Muigizaji maarufu Korea Kusini, Kim Sae-ron akutwa amefariki nyumbani kwake

Na Mwandishi Wetu

TASNIA ya filamu na burudani Korea Kusini imepata pigo baada ya taarifa za kifo cha mwigizaji maarufu Kim Sae-ron (24) aliyefariki dunia nyumbani kwake jijini Seoul.

Kwa mujibu wa vyombo vya usalama nchini humo, mwili wa msanii huyo uligunduliwa na rafiki yake jana Jumapili Februari 16, 2025 na kutoa taarifa Polisi.

Polisi wamesema kuwa uchunguzi wa awali haujaonyesha dalili za uhalifu, lakini wanaendelea kuchunguza mazingira ya kifo chake.

Kim alizaliwa Julai 31, 2000, na alianza safari yake ya sanaa akiwa na umri wa miaka tisa kupitia filamu A Brand New Life (2009), ambayo ilimpatia umaarufu mkubwa.

Aidha aliendelea kung’ara zaidi kupitia filamu The Man from Nowhere (2010), ambayo ilimfanya kuwa miongoni mwa waigizaji chipukizi wenye mvuto mkubwa katika tasnia ya filamu ya Korea Kusini.

Katika miaka iliyofuata, alishiriki katika filamu zingine kubwa kama ‘A Girl at My Door’ (2014) na tamthilia za televisheni zikiwemo ‘Secret Healer na Leverage’.

spot_img

Latest articles

Natoa nishani ya uthubutu kwa Kanisa Katoliki 2025

Siyo hulka yangu kujadili masuala ya dini katika chambuzi ninazofanya. Wala, sikusudii kujikita kuibua...

Benki ya CRDB yafunga mwaka kwa kukabidhi zawadi ya magari kwa washindi wa Simbanking

Na Mwandishi Wetu BENKI ya CRDB, imemkabidhi Deo Ferdinand Mlawa na wenzake watano zawadi...

SMZ yapongeza udhamini mnono wa NMB Mapinduzi Cup

Na Mwandishi Wetu, Zanzibar SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ), imeipongeza Benki ya NMB kwa...

Mwakinyo ashinda kwa K.O, afichua siri

Na Winfrida Mtoi Bondia wa ngumi za kulipwa nchini, Hassan Mwakinyo ameibuka mshindi kwa K.O...

More like this

Natoa nishani ya uthubutu kwa Kanisa Katoliki 2025

Siyo hulka yangu kujadili masuala ya dini katika chambuzi ninazofanya. Wala, sikusudii kujikita kuibua...

Benki ya CRDB yafunga mwaka kwa kukabidhi zawadi ya magari kwa washindi wa Simbanking

Na Mwandishi Wetu BENKI ya CRDB, imemkabidhi Deo Ferdinand Mlawa na wenzake watano zawadi...

SMZ yapongeza udhamini mnono wa NMB Mapinduzi Cup

Na Mwandishi Wetu, Zanzibar SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ), imeipongeza Benki ya NMB kwa...