Mchengerwa amtaka mkandarasi wa Daraja la Mbambe kuongeza kasi ya ujenzi

Na Mwandishi Wetu

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais-Tawala, Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mohamed Mchengerwa, amemtaka mkandarasi wa Kampuni ya Nyanza Road Works kuongeza kasi ya ujenzi wa Daraja la Mbambe lenye urefu wa mita 81 ili likamilike kwa wakati na kuondoa adha inayowakabili wananchi wa Wilaya ya Rufiji.

Mchengerwa ameyasema hayo wakati wa ziara yake ya kikazi katika Kijiji cha Mbambe ya kufuatilia maendeleo ya ujenzi wa daraja hilo.

“Mkandarasi ongeza kasi ya ujenzi wa daraja hili kwani asilimia 22 iliyofikiwa bado ni ndogo sana. Kwa mwendo huu, mvua zikiongezeka zitaleta changamoto itakayokwamisha ujenzi,” amesema.

Aidha, amewataka wananchi wa Kijiji cha Mbambe kushirikiana na uongozi wa wilaya kwa kutoa taarifa pale wanapoona hali ya kusuasua katika ujenzi wa daraja hilo na kuwahakikishia kuwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan tayari ametoa fedha kwa ajili ya fidia kwa wote waliopitiwa na mradi huo, ambao unahusisha pia ujenzi wa barabara za maingilio zenye urefu wa kilomita 3.

“Mkuu wa Wilaya, naelekeza Meneja wa TANROADS wa mkoa kuhakikisha kuanzia wiki ijayo fidia inalipwa kwa wale wote waliokwishahakikiwa madai yao. Rais Samia ameshatoa shilingi milioni 500 kwa ajili ya fidia,” ameagiza Mchengerwa.

Hata hivyo, Waziri Mchengerwa amewataka wananchi wa Mbambe na Rufiji kwa ujumla kupuuza taarifa potofu kwamba mradi wa daraja hilo umesimama, akisisitiza kuwa ujenzi unaendelea.

Awali, Msimamizi wa Mradi kutoka Kampuni ya Nyanza Road Works, Mhandisi Emmanurel Owoya, amesema kuwa ujenzi huo umefikia asilimia 22, ambapo tayari nguzo za msingi 64 kati ya 107 zimejengwa na Sh.Bilioni 24.16 zitatumika kukamilisha ujenzi wa Daraja la Mbambe, likijumuisha barabara za maingilio za kilomita 3 kwa pande zote mbili za daraja.

spot_img

Latest articles

Tanzania yataka ushirikiano imara na kuvuka mipaka kutokomeza maralia 

Na John Mapepele, Geneva, Uswisi  WAZIRI wa Afya wa Tanzania, Mohamed Mchengerwa, ametoa wito wa...

Ofisi ya Msajili wa Hazina yaendesha mafunzo ya Usimamizi wa vihatarishi kwa Taasisi za Umma

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina (OMH), kupitia Kitengo cha usimamizi wa...

Mradi wa njia ya kusafirisha umeme Chalinze-Dodoma kukamilika Agosti 2026: MD Twange

Utekelezaji wa Mradi wafikia asilimia 82.5 📌Shilingi bilioni 514 kutumika ajili utekelezaji wa...

Tume juu ya Tume, tunavuka au tunatumbukia zaidi?

MSINGI ni neno linalobeba maana kubwa katika mambo mengi. Katika ujenzi iwe wa barabara...

More like this

Tanzania yataka ushirikiano imara na kuvuka mipaka kutokomeza maralia 

Na John Mapepele, Geneva, Uswisi  WAZIRI wa Afya wa Tanzania, Mohamed Mchengerwa, ametoa wito wa...

Ofisi ya Msajili wa Hazina yaendesha mafunzo ya Usimamizi wa vihatarishi kwa Taasisi za Umma

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina (OMH), kupitia Kitengo cha usimamizi wa...

Mradi wa njia ya kusafirisha umeme Chalinze-Dodoma kukamilika Agosti 2026: MD Twange

Utekelezaji wa Mradi wafikia asilimia 82.5 📌Shilingi bilioni 514 kutumika ajili utekelezaji wa...