TAWA yasherehekea Siku ya Wanyamapori Duniani kwa kutoa misaada na elimu ya uhifadhi

Na Mwandishi Wetu

MAMLAKA ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania – TAWA Kanda ya Magharibi jana Machi 3, 2025 imesherehekea Siku ya Wanyamapori Duniani kwa kufanya shughuli mbalimbali za kijamii na uhifadhi, ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za kulinda wanyamapori na mazingira.

Katika maadhimisho hayo, Kanda hiyo ilitoa misaada ya vyakula kwa wanafunzi wenye uhitaji kutoka Shule ya Wanafunzi wenye changamoto ya uoni ya Furaha ikiwemo mchele, unga, mafuta, sukari na sabuni vyote vikiwa na thamani ya shillingi millioni moja.

Misaada hii imelenga kuwasaidia wanafunzi hao na kuhamasisha jamii kuhusu umuhimu wa elimu kwa watoto wenye mahitaji maalum.

Vilevile TAWA ilitembelea Shule ya Sekondari Fundikila na kutoa miche 4000 ya miti ya matunda ya muda mfupi, ikihamasisha upandaji wa miti na kutoa elimu kuhusu uhifadhi wa mazingira.

Shule ya Sekondari Kanyenye nayo ilipokea miche 2000 mingine, kama sehemu ya juhudi za kukuza mazingira bora na endelevu kwa jamii.

Akikabidhi misaada hiyo na miche ya miti Kaimu Kamanda wa Uhifadhi wa Kanda ya Magharibi Lupondije Nyanda ametoa wito kwa wananchi wa Mkoa wa Tabora kushirikiana na Serikali katika jitihada za kulinda rasilimali wanyamapori ikiwa ni pamoja na kutunza mazingira yao huku akiwahamasisha kutembelea vivutio vya utalii hususani bustani ya wanyamapori hai almaarufu Tabora ZOO.

Kilele cha maadhimisho ya Siku ya Wanyamapori Duniani Kitaifa yaliyanyika katika viwanja vya ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete Dodoma mgeni rasmi akiwa ni Waziri wa Maliasili na Utalii Balozi Dkt. Pindi Chana.

spot_img

Latest articles

DCEA yakamata Lita 66,048 za kemikali bashirifu

NA MWANDISHI WETU MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ((DCEA), imefanikiwa kukamata...

Chevron yaonesha nia ya kuwekeza Tanzania katika sekta ndogo ya Mafuta na Gesi Asilia

Na Mwandishi Wetu KAMPUNI kubwa ya nishati kutoka Marekani, Chevron Corporation imeeleza utayari wake wa...

Jumba la maajabu laiponza Yanga,  yapigwa faini  milioni 30,  Meneja  matatani

Na Mwandishi Wetu KLABU ya Yanga imetozwa faini ya Sh 30 milioni  kwa kosa la...

Waziri Ndejembi atoa maelekezo mazito utekelezaji wa mradi Malagarasi MW 49.6 KIGOMA

📌Hajaridhishwa na kasi ya utekelezaji wa mkandarasi kwenye mradi 📌Aagiza ukaguzi maalum wa matumizi ya...

More like this

DCEA yakamata Lita 66,048 za kemikali bashirifu

NA MWANDISHI WETU MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ((DCEA), imefanikiwa kukamata...

Chevron yaonesha nia ya kuwekeza Tanzania katika sekta ndogo ya Mafuta na Gesi Asilia

Na Mwandishi Wetu KAMPUNI kubwa ya nishati kutoka Marekani, Chevron Corporation imeeleza utayari wake wa...

Jumba la maajabu laiponza Yanga,  yapigwa faini  milioni 30,  Meneja  matatani

Na Mwandishi Wetu KLABU ya Yanga imetozwa faini ya Sh 30 milioni  kwa kosa la...