Ewura yazitaka kampuni za gesi kuongeza mawakala, kudhibiti uchakachuaji wa gesi

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

MAMLAKA ya Udhibiti wa Huduma za nishati na Maji (Ewura) imezitaka Kampuni za gesi kuongeza idadi ya mawakala wa usambazaji kwenye maeneo mengi ili kuepusha watu kwenda kununua gesi kwa wauzaji wasio rasmi.

Wito huo umetolewa leo Aprili 24, 2025 na Meneja wa Ewura, Kanda ya Mashariki, Mhandisi Nyirabu Musira wakati akifungua semina kwa wasambazaji wa gesi za kupikia (LPG) yenye lengo la kuhakikisha usambazaji wa gesi ya LPG unafanyika kwa njia zilizo halali na salama kwa watu na mazingira.

Amesema kuwa uchakachuaji wa gesi ya kupikia ni changamoto ambayo imekuwa ikiongezeka siku za hivi karibuni ambapo wafanyabiashara wasio waaminifu wamekuwa wakitumia mitungi kujaza mitungi midogo kwa kiwango hafifu.

“Zipo changamoto kadhaa kwenye biashara hii ya LPG, lakini changamoto ambayo imekuwa ikiongezeka sana kwa siku za hivi karibuni ni ujazaji haramu wa mitungi ya gesi. Licha ya kufanya hivyo ni uhalifu kisheria, lakini pia ni hatari kwa usalama wa watu na mali kwani tumeshuhudia ajali za milipuko ya mioto inayotokana na shughuli hizi.

“Niwaonye wafanyabiashara kuacha tabia hii kwani ni kinyume cha taratibu na sheria, tunaendelea na ufuatialiaji, watakaobainika hatua Kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao,” amesema.

Aidha ametoa wito kwa mawakala wa LPG kuhakikisha wanakuwa na leseni hai za Ewura na wanafanya biashara kwa kufuata masharti ya leseni.

Mhandisi Musira ameeleza kuwa matumizi ya LPG nchini yamekuwa kwa kiasi kikubwa ambapo katika kipindi cha mwaka 2023/24 kiasi cha gesi kilichoingizwa nchini ni takribani Tani za ujazo 403,638.

“Hili ni ongezeko la asilimia 38 ukilinganisha na kiasi cha Tani 293,167 zilizoingizwa nchini mwaka 2022/23. Kulingana na rekodi zetu ongezeko hili ndilo kubwa kwa takribani miaka mitano iliyopita,” amesema Mhandisi Musira.

Hata hivyo amesema kuwa, Ewura inaendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhamasisha matumizi sahihi ya gesi, ili kuepuka majanga ya moto yatokanayo na gesi za majumbani.

Ahmed Sharifu ambaye ni Wakala wa gesi ya Oryx Wilaya ya Temeke amesema semina hizo zinawasaidia katika utekelezaji wa kazi zao za kila siku.

“Tunawashukuru Ewura kwani semina hizi zinatupa maono ya mbele na kujua matakwa ya kisheria katika utekelezaji wa majukumu yetu na hii inaonesha kwamba kazi kubwa ya Ewura ni kutuelimisha katika usalama na kujua utaratibu wa kupata leseni,” amesema.

spot_img

Latest articles

CRDB na Costech watenga Sh. Bilioni 4.6 kuwezesha mitaji kwa vijana wabunifu

Na Mwandishi Wetu WIZARA ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kupitia TUME ya Sayansi na...

Wanahabari watakiwa kuweka usawa katika uandishi wa mabadiliko ya tabianchi

Na Tatu Mohamed MWAKILISHI wa kimataifa kutoka ActionAid International, Teresa Anderson, amesema ipo haja...

Dkt. Mwigulu aweka jiwe la Msingi Mradi wa Umeme Mkata

Ni ujenzi wa kituo cha kupokea na kupoza umeme chenye uwezo wa MVA 60 📌Mradi...

Ithibati yatajwa kuimarisha uaminifu wa Sekta ya Habari na Uchumi wa Vyombo vya Utangazaji

Na Mwandishi Wetu BODI ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imesema utekelezaji wa mfumo...

More like this

CRDB na Costech watenga Sh. Bilioni 4.6 kuwezesha mitaji kwa vijana wabunifu

Na Mwandishi Wetu WIZARA ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kupitia TUME ya Sayansi na...

Wanahabari watakiwa kuweka usawa katika uandishi wa mabadiliko ya tabianchi

Na Tatu Mohamed MWAKILISHI wa kimataifa kutoka ActionAid International, Teresa Anderson, amesema ipo haja...

Dkt. Mwigulu aweka jiwe la Msingi Mradi wa Umeme Mkata

Ni ujenzi wa kituo cha kupokea na kupoza umeme chenye uwezo wa MVA 60 📌Mradi...