DRC kukutana na M23 Angola kutafuta Suluhu

Na Mwandishi Wetu

JAMHURI ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) itatuma ujumbe nchini Angola siku ya Jumanne kwa ajili ya mazungumzo yenye lengo la kusuluhisha mzozo unaoendelea dhidi ya waasi wanaaminika kuungwa mkono na Rwanda Mashariki, ofisi ya Rais ilisema Jumapili.

Angola ilisema wiki iliyopita kuwa mazungumzo ya moja kwa moja ya amani kati ya DRC na waasi wa M23 yataanza katika mji mkuu wa Angola Luanda mnamo Machi 18.

Rais Felix Tshisekedi, ambaye kwa muda mrefu amefutilia mbali mazungumzo na M23, alikuwa akifikiria kubadili msimamo wake baada ya uungwaji mkono wa kikanda kwa Kongo ukipungua.

“Kwa wakati huu, hatuwezi kusema ni nani atakayekuwa sehemu ya ujumbe,” msemaji wa ofisi ya rais Tina Salama alisema.

M23 imekubali kupokea mwaliko wa Angola, msemaji wake Lawrence Kanyuka alisema siku ya Jumapili, bila kusema kama itashiriki.

M23 ilitoa madai kadhaa baada ya mazungumzo hayo kutangazwa, ikiwa ni pamoja na kumtaka Tshisekedi aeleze hadharani dhamira yake ya kujadiliana nao moja kwa moja.

spot_img

Latest articles

Rais Samia atangaza Baraza Jipya la Mawaziri, nane watemwa

Tatu Mohamed na Winfrida Mtoi RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan,...

MC Pilipili afariki dunia

Na Mwandishi Wetu Mchekeshaji na mshereheshaji maarufu nchini, Emmanuel Mathias 'MC Pilipili' amefariki dunia leo,...

Watahiniwa 595,816 kuanza Mtihani wa Kidato cha Nne kesho

Na Tatu Mohamed JUMLA ya watahiniwa 595,816 wamesajiliwa kufanya Mtihani wa Kidato cha Nne 2025...

More like this

Rais Samia atangaza Baraza Jipya la Mawaziri, nane watemwa

Tatu Mohamed na Winfrida Mtoi RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan,...

MC Pilipili afariki dunia

Na Mwandishi Wetu Mchekeshaji na mshereheshaji maarufu nchini, Emmanuel Mathias 'MC Pilipili' amefariki dunia leo,...