Dkt. Biteko: Ufundi Stadi umepewa kipaumbele na serikali

📌 Asisitiza kuwa, Rais Samia anajenga vyuo kila wilaya nchini

📌 Apongeza utoaji wa mafunzo na ujuzi kuendana na teknolojia ya kisasa

📌 Makundi maalumu kupewa kipaumbele

📌 Asema VETA itakuwa msingi kwa malezi ya watoto na Vijana

SERIKALI ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeamua kuwekeza kwenye ufundi ili Watanzania waweze kujikomboa katika uchumi.

Hayo yamebainishwa leo Machi 21, 2025 jijini Dar es Salaam na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko akimwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kilele cha Maadhimisho ya miaka 30 ya Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA).

Dkt. Biteko amesema kuwa, Serikali imeweka msukumo mkubwa katika ufundi stadi ili Watanzania wapate elimu yenye viwango vikubwa na ujuzi wa kuweza kujikomboa katika nyanja za kiuchumi na kijamii.

“Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan anajenga VETA kila wilaya ili kuwapa ujuzi watanzania waweze kuajirika katika sekta zote,” amesisitiza Dkt. Biteko.

Aidha, ameipongeza VETA kwa maadhimisho hayo kwani ni hatua kubwa na kuwataka kuendelea kufanya kazi ili kuwajengea uwezo watanzania katika ujuzi mbalimbali.

“Kwa mara myingine nawapongeza VETA kwa kuendelea kutoa mafunzo na ujuzi kuendana na mabadiliko ya teknolojia ili kuhakikisha kuwa ujuzi unatolewa kwa kuzingatia ubora na viwango vya kimataifa, ” amesema Dkt. Biteko.

Vile vile, amesisitiza elimu kutolewa kwa watu wenye mahitaji maalumu na wanaotoka kwenye mazingira magumu nchini yaweze kuongeza fursa kwa kila mtanzania kupata elimu ya ujuzi.

Naye, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda amesema kwamba, Maadhimisho ya Miaka 30 ya VETA ni uhalisia kuwa Serikali imeipa kipaumbele VETA ili vijana wapate elimu ikiwemo kujenga vyuo vya ufundi katika maeneno mengi nchini.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa VETA, CPA, Anthony Kasore amesema kuwa, VETA imezingatia viwango na ubora wa mafunzo unazingatiwa ili vijana wanaohitimu waweze kumudu soko la ajira.

Aidha amemshukuru Rais Samia kwa usimamizi na uwezeshaji wake mkubwa katika mafunzo ya ufundi stadi nchini ili vijana waweze kupata maarifa na ujuzi ya kufanya shughuli za kiuchumi kwa tija.

spot_img

Latest articles

Oktoba 29 siku ya giza, ifungue milango ya haki

OKTOBA 29, 2025 itabakia kuwa siku ya giza na machungu katika historia ya Jamhuri...

Fountain Gate yatoa kocha bora

Na Mwandishi Wetu Kocha wa timu ya Fountain Gate,  Mohamed Laizer amechaguliwa kuwa kocha bora...

Nyota JKT Queens aipigia hesabu Asec Mimosa

Na Winfrida Mtoi Mshambuliaji wa JKT Queens FC, Jamila Rajabu, amesema  amejipanga  kutengeneza  nafasi na...

Zungu achaguliwa kuwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Na Mwandishi Wetu MBUNGE mteule wa Jimbo la Ilala Mussa Azzan Zungu ameibuka mshindi...

More like this

Oktoba 29 siku ya giza, ifungue milango ya haki

OKTOBA 29, 2025 itabakia kuwa siku ya giza na machungu katika historia ya Jamhuri...

Fountain Gate yatoa kocha bora

Na Mwandishi Wetu Kocha wa timu ya Fountain Gate,  Mohamed Laizer amechaguliwa kuwa kocha bora...

Nyota JKT Queens aipigia hesabu Asec Mimosa

Na Winfrida Mtoi Mshambuliaji wa JKT Queens FC, Jamila Rajabu, amesema  amejipanga  kutengeneza  nafasi na...