Muigizaji maarufu Korea Kusini, Kim Sae-ron akutwa amefariki nyumbani kwake

Na Mwandishi Wetu

TASNIA ya filamu na burudani Korea Kusini imepata pigo baada ya taarifa za kifo cha mwigizaji maarufu Kim Sae-ron (24) aliyefariki dunia nyumbani kwake jijini Seoul.

Kwa mujibu wa vyombo vya usalama nchini humo, mwili wa msanii huyo uligunduliwa na rafiki yake jana Jumapili Februari 16, 2025 na kutoa taarifa Polisi.

Polisi wamesema kuwa uchunguzi wa awali haujaonyesha dalili za uhalifu, lakini wanaendelea kuchunguza mazingira ya kifo chake.

Kim alizaliwa Julai 31, 2000, na alianza safari yake ya sanaa akiwa na umri wa miaka tisa kupitia filamu A Brand New Life (2009), ambayo ilimpatia umaarufu mkubwa.

Aidha aliendelea kung’ara zaidi kupitia filamu The Man from Nowhere (2010), ambayo ilimfanya kuwa miongoni mwa waigizaji chipukizi wenye mvuto mkubwa katika tasnia ya filamu ya Korea Kusini.

Katika miaka iliyofuata, alishiriki katika filamu zingine kubwa kama ‘A Girl at My Door’ (2014) na tamthilia za televisheni zikiwemo ‘Secret Healer na Leverage’.

spot_img

Latest articles

2020 Vunjo primaries leader to challenge Dr. Kimei again

Enock Koola (35), a staunch member of the ruling Chama Cha Mapinduzi (CCM) party...

Makamu wa Rais atoa wito uboreshaji mfumo wa fedha

Na Mwandishi Wetu Makamu wa Rais Dk. Philip Mpango ametoa wito wa kufanyika maboresho ya...

Esther Bulaya: Nilikuwa Chadema kwa mkopo nimerejea, CCM ni kama  Barcelona 

Na Mwandishi Wetu Aliyekuwa Mbunge wa viti maalumu kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema),...

Kihongosi aahidi kutekeleza alichoagizwa na Rais Samia  Arusha

Na Mwandishi Wetu  Mkuu mpya wa Mkoa wa Arusha,  Kenani Kihongosi amesema  atafanya kazi aliyotumwa na Rais...

More like this

2020 Vunjo primaries leader to challenge Dr. Kimei again

Enock Koola (35), a staunch member of the ruling Chama Cha Mapinduzi (CCM) party...

Makamu wa Rais atoa wito uboreshaji mfumo wa fedha

Na Mwandishi Wetu Makamu wa Rais Dk. Philip Mpango ametoa wito wa kufanyika maboresho ya...

Esther Bulaya: Nilikuwa Chadema kwa mkopo nimerejea, CCM ni kama  Barcelona 

Na Mwandishi Wetu Aliyekuwa Mbunge wa viti maalumu kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema),...