RAIS SAMIA KUZINDUA BENKI YA USHIRIKA

Na Mwandishi Wetu

Rais Dk. Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuzindua Benki ya Ushirika (Coop BankTanzania), lengo likiwa ni kufufua benki za kijamii zilizofilisika nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Aprili 10, Dodoma, Waziri wa Kilimo, Husein Bashe amesema Wizara ilipokea maagizo ya Rais Samia, kuhakikisha benki za kijamii zilizofilisika zinarejea na katika hatua za awali Aprili 28, 2025 Rais anatarajiwa kuzindua Benki ya Ushirika nchini.

Amesema benki hiyo itazinduliwa ikiwa na matawi manne ambayo yanapatikana Dodoma, Mtwara, Kilimanjaro na Tabora.

“Hatua ya pili itahusisha matawi ya Kagera, Mwanza,Dar es Salaam, Mbeya na Katavi.
Mafunzo kwa mawakala yanaendelea hivyo mbali na matawi hayo kutakuwa na mawakala nchi nzima na kabla ya uzinduzi mnamo Aprili 28 kutatanguliwa na kongamano la wanaushirikika Aprili 27,”amesema Bashe.

Amesema, benki nyingi za ushirika zimefilisika na Rais Dk.Samia ameona haja ya kurejesha benki hizo ili kuinua uchumi kwa jamii hususani wa wakulima.

“Lengo hapa ni wakulima na jamii kuwa na benki ambazo zitawasaidia na kuwaondolea adha wanazokutana nazo katika Benki za kibiashara,” amesema.

Waziri Bashe ameongeza kuwa, mbali na hatua hiyo ya uzinduzi wa benki hiyo, Wizara inaendelea na mazungumzo na Wizara ya Fedha na Mipango kuona haja ya kuiacha Benki ya Kilimo (TADB) ifanye kazi zake za msingi za kuwawezesha wakulima.

“TADB ni Benki ya Kilimo si ya biashara hivyo hata mikopo yake inatakiwa isiwe ya kibishara wakulima wetu hawawezi mikopo ya marejesho ya miaka miwili ama mitatu inawaumiza,” amesema.

Ametoa wito kwa washiriki wa mkutano huo kujiandikisha kwa wingi na kutumia fursa hiyo kunufaika na huduma za kibenki zitakazotolewa.

spot_img

Latest articles

UMEME JUA KISHAPU AWAMU YA PILI KUIONGEZEA TANZANIA MEGAWATI 100 ZA NISHATI JADIDIFU

📌Waziri Ndejembi ashuhudia utiaji saini, asema ni alama ya miradi ya kielelezo nchini 📌Mradi utakuwa...

NDEJEMBI ASHUHUDIA UTIAJI SAINI WA MKATABA WA SHILINGI BILIONI 204.7 WA MRADI WA UMEME WA JUA WA MEGAWATI 100 KISHAPU

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius J. Ndejembi, leo Julai 27, 2026, ameshuhudia...

DHAHABU YENYE THAMANI YA ZAIDI YA BILIONI 1.2 YAKAMATWA IKITOROSHWA

Na Mwandishi Wetu KUFUATIA kuimarishwa kwa mfumo wa udhibiti wa biashara haramu ya madini...

Taasisi za Umma zatakiwa kutokuwa kikwazo kwa wawekezaji

Na Mwandishi Pwani SERIKALI imezitaka Taasisi za Umma kuhakikisha zinakuwa chachu ya ukuaji wa uchumi...

More like this

UMEME JUA KISHAPU AWAMU YA PILI KUIONGEZEA TANZANIA MEGAWATI 100 ZA NISHATI JADIDIFU

📌Waziri Ndejembi ashuhudia utiaji saini, asema ni alama ya miradi ya kielelezo nchini 📌Mradi utakuwa...

NDEJEMBI ASHUHUDIA UTIAJI SAINI WA MKATABA WA SHILINGI BILIONI 204.7 WA MRADI WA UMEME WA JUA WA MEGAWATI 100 KISHAPU

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius J. Ndejembi, leo Julai 27, 2026, ameshuhudia...

DHAHABU YENYE THAMANI YA ZAIDI YA BILIONI 1.2 YAKAMATWA IKITOROSHWA

Na Mwandishi Wetu KUFUATIA kuimarishwa kwa mfumo wa udhibiti wa biashara haramu ya madini...