Derby ya wanawake kesho, ubabe ubabe

Na Winfrida Mtoi

Simba Queens na Yanga Princess kesho Machi 18,2025 zinashuka dimbani katika mchezo wa Ligi Kuu ya Wanawake Tanzania Bara, kwenye Uwanja wa KMC Complex, Dar es Salaam.

Kila mmoja akionekana kuwa na hamu ya  kuondoka na alama zote tatu ambapo Yanga Princess inahitaji kulipa kisasi ya kipigo cha bao 1-0 ilichopokea katika mechi ya mzunguko wa kwanza, huku Simba Queens ikitaka kuendeleza ubabe mbele ya wadada hao wa Jangwani.

Simba Queens ambayo ni mwenyeji wa mchezo huo, inaongoza katika msimamo wa ligi hiyo ikiwa na pointi 34 wakati Yanga ikiwa nafasi ya tatu na alama 24 zote zikicheza mechi 12.

Akizungumzia mchezo huo kocha mkuu wa Simba Queens, Yussif Basigi amesema ni mechi muhimu kwao kutokana na kila mmoja kuitolea macho, huku akihitaji ushindi ili kuendelea kukaa kileleni kwa sababu wamepishana alama mbili na JKT Queens iliyopo nafasi ya pili.

Kwa upande wake kocha mkuu wa Yanga Princess, Edna Lema, ametamba kuwa licha ya wapinzani wao kuwa kwenye ubora na kuongoza ligi lakini  wamejiandaa vizuri na hawana presha.

spot_img

Latest articles

Rais Samia afanya mazungumzo na Askofu Malasusa

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu...

Ofisi ya Msajili Hazina yaendesha mafunzo kwa kamati za Bunge Dodoma

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina imeendesha mafunzo kwa Kamati tatu za...

Tume, Serikali na vyama vya siasa kusaini maadili ya uchaguzi kesho

Na Mwandishi Wetu TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, vyama vya siasa na Serikali kesho...

Rais Samia afanya mazungumzo na Mmiliki wa Klabu ya Manchester United, Ratcliffe

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan...

More like this

Rais Samia afanya mazungumzo na Askofu Malasusa

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu...

Ofisi ya Msajili Hazina yaendesha mafunzo kwa kamati za Bunge Dodoma

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina imeendesha mafunzo kwa Kamati tatu za...

Tume, Serikali na vyama vya siasa kusaini maadili ya uchaguzi kesho

Na Mwandishi Wetu TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, vyama vya siasa na Serikali kesho...