SIMBA YAIFUATA AL MASRY NA HESABU KALI

Na Winfrida Mtoi

Kikosi cha Simba kinatarajia kuondoka Machi 28,2025 kuifuata timu ya Al Masry nchini Misri kwa mchezo wao wa robo fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika huku uongozi wa klabu hiyo ukiwa na hesabu za kutinga nusu fainali.

Akizungumza na waandishi wa habari, Meneja Habari na Mawasiliano wa hiyo, Ahmed Ally amesema malengo yao msimu huu ni kuhakikisha wanavuka hatua ya robo fainali na kutinga nusu fainali.

Ahmed amesema licha ya kukutana na mpinzani mgumu hatua ya robo fainali lakini wamejipanga kuhakikisha wanavuka na ndiyo sababu ya kuja na kauli mbiu ya ‘Hii tunavuka’.

“Kwa miaka mitano mfululizo tumekuwa tukiishia robo fainali kwenye michuano ya Afrika lakini safari hii tumedhamiria kuhakikisha tunavuka,”amesema Ahmed.

Aidha amesema wachezaji waliokuwa sehemu ya timu ya taifa, Taifa Stars, wataungana na wenzao nchini Misri ili kukamilisha maandalizi ya mchezo huo wakati Camara na Mukwala, tayari wamewasili na kuungana na wenzao kwa maandalizi zaidi kabla ya safari.

spot_img

Latest articles

Serikali yajipanga kuimarisha utumishi wa umma, kuendeleza mageuzi ya kidigitali

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa...

Bokya amtahadharisha mapema Tyson wa Bongo

Na Winfrida Mtoi Bondia Ismail Khalid maarufu Boyka ametamba kutoa kipigo kikali kwa mpinza wake...

Mwili wa Jenista Mhagama Kuzikwa Jumanne Mbinga, Ruvuma

Na Mwandishi Wetu MWILI wa aliyekuwa Mbunge wa Peramiho (CCM), Jenista Mhagama unatarajiwa kuzikwa...

Mradi wa upanuzi Kituo cha kupokea na kupoza umeme cha Kinyerezi I Extension umekamilika

Na Mwandishi Wetu NAIBU Waziri wa Nishati, Salome Makamba, amesema kuwa mradi wa upanuzi...

More like this

Serikali yajipanga kuimarisha utumishi wa umma, kuendeleza mageuzi ya kidigitali

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa...

Bokya amtahadharisha mapema Tyson wa Bongo

Na Winfrida Mtoi Bondia Ismail Khalid maarufu Boyka ametamba kutoa kipigo kikali kwa mpinza wake...

Mwili wa Jenista Mhagama Kuzikwa Jumanne Mbinga, Ruvuma

Na Mwandishi Wetu MWILI wa aliyekuwa Mbunge wa Peramiho (CCM), Jenista Mhagama unatarajiwa kuzikwa...