THRDC yashauri kuitishwa mkutano wa kitaifa wa maridhiano

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC) umesema kuna umuhimu wa kukaa kwenye muafaka wa kitaifa na kukubaliana mambo ya msingi kabla ya kwenda kwenye Uchaguzi Mkuu wa Oktaba mwaka huu.

Mtandano huo umesema siyo afya kuona kuna mvutano unaendelea kwa sura inayoonekana na kwamba mambo yote ambayo yanalalamikiwa yanapaswa kujadiliwa kupitia mkutano wa kitaifa utakaohusisha makundi yote.

Mratibu Taifa wa THRDC, Wakili Onesmo Olengurumwa, ameeleza hayo kufuatia mvutano unaoendelea kuhusu Mwenyekiti wa Chadema, Tundu Lissu, ambaye anashtakiwa kwa kosa la uhaini katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

“Tunafanya kosa pale ambapo tunataka kuwazuia Watanzania wasiende kuwafuatilia ndugu zao magereza, mahakamani, hospitali na mahali popote ambapo wanahitaji kwenda kuwafuatilia…suala hili linaendelea kujenga taswira mbaya katika Serikali…nguvu kubwa inatumika pasipo sababu ya msingi,” amesema Wakili Olengurumwa.

Amesema suala hilo halipaswi kuendelea na kushauri na kwamba huu ni muda muafaka wa kuondoa changamoto zinazoendelea kwa kutumia falsafa ya Rais Samia Suluhu Hassan (4R) na mambo yanayolalamikiwa yanaweza yakaingia kwenye makubaliano ya muafaka na kila mmoja kwenda kwenye uchaguzi akiwa ameridhika.

“Suala hili linaweza likamalizwa kwa mazungumzo, bado tunasisitiza twende kwenye muafaka wa kitaifa kabla ya kwenda kwenye uchaguzi. Sio afya kuona mvutano unaendelea. Mambo yote ambayo yanalalamikiwa kama taifa ni nafasi ya kukaa kwenye mazungumzo na kujadiliwa, tunahitaji kuwa na mkutano wa kitaifa utakaohusisha makundi yote.

“Viongozi wa dini, siasa, serikali, polisi, tume, msajili wa vyama vya siasa, taasisi zote zinazohusika na uchaguzi wote kwa pamoja kama inawezekana tushirikiane kufanya mkutano wa kitaifa wa maridhiano…bado tunasisitiza itafutwe namna ya kutengeneza muafaka kwa taifa letu.

Wakili Olengurumwa pia amevishauri vyama vya upinzani hasa Chadema wawe tayari kwenda kwenye meza ya mazungumzo na makundi yote yashauriwe kwamba ni muhimu kushiriki na kuzingatia amani, utulivu, haki, uzalendo, umoja na upendo katika taifa.

“Yaliyotokea Kisutu tunayakemea, tunashauri vyombo vya usalama mambo ya kwenda mahakamani yanapaswa kuangaliwa kwa umakini kwa sababu suala la kwenda mahakamani ni haki ya kila Mtanzania ambaye ana ndugu na jamaa katika vyombo hivi,” amesema Wakili Olengurumwa.

spot_img

Latest articles

Papa mpya apatikana ni Robert Prevost

Na Mwandishi Wetu Papa Mpya wa Kanisa Katoliki Duniani, ametangazwa ni Kardinali Robert Francis Prevost(69),...

Waziri Masauni, Umoja wa Ulaya wajadili Mazingira

Mwandishi Maalum-Denmark Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhandisi Hamad...

Serikali yasamehe faini za maji, yataka wananchi warejeshewe huduma

Na Mwandishi Wetu Waziri wa Maji, Jumaa Aweso ametangaza msamaha wa faini zote kwa wananchi...

Spika wa Bunge ateta na Dk. Mwapinga, amhakikishia ushirikiano

Na Mwandishi Wetu Spika wa Bunge la Tanzania na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani...

More like this

Papa mpya apatikana ni Robert Prevost

Na Mwandishi Wetu Papa Mpya wa Kanisa Katoliki Duniani, ametangazwa ni Kardinali Robert Francis Prevost(69),...

Waziri Masauni, Umoja wa Ulaya wajadili Mazingira

Mwandishi Maalum-Denmark Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhandisi Hamad...

Serikali yasamehe faini za maji, yataka wananchi warejeshewe huduma

Na Mwandishi Wetu Waziri wa Maji, Jumaa Aweso ametangaza msamaha wa faini zote kwa wananchi...