Rais Samia kufanya ziara nchini Ethiopia, kushiriki Mkutano wa Au

Na Mwandishi Wetu

RAIS wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan anatarajia kufanya ziara ya kikazi Addis Ababa nchini Ethiopia kuanzia leo Februari 14 hadi 16 kushiriki mkutano wa kawaida wa 38 wa Nchi na serikali wa Umoja wa Afrika (AU).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Sharifa Nyanga, imeeleza kuwa mkutano huo unatarajia kuchagua mwenyekiti mpya wa AU kwa mwaka 2025 atakayechukua nafasi ya mwenyekiti wa sasa Jamhuri ya Kiislamu ya Mauritania.

Pia, mkutano huo pia utachagua viongozi wapya wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika ikiwemo mwenyekiti, makamu mwenyekiti na makamishna sita.

“Aidha, mkutano huo pia utachagua viongozi wapya wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika ikiwemo Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti na Makamishna 6.

“Vilevile, Mkutano utajadili Taarifa ya Ushiriki wa Umoja wa Afrika kwenye Mkutano wa Nchi Tajiri Duniani (G20), Utekelezaji wa Ajenda 2063 ya Umoja wa Afrika na Taarifa kuhusu masuala ya mabadiliko ya tabianchi,” imeeleza taarifa hiyo.

Imeongeza kuwa mbali na masuala hayo, Mkutano utajadili Ajenda kuhusu Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia iliyopendekezwa na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

“Kabla ya kushiriki Mkutano wa 38, Rais Dkt. Samia atashiriki Mkutano wa Baraza la Amani na Usalama la Umoja wa Afrika utakaofanyika Februari 14,

spot_img

Latest articles

Papa mpya apatikana ni Robert Prevost

Na Mwandishi Wetu Papa Mpya wa Kanisa Katoliki Duniani, ametangazwa ni Kardinali Robert Francis Prevost(69),...

Waziri Masauni, Umoja wa Ulaya wajadili Mazingira

Mwandishi Maalum-Denmark Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhandisi Hamad...

Serikali yasamehe faini za maji, yataka wananchi warejeshewe huduma

Na Mwandishi Wetu Waziri wa Maji, Jumaa Aweso ametangaza msamaha wa faini zote kwa wananchi...

Spika wa Bunge ateta na Dk. Mwapinga, amhakikishia ushirikiano

Na Mwandishi Wetu Spika wa Bunge la Tanzania na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani...

More like this

Papa mpya apatikana ni Robert Prevost

Na Mwandishi Wetu Papa Mpya wa Kanisa Katoliki Duniani, ametangazwa ni Kardinali Robert Francis Prevost(69),...

Waziri Masauni, Umoja wa Ulaya wajadili Mazingira

Mwandishi Maalum-Denmark Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhandisi Hamad...

Serikali yasamehe faini za maji, yataka wananchi warejeshewe huduma

Na Mwandishi Wetu Waziri wa Maji, Jumaa Aweso ametangaza msamaha wa faini zote kwa wananchi...