Tanesco yashinda tena Tuzo za Ubora Huduma kwa Wateja za CICM

📌Urahisi wa upatikanaji whuduma kwa njia za kidigitali watajwa moja ya kigezo cha kushinda tuzo hiyo

📌MD Gissima aibuka kidedea kwa Kusimamia Maboresho yenye tija huduma kwa wateja Sekta ya Umma.

Na Mwandishi Wetu

SHIRIKA la umeme Tanzania (TANESCO) kwa mara nyingine tena limeshinda tuzo ya the ”Most improved Organization” eneo la huduma kwa wateja iliyotolewa na Taasisi ya Chartered Institute of Customer Management(CICM).

Tuzo hizo zimetolewa 28, Machi 2025 jijini Dar es Salaam ambapo Shirika limepata tuzo hiyo baada ya kufanya maboresho ya kutumia njia za kidigitali kurahisisha mchakato wa maombi ya umeme na upatikanaji wa huduma kuwa mwepesi kwa wateja wake.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO , Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano na Huduma kwa Wateja, Irene Gowelle amesema Tuzo hizo ni heshima kwa Shirika ikiwa ni ishara nzuri ya maboresho yanayofanyika kutambuliwa na kuthaminiwa.

“Tuzo hizi ni heshima kubwa kwa TANESCO, zinatuongezea ari ya kufanya vizuri zaidi,tutaongeza ubunifu katika utoaji wa huduma bora kwa wateja wetu,’’.

Aidha , Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO Mha. Gissima Nyamo-Hanga na yeye alishinda Tuzo ya heshima ya Kiongozi anayefanya mabadiliko chanya yenye tija upande wa huduma kwa wateja katika Sekta ya Umma.

Tuzo za Tanzania Service excellence awards hutolewa kila mwaka na zinalenga kutambua Taasisi za Umma na binafsi zinazoimarisha na kuboresha huduma bora kwa wateja wake.

spot_img

Latest articles

Upanuzi wa Kituo cha Kupoza umeme Mbagala mbioni kukamilika

📌Awamu ya kwanza ya upanuzi wa Kituo Megawati 45 yakamilika 📌Asema wananchi wa Mbagala...

Rais Samia aeleza mambo ya kujifunza kutoka kwa Hayati Cleopa Msuya

Na Mwandishi Wetu Rais Samia Suluhu Hassan ameongoza mazishi ya aliyekuwa Makamu wa Kwanza wa...

TFF yamfungia miaka sita Katibu Mkuu DRFA

Na Mwandishi Wetu Katibu Mkuu wa Chama cha Soka Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA),Ramadhan...

Jeshi la Polisi lamkamata kiongozi wa Chadema

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam limemkamata Naibu Katibu Mkuu...

More like this

Upanuzi wa Kituo cha Kupoza umeme Mbagala mbioni kukamilika

📌Awamu ya kwanza ya upanuzi wa Kituo Megawati 45 yakamilika 📌Asema wananchi wa Mbagala...

Rais Samia aeleza mambo ya kujifunza kutoka kwa Hayati Cleopa Msuya

Na Mwandishi Wetu Rais Samia Suluhu Hassan ameongoza mazishi ya aliyekuwa Makamu wa Kwanza wa...

TFF yamfungia miaka sita Katibu Mkuu DRFA

Na Mwandishi Wetu Katibu Mkuu wa Chama cha Soka Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA),Ramadhan...