Usafiri Dar kwenda Mikoa ya Kusini warejea

Na Mwandishi Wetu

USAFIRI umeanza kurejea katika barabara kuu kutoka Dar es Salaam kwenda Lindi baada ya wataalamu wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) kufanya kazi usiku na mchana kurekebisha eneo la Somanga Matandu lililoharibiwa na mvua na kufanya njia isipitike.

Daraja la Somanga lilikatika Aprili 06, 2025 huku lile la Mto Matandu likikatika Aprili 07, 2025 na kusababisha adha kwa abiria wanaotumia Barabara hiyo.

Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega ambaye ameweka kambi katika eneo hilo tangu jana, amewaambia waandishi wa habari kuwa magari madogo 230, mabasi 10 na baadhi ya malori 30 yaliyobeba bidhaa mbalimbali yakiwemo mawe makubwa yamefanikiwa kupita katika eneo la Somanga Mtama na Matandu leo kati ya saa 11:30 alfajiri hadi saa 12:00 asubuhi.

Ulega ameyasema hayo leo Aprili 8, 2025 wakati akitoa taarifa ya awali akiwa mkoani Lindi wakati akiendelea kusimamia zoezi la urejeshaji wa maeneo yaliyokatika katika barabara kuu ya Dar es Salaam – Lindi linaoofanywa na wataalamu wa Wizara ya Ujenzi na TANROADS kwa kushirikiana na mkandarasi.

spot_img

Latest articles

Yacouba atambulishwa Mbeya City

Na Mwandishi Wetu NYOTA wa zamani wa Yanga, raia wa Burkina Faso, Yacouba Songne, ametambulishwa ...

Waziri Ndejembi: Tanzania ina fursa kubwa ya kuendeleza nishati ya Jotoardhi

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi, amesema kutokana na uwepo wa vyanzo...

‘Guardians of the Peak’ kuinua utangazaji utalii wa Kilimanjaro kupitia filamu

Na Mwandishi Wetu MRADI wa Guardians of the Peak, unaoingia msimu wake wa pili,...

Serikali yazindua Jukwaa la Vijana, yataja vijana kuwa mhimili Mkuu wa Maendeleo ya Taifa

Na Tatu Mohamed SERIKALI imezindua rasmi jukwaa la kitaifa la vijana lijulikanalo kama ‘Vijana...

More like this

Yacouba atambulishwa Mbeya City

Na Mwandishi Wetu NYOTA wa zamani wa Yanga, raia wa Burkina Faso, Yacouba Songne, ametambulishwa ...

Waziri Ndejembi: Tanzania ina fursa kubwa ya kuendeleza nishati ya Jotoardhi

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi, amesema kutokana na uwepo wa vyanzo...

‘Guardians of the Peak’ kuinua utangazaji utalii wa Kilimanjaro kupitia filamu

Na Mwandishi Wetu MRADI wa Guardians of the Peak, unaoingia msimu wake wa pili,...