Muigizaji maarufu Korea Kusini, Kim Sae-ron akutwa amefariki nyumbani kwake

Na Mwandishi Wetu

TASNIA ya filamu na burudani Korea Kusini imepata pigo baada ya taarifa za kifo cha mwigizaji maarufu Kim Sae-ron (24) aliyefariki dunia nyumbani kwake jijini Seoul.

Kwa mujibu wa vyombo vya usalama nchini humo, mwili wa msanii huyo uligunduliwa na rafiki yake jana Jumapili Februari 16, 2025 na kutoa taarifa Polisi.

Polisi wamesema kuwa uchunguzi wa awali haujaonyesha dalili za uhalifu, lakini wanaendelea kuchunguza mazingira ya kifo chake.

Kim alizaliwa Julai 31, 2000, na alianza safari yake ya sanaa akiwa na umri wa miaka tisa kupitia filamu A Brand New Life (2009), ambayo ilimpatia umaarufu mkubwa.

Aidha aliendelea kung’ara zaidi kupitia filamu The Man from Nowhere (2010), ambayo ilimfanya kuwa miongoni mwa waigizaji chipukizi wenye mvuto mkubwa katika tasnia ya filamu ya Korea Kusini.

Katika miaka iliyofuata, alishiriki katika filamu zingine kubwa kama ‘A Girl at My Door’ (2014) na tamthilia za televisheni zikiwemo ‘Secret Healer na Leverage’.

spot_img

Latest articles

Dk. Nchimbi: Uhuru wa Mahakama situmike kuficha uzembe

Na Mwandishi Wetu MAKAMU wa Rais Dk. Emmanuel Nchimbi ametoa rai kwa Majaji na Mahakimu...

Rais Samia kushiriki mkutano wa WGS 2026

Na Mwandishi Wetu RAIS Samia Suluhu Hassan ameondoka nchini leo Februari 2, 2026 kwenda...

Yanga yaingilia ugomvi wa Mangungu na mshabiki Simba

Na Mwandishi Wetu UONGOZI wa Klabu ya Yanga umesema umesikitishwa na kitendo cha vurugu alichofanyiwa...

Watanzania Watakiwa Kujitokeza Kuomba Nafasi 1,150 za Udereva Qatar

Na Mwandishi Wetu WATANZANIA wametakiwa kujitokeza kwa wingi kuchangamkia fursa ya ajira iliyotangazwa na...

More like this

Dk. Nchimbi: Uhuru wa Mahakama situmike kuficha uzembe

Na Mwandishi Wetu MAKAMU wa Rais Dk. Emmanuel Nchimbi ametoa rai kwa Majaji na Mahakimu...

Rais Samia kushiriki mkutano wa WGS 2026

Na Mwandishi Wetu RAIS Samia Suluhu Hassan ameondoka nchini leo Februari 2, 2026 kwenda...

Yanga yaingilia ugomvi wa Mangungu na mshabiki Simba

Na Mwandishi Wetu UONGOZI wa Klabu ya Yanga umesema umesikitishwa na kitendo cha vurugu alichofanyiwa...