Muigizaji maarufu Korea Kusini, Kim Sae-ron akutwa amefariki nyumbani kwake

Na Mwandishi Wetu

TASNIA ya filamu na burudani Korea Kusini imepata pigo baada ya taarifa za kifo cha mwigizaji maarufu Kim Sae-ron (24) aliyefariki dunia nyumbani kwake jijini Seoul.

Kwa mujibu wa vyombo vya usalama nchini humo, mwili wa msanii huyo uligunduliwa na rafiki yake jana Jumapili Februari 16, 2025 na kutoa taarifa Polisi.

Polisi wamesema kuwa uchunguzi wa awali haujaonyesha dalili za uhalifu, lakini wanaendelea kuchunguza mazingira ya kifo chake.

Kim alizaliwa Julai 31, 2000, na alianza safari yake ya sanaa akiwa na umri wa miaka tisa kupitia filamu A Brand New Life (2009), ambayo ilimpatia umaarufu mkubwa.

Aidha aliendelea kung’ara zaidi kupitia filamu The Man from Nowhere (2010), ambayo ilimfanya kuwa miongoni mwa waigizaji chipukizi wenye mvuto mkubwa katika tasnia ya filamu ya Korea Kusini.

Katika miaka iliyofuata, alishiriki katika filamu zingine kubwa kama ‘A Girl at My Door’ (2014) na tamthilia za televisheni zikiwemo ‘Secret Healer na Leverage’.

spot_img

Latest articles

Watahiniwa 595,816 kuanza Mtihani wa Kidato cha Nne kesho

Na Tatu Mohamed JUMLA ya watahiniwa 595,816 wamesajiliwa kufanya Mtihani wa Kidato cha Nne 2025...

Tume kuundwa kuchunguza vurugu zilizotokea Oktoba 29, mwaka huu

Na Mwandishi Wetu  RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametangaza...

Mkakati wa Mawasiliano wa Nishati Safi ya kupikia: Dira ya Mafanikio ya Taifa

Na Mwandishi Wetu IMEELEZWA kuwa Mkakati wa Mawasiliano wa Nishati Safi ya Kupikia ni...

JKT Queens na matumaini nusu  fainali CAFWCL mbele ya TP Mazembe

Na Mwandishi Wetu Baada ya timu ya JKT Queens kutoa sare mbili mfululizo Ligi ya...

More like this

Watahiniwa 595,816 kuanza Mtihani wa Kidato cha Nne kesho

Na Tatu Mohamed JUMLA ya watahiniwa 595,816 wamesajiliwa kufanya Mtihani wa Kidato cha Nne 2025...

Tume kuundwa kuchunguza vurugu zilizotokea Oktoba 29, mwaka huu

Na Mwandishi Wetu  RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametangaza...

Mkakati wa Mawasiliano wa Nishati Safi ya kupikia: Dira ya Mafanikio ya Taifa

Na Mwandishi Wetu IMEELEZWA kuwa Mkakati wa Mawasiliano wa Nishati Safi ya Kupikia ni...