Usafiri Dar kwenda Mikoa ya Kusini warejea

Na Mwandishi Wetu

USAFIRI umeanza kurejea katika barabara kuu kutoka Dar es Salaam kwenda Lindi baada ya wataalamu wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) kufanya kazi usiku na mchana kurekebisha eneo la Somanga Matandu lililoharibiwa na mvua na kufanya njia isipitike.

Daraja la Somanga lilikatika Aprili 06, 2025 huku lile la Mto Matandu likikatika Aprili 07, 2025 na kusababisha adha kwa abiria wanaotumia Barabara hiyo.

Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega ambaye ameweka kambi katika eneo hilo tangu jana, amewaambia waandishi wa habari kuwa magari madogo 230, mabasi 10 na baadhi ya malori 30 yaliyobeba bidhaa mbalimbali yakiwemo mawe makubwa yamefanikiwa kupita katika eneo la Somanga Mtama na Matandu leo kati ya saa 11:30 alfajiri hadi saa 12:00 asubuhi.

Ulega ameyasema hayo leo Aprili 8, 2025 wakati akitoa taarifa ya awali akiwa mkoani Lindi wakati akiendelea kusimamia zoezi la urejeshaji wa maeneo yaliyokatika katika barabara kuu ya Dar es Salaam – Lindi linaoofanywa na wataalamu wa Wizara ya Ujenzi na TANROADS kwa kushirikiana na mkandarasi.

spot_img

Latest articles

DCEA yakamata Lita 66,048 za kemikali bashirifu

NA MWANDISHI WETU MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ((DCEA), imefanikiwa kukamata...

Chevron yaonesha nia ya kuwekeza Tanzania katika sekta ndogo ya Mafuta na Gesi Asilia

Na Mwandishi Wetu KAMPUNI kubwa ya nishati kutoka Marekani, Chevron Corporation imeeleza utayari wake wa...

Jumba la maajabu laiponza Yanga,  yapigwa faini  milioni 30,  Meneja  matatani

Na Mwandishi Wetu KLABU ya Yanga imetozwa faini ya Sh 30 milioni  kwa kosa la...

Waziri Ndejembi atoa maelekezo mazito utekelezaji wa mradi Malagarasi MW 49.6 KIGOMA

📌Hajaridhishwa na kasi ya utekelezaji wa mkandarasi kwenye mradi 📌Aagiza ukaguzi maalum wa matumizi ya...

More like this

DCEA yakamata Lita 66,048 za kemikali bashirifu

NA MWANDISHI WETU MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ((DCEA), imefanikiwa kukamata...

Chevron yaonesha nia ya kuwekeza Tanzania katika sekta ndogo ya Mafuta na Gesi Asilia

Na Mwandishi Wetu KAMPUNI kubwa ya nishati kutoka Marekani, Chevron Corporation imeeleza utayari wake wa...

Jumba la maajabu laiponza Yanga,  yapigwa faini  milioni 30,  Meneja  matatani

Na Mwandishi Wetu KLABU ya Yanga imetozwa faini ya Sh 30 milioni  kwa kosa la...