DRC kukutana na M23 Angola kutafuta Suluhu

Na Mwandishi Wetu

JAMHURI ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) itatuma ujumbe nchini Angola siku ya Jumanne kwa ajili ya mazungumzo yenye lengo la kusuluhisha mzozo unaoendelea dhidi ya waasi wanaaminika kuungwa mkono na Rwanda Mashariki, ofisi ya Rais ilisema Jumapili.

Angola ilisema wiki iliyopita kuwa mazungumzo ya moja kwa moja ya amani kati ya DRC na waasi wa M23 yataanza katika mji mkuu wa Angola Luanda mnamo Machi 18.

Rais Felix Tshisekedi, ambaye kwa muda mrefu amefutilia mbali mazungumzo na M23, alikuwa akifikiria kubadili msimamo wake baada ya uungwaji mkono wa kikanda kwa Kongo ukipungua.

“Kwa wakati huu, hatuwezi kusema ni nani atakayekuwa sehemu ya ujumbe,” msemaji wa ofisi ya rais Tina Salama alisema.

M23 imekubali kupokea mwaliko wa Angola, msemaji wake Lawrence Kanyuka alisema siku ya Jumapili, bila kusema kama itashiriki.

M23 ilitoa madai kadhaa baada ya mazungumzo hayo kutangazwa, ikiwa ni pamoja na kumtaka Tshisekedi aeleze hadharani dhamira yake ya kujadiliana nao moja kwa moja.

spot_img

Latest articles

Tume ya Jaji Chande ijitafakari upya

KATIKA dunia tunayoishi sasa suala la uwazi katika kuendesha mambo limekuwa miongoni mwa nguzo...

Msajili wa Hazina azindua Mpango Mkakati wa NMB 2026–2030

Na Mwandishi Wetu MSAJILI wa Hazina, Nehemiah Mchechu, amezindua Mpango Mkakati wa Muda wa...

Tanesco yafanya ukaguzi wa Mita kitaalamu kubaini ukweli malalamiko ya umeme kuisha haraka yagundua mita zipo sawa

📌 Ni kufuatia malalamiko ya baadhi ya wateja kwenye mitandao ya kijamii na vyombo...

Vijana Dar wakutana kusherehekea kumbukizi ya kuzaliwa Rais Samia, wasifu mchango wake kwa maendeleo ya vijana

Na Mwandishi Wetu VIJANA Jijini Dar es Salaam wameungana kusherehekea siku ya kumbukizi ya...

More like this

Tume ya Jaji Chande ijitafakari upya

KATIKA dunia tunayoishi sasa suala la uwazi katika kuendesha mambo limekuwa miongoni mwa nguzo...

Msajili wa Hazina azindua Mpango Mkakati wa NMB 2026–2030

Na Mwandishi Wetu MSAJILI wa Hazina, Nehemiah Mchechu, amezindua Mpango Mkakati wa Muda wa...

Tanesco yafanya ukaguzi wa Mita kitaalamu kubaini ukweli malalamiko ya umeme kuisha haraka yagundua mita zipo sawa

📌 Ni kufuatia malalamiko ya baadhi ya wateja kwenye mitandao ya kijamii na vyombo...