DRC kukutana na M23 Angola kutafuta Suluhu

Na Mwandishi Wetu

JAMHURI ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) itatuma ujumbe nchini Angola siku ya Jumanne kwa ajili ya mazungumzo yenye lengo la kusuluhisha mzozo unaoendelea dhidi ya waasi wanaaminika kuungwa mkono na Rwanda Mashariki, ofisi ya Rais ilisema Jumapili.

Angola ilisema wiki iliyopita kuwa mazungumzo ya moja kwa moja ya amani kati ya DRC na waasi wa M23 yataanza katika mji mkuu wa Angola Luanda mnamo Machi 18.

Rais Felix Tshisekedi, ambaye kwa muda mrefu amefutilia mbali mazungumzo na M23, alikuwa akifikiria kubadili msimamo wake baada ya uungwaji mkono wa kikanda kwa Kongo ukipungua.

“Kwa wakati huu, hatuwezi kusema ni nani atakayekuwa sehemu ya ujumbe,” msemaji wa ofisi ya rais Tina Salama alisema.

M23 imekubali kupokea mwaliko wa Angola, msemaji wake Lawrence Kanyuka alisema siku ya Jumapili, bila kusema kama itashiriki.

M23 ilitoa madai kadhaa baada ya mazungumzo hayo kutangazwa, ikiwa ni pamoja na kumtaka Tshisekedi aeleze hadharani dhamira yake ya kujadiliana nao moja kwa moja.

spot_img

Latest articles

Serikali: Tuchukue hatua kuepuka madhara ya usugu wa vimelea vya magonjwa dhidi ya dawa (UVIDA)

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia kwa Mkurugenzi msaidizi, Kitengo cha Afya Moja, Ofisi ya...

Serikali yawaita wadau kujitokeza kusapoti ushiriki wa wanawake michezoni

Na Winfrida Mtoi Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamis Mwinjuma 'MwanaFA' amewaomba...

Ndejembi awahakikishia wakazi wa Kigamboni umeme wa uhakika

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amefanya ziara ya kikazi ndani ya...

Viongozi Chadema washinda shauri la kuidharau Mahakama

Na Mwandishi Wetu Mahakama Kuu Masjala Ndogo Dar es Salaam imetupilia mbali shauri la maombi...

More like this

Serikali: Tuchukue hatua kuepuka madhara ya usugu wa vimelea vya magonjwa dhidi ya dawa (UVIDA)

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia kwa Mkurugenzi msaidizi, Kitengo cha Afya Moja, Ofisi ya...

Serikali yawaita wadau kujitokeza kusapoti ushiriki wa wanawake michezoni

Na Winfrida Mtoi Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamis Mwinjuma 'MwanaFA' amewaomba...

Ndejembi awahakikishia wakazi wa Kigamboni umeme wa uhakika

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amefanya ziara ya kikazi ndani ya...