Shilingi Trilioni 8.2 zatumika kukopesha wanafunzi katika kipindi cha miaka 20

Na Mwandishi Wetu 

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema kuwa Serikali kupitia Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu imetumia shilingi trilioni 8.2 kugharamia wanafunzi tangu ilipoanzishwa.

Amesema kuwa pia katika kipindi hicho wanafunzi takribani 830,000 wamenufaika na mfumo huo wa ugharimiaji wa elimu ya juu kupitia Bodi ya mikopo.

Amesema hayo leo Februari 17, 2025 alipomwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye kilele cha maadhimisho ya miaka 20 ya Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu, iliyofanyika kwenye Kituo cha Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam.

“Mafanikio tuliyonayo leo, ni matokeo ya utashi wa kisiasa, uongozi thabiti, maono na michango ya viongozi wetu. Viongozi wetu katika awamu zote walifanya kazi kubwa ya kuhakikisha Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu inafanya vizuri, viongozi wetu walioona mbali kuanzisha mfumo huu wa ugharimiaji wa elimu ya juu kupitia Bodi ya mikopo,” amesema Majaliwa.

Aidha, Majaliwa amesema kuwa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu imefanikiwa kukusanya fedha kiasi cha shilingi trilioni 1.5.

“Ninatambua marejesho hayo yamepatikana kutokana na jitihada na ubunifu mkubwa ambao unasaidia kuwafikia wanufaika ambao wamehitimu na mikopo yao imeiva,” amesema Majaliwa.

Ameongeza kuwa katika kuhakikisha kuwa Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu haiwi mzigo kwa Wanafunzi, Serikali iliamua kufuta tozo za kulinda thamani ya fedha ili kuondoa changamoto katika urejeshaji wa mikopo.

“Kwa sasa mnufaika anarejesha kiasi kile kile ambacho amekopeshwa kwani tozo hizo zilikuwa zinasababisha ongezeko la madeni ya mikopo hiyo,” Majaliwa.

Ameiagiza Bodi ya Mikopo kuendelea kuweka mikakati ya kuendana na kasi ya mababiliko ya teknolojia na ifanye maboresho ya kujiunganisha na kuzungumza lugha moja na taasisi za fedha nchini. 

Kwa upande wake, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda amesema kuwa wakati Rais Dkt. Samia anaingia madarakani alikuta fedha zinazotolewa kwa ajili ya mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu ilikuwa ni shilingi bilioni 464.

“Lakini alipoingia aliagiza fedha kwa ajili ya mikopo ziongezwe, na tuliongeza hadi kufikia bilioni 570, tukaendelea hadi bilioni 654 na sasa ni shilingi bilioni 731,” amesema Majaliwa.

Ameongeza kuwa Rais Dkt. Samia katika kuhakikisha kada za Sayansi zinaendelea kupewa kipaumbele ili kuzalisha wataalam wengi zaidi, aliiagiza Wizara ya Elimu kutenga fedha kwa ajili ya kuanza kutoa ufadhili kwa ajili ya kada hizo ambayo tuliita Samia Scholarship.

“Wakati tunaanza tulitoa shilingi bilioni 3 kama majaribio, baadae tulitoa bilioni 6 na sasa hivi tumetoa shilingi bilioni 8.9,” amesema.

spot_img

Latest articles

Ofisi ya Msajili wa Hazina yafanya mazungumzo na Balozi wa China

Na Mwandishi wa OMH, Dar es Salaam OFISI ya Msajili wa Hazina imekutana na kufanya...

Rais Samia aunda Tume ya Uchunguzi wa Kijinai ghasia za Oktoba 29

Na Mwandishi Wetu RAIS Samia Suluhu Hassan, ameunda Tume ya Uchunguzi wa Kijinai wa matukio...

Tanesco yatakiwa kubuni teknolojia mpya kuboresha huduma kwa wateja

Na Mwandishi Wetu NAIBU Waziri wa Nishati, Salome Makamba, ameielekeza TANESCO kuendelea kufanya tafiti...

DAWASA yaja na operesheni siku 90 kudhibiti upotevu wa maji

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)...

More like this

Ofisi ya Msajili wa Hazina yafanya mazungumzo na Balozi wa China

Na Mwandishi wa OMH, Dar es Salaam OFISI ya Msajili wa Hazina imekutana na kufanya...

Rais Samia aunda Tume ya Uchunguzi wa Kijinai ghasia za Oktoba 29

Na Mwandishi Wetu RAIS Samia Suluhu Hassan, ameunda Tume ya Uchunguzi wa Kijinai wa matukio...

Tanesco yatakiwa kubuni teknolojia mpya kuboresha huduma kwa wateja

Na Mwandishi Wetu NAIBU Waziri wa Nishati, Salome Makamba, ameielekeza TANESCO kuendelea kufanya tafiti...