Gavana Tutuba afanya mazungumzo na Makamu wa Rais wa IFC, John Gandolfo

Na Mwandishi Wetu

GAVANA wa Benki Kuu ya Tanzania, Emmanuel Tutuba, amekutana na kufanya mazungumzo na Makamu wa Rais wa Taasisi ya Fedha ya Kimataifa ya Benki ya Dunia (IFC), John Gandolfo, katika ukumbi wa mikutano wa Ubalozi wa Tanzania, jijini Washington D.C., Marekani.

Katika mazungumzo hayo, walijadili masuala mbalimbali yanayohusu namna ya kuongeza upatikanaji wa mitaji na mikopo kwa sekta binafsi, ufanisi na maendeleo ya masoko ya fedha na mitaji, pamoja na fursa za uwekezaji nchini Tanzania.

Gavana Tutuba alieleza kuwa uchumi wa Tanzania ni imara na thabiti, jambo linalodhihirishwa na viashiria mbalimbali vya kiuchumi.

Alitoa wito kwa IFC pamoja na mashirika mengine ya kimataifa kuwawezesha kifedha wawekezaji wote wenye nia ya kuwekeza nchini Tanzania.

Kikao hicho pia kilihudhuriwa na Naibu Gavana, Dkt. Yamungu Kayandabila, Mkurugenzi wa Utafiti na Sera za Uchumi BoT, Dkt. Suleiman Missango, Meneja wa Sera ya Fedha BoT, Asimwe Bashagi, pamoja na maafisa waandamizi kutoka IFC.

spot_img

Latest articles

Waziri Aweso: Tuna uhakika wa maji ya kutosha Dar na Pwani

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Maji, Jumaa Aweso amewatoa hofu wakazi wa mikoa ya...

PURA yajivunia mafanikio katika Ajenda ya Nishati Safi na ushiriki wa Watanzania Sekta ya Mafuta na Gesi

Na Tatu Mohamed MAMLAKA ya Kudhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) imesema inajivunia...

Machungu, damu yamwagwa tena

Maadhimisho ya Saba Saba nchini Kenya ni tukio muhimu katika kukumbuka mapambano ya kudai...

eGA yatumia Sabasaba kuelimisha umma kuhusu Mfumo wa e-Mrejesho, yajivunia Tuzo ya Kimataifa

Na Tatu Mohamed MAMLAKA ya Serikali Mtandao (eGA) imeendelea kuonesha namna ambavyo Serikali inavyotekeleza mageuzi...

More like this

Waziri Aweso: Tuna uhakika wa maji ya kutosha Dar na Pwani

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Maji, Jumaa Aweso amewatoa hofu wakazi wa mikoa ya...

PURA yajivunia mafanikio katika Ajenda ya Nishati Safi na ushiriki wa Watanzania Sekta ya Mafuta na Gesi

Na Tatu Mohamed MAMLAKA ya Kudhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) imesema inajivunia...

Machungu, damu yamwagwa tena

Maadhimisho ya Saba Saba nchini Kenya ni tukio muhimu katika kukumbuka mapambano ya kudai...