DRC kukutana na M23 Angola kutafuta Suluhu

Na Mwandishi Wetu

JAMHURI ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) itatuma ujumbe nchini Angola siku ya Jumanne kwa ajili ya mazungumzo yenye lengo la kusuluhisha mzozo unaoendelea dhidi ya waasi wanaaminika kuungwa mkono na Rwanda Mashariki, ofisi ya Rais ilisema Jumapili.

Angola ilisema wiki iliyopita kuwa mazungumzo ya moja kwa moja ya amani kati ya DRC na waasi wa M23 yataanza katika mji mkuu wa Angola Luanda mnamo Machi 18.

Rais Felix Tshisekedi, ambaye kwa muda mrefu amefutilia mbali mazungumzo na M23, alikuwa akifikiria kubadili msimamo wake baada ya uungwaji mkono wa kikanda kwa Kongo ukipungua.

“Kwa wakati huu, hatuwezi kusema ni nani atakayekuwa sehemu ya ujumbe,” msemaji wa ofisi ya rais Tina Salama alisema.

M23 imekubali kupokea mwaliko wa Angola, msemaji wake Lawrence Kanyuka alisema siku ya Jumapili, bila kusema kama itashiriki.

M23 ilitoa madai kadhaa baada ya mazungumzo hayo kutangazwa, ikiwa ni pamoja na kumtaka Tshisekedi aeleze hadharani dhamira yake ya kujadiliana nao moja kwa moja.

spot_img

Latest articles

Jaji Warioba ni lulu, mtake msitake

KUMEKUWA na mjadala wa wiki kadhaa sasa ukimlenga Waziri Mkuu Mstaafu, Jaji Joseph Warioba,...

🔴🔴Wizara ya Maliasili yaendelea kuwasilisha taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya Taasisi zake kwa Kamati za Bunge

📍 Kamati yaipongeza TAWA kwa ubunifu uliopelekea ongezeko la watalii, mapato Na Mwandishi Wetu, Dodoma KAMATI...

JAB yaonya waajiri katika vyombo vya habari kuzingatia Sheria kuepuka migogoro ya kisheria

Na Mwandishi Wetu BODI ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imewasisitiza waajiri kwenye vyombo...

Kata za Mzinga, Malangali kupiga kura kuchagua madiwani kesho

Na Mwandishi wetu, Dodoma JUMLA ya Wapiga Kura 38,151 walioandikishwa katika Daftari la Kudumu la...

More like this

Jaji Warioba ni lulu, mtake msitake

KUMEKUWA na mjadala wa wiki kadhaa sasa ukimlenga Waziri Mkuu Mstaafu, Jaji Joseph Warioba,...

🔴🔴Wizara ya Maliasili yaendelea kuwasilisha taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya Taasisi zake kwa Kamati za Bunge

📍 Kamati yaipongeza TAWA kwa ubunifu uliopelekea ongezeko la watalii, mapato Na Mwandishi Wetu, Dodoma KAMATI...

JAB yaonya waajiri katika vyombo vya habari kuzingatia Sheria kuepuka migogoro ya kisheria

Na Mwandishi Wetu BODI ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imewasisitiza waajiri kwenye vyombo...