa zawadi hizo, Prof. Kabudi amesema habari na makala ambazo wameziandika wakongwe  hao zimekuwa mchango mkubwa na zimewaleta watanzania pamoja bila kuligawa Taifa.

“Mheshimiwa Rais nawiwa wingi wa shukrani kwa  waandishi wenzangu wa habari, na wapo  waandishi wa habari mahiri wa habari za siasa zenye uchambuzi wa kina, zinazojenga umoja, uzalendo, mshikamano na zinazotambua hatua kubwa za kimaendeleo ambayo Taifa letu limepga hasa katika miaka hii minne ya uongozi wako.

“Habari na makala ambazo wameziandika Mheshimiwa Rais ni makala ambazo zimetuleta pamoja, zimetujenga pamoja na ni makala ambazo haziligawi Taifa. Kawa kutambua mchango wa hao waandishi wa habari, Wizara imeona ni vyema nao watunukiwe zawadi na wizara,” ameeleza Prof. Kabudi.

spot_img

Latest articles

DCEA yakamata Lita 66,048 za kemikali bashirifu

NA MWANDISHI WETU MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ((DCEA), imefanikiwa kukamata...

Chevron yaonesha nia ya kuwekeza Tanzania katika sekta ndogo ya Mafuta na Gesi Asilia

Na Mwandishi Wetu KAMPUNI kubwa ya nishati kutoka Marekani, Chevron Corporation imeeleza utayari wake wa...

Jumba la maajabu laiponza Yanga,  yapigwa faini  milioni 30,  Meneja  matatani

Na Mwandishi Wetu KLABU ya Yanga imetozwa faini ya Sh 30 milioni  kwa kosa la...

Waziri Ndejembi atoa maelekezo mazito utekelezaji wa mradi Malagarasi MW 49.6 KIGOMA

📌Hajaridhishwa na kasi ya utekelezaji wa mkandarasi kwenye mradi 📌Aagiza ukaguzi maalum wa matumizi ya...

More like this

DCEA yakamata Lita 66,048 za kemikali bashirifu

NA MWANDISHI WETU MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ((DCEA), imefanikiwa kukamata...

Chevron yaonesha nia ya kuwekeza Tanzania katika sekta ndogo ya Mafuta na Gesi Asilia

Na Mwandishi Wetu KAMPUNI kubwa ya nishati kutoka Marekani, Chevron Corporation imeeleza utayari wake wa...

Jumba la maajabu laiponza Yanga,  yapigwa faini  milioni 30,  Meneja  matatani

Na Mwandishi Wetu KLABU ya Yanga imetozwa faini ya Sh 30 milioni  kwa kosa la...