Mramba: Kununua umeme nje ya nchi, haimaanishi kuna upungufu nchini

Na Mwandishi Wetu

KATIBU Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mhandisi Felchesmi Mramba amesema kuwa ununuzi wa Umeme kutoka nchi Jirani haimaanishi kuwa nchi iko katika changamoto ya upungufu wa umeme kwa kuwa mpaka sasa Tanzania inazalisha umeme wa kutosha ambao ni takribani Megawati 3796.

Aidha amesema kuwa kununua na kuuziana umeme kwa nchi si jambo geni na Tanzania kwa muda mrefu imekuwa ikinunua umeme nchini Uganda kwa ajili ya Mkoa wa Kagera, nchini Zambia kwa ajili ya Mkoa wa Rukwa na nchini Kenya kwa baadhi ya maeneo ya mkoa wa Tanga hususani ya mpakani.

Ameyasema hayo leo Machi 10, 2025 wakati akitoa Ufafanuzi zaidi kuhusu hatua ya Serikali kununua Umeme nchini Ethiopitia kupitia Nchini Kenya hadi Namanga Mkoani Arusha utaimarisha Upatikanaji wa Umeme katika Mikoa ya Kanda ya Kaskazini ambayo kimsingi kwa sasa inatumia umeme unaozalishwa katika Mikoa ya Kusini.

Amefafanua kuwa hatua hii ina faida kwa pande zote mbili kwa kuwa njia itakayotumiwa kununua umeme nchini Ethiopia ndio hiyo itakayotumiwa kuuza umeme kwa nchi zenye Uhitaji.

Akifafanunua zaidi amesema kuwa jinsi umeme utakavyokuwa ukinunuliwa, umeme wa Ethiopia utaingizwa kwenye mfumo wa Gridi ya Kenya na kisha Kenya itatoa umeme kuja Tanzania ikifidia umeme ulioingizwa kutoka nchini Ethiopia.

“Uamuzi wa Tanzania kuchukua umeme Ethiopia ni kitu chenye faida na sio hasara kama watu wanavyodhani, kwani baadhi ya vyanzo vya umeme hapa nchini vinazalisha uniti moja kwa bei kubwa kuliko bei ambayo umeme huo utanunuliwa kutoka Ethiopia.

“Tunamshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa ridhaa kuruhusu umeme kuingia Kaskazini kutoka nchi Jirani kutokana na hali ya umeme kanda ya Kaskazini kuwa inaingia kidogo katika gridi ya Taifa katika kanda hii,” amesema.

Ameongeza kuwa, tayari kuna nchi zimekuja zinataka kununua umeme nchini ambapo kama nchi inaweza kuwauzia kwa bei kubwa kuliko unaonunuliwa Ethiopia.

Amesema umeme huo unaotoka nchini Ethiopia utasaidia kwa kiasi kikubwa umeme kuimarika kwa kanda ya Kaskazini kwani hali ya umeme kutokuwa na nguvu kumalizika.

“Umeme unaopelekwa mikoa ya Kaskazini unapotea kwa kiwango cha megawati 17 ambazo zinatosha kuhudumia Mkoa wa Songwe ambao unatumia megawati 14, hivyo tukisema tuutoe Bwawa la Mwalimu Nyerere kunakuwa na upotevu wa umeme mwingi.

spot_img

Latest articles

Serikali yaahidi kushirikiana na wadau kuendeleza mchezo wa kuogelea

Na Winfrida Mtoi WADAU wa mchezo wakuogelea Afrika Mashariki wamekutana kujadili maendeleo ya mchezo huo,...

Ndejembi: Tanesco mmefanya mageuzi makubwa katika huduma ya umeme kwa wananchi

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi, amesema kuwa Shirika la Umeme Tanzania...

Dube awapa raha wananchi

Na Winfrida Mtoi BAO pekee lililofungwa na Prince Dube dakika ya 58, limeipa Yanga alama...

Mexico yatwaa taji la Miss Universe 2025, Ivory Coast namba tano

Na Mwandishi Wetu Mexico imeibuka mshindi wa taji la Miss Universe 2025 kupitia mrembo wake...

More like this

Serikali yaahidi kushirikiana na wadau kuendeleza mchezo wa kuogelea

Na Winfrida Mtoi WADAU wa mchezo wakuogelea Afrika Mashariki wamekutana kujadili maendeleo ya mchezo huo,...

Ndejembi: Tanesco mmefanya mageuzi makubwa katika huduma ya umeme kwa wananchi

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi, amesema kuwa Shirika la Umeme Tanzania...

Dube awapa raha wananchi

Na Winfrida Mtoi BAO pekee lililofungwa na Prince Dube dakika ya 58, limeipa Yanga alama...