AJALI YAAHIRISHA MCHEZO WA SIMBA, DODOMA JIJI

Na Mwandishi Wetu

Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB), imeahirisha   mchezo Ligi Kuu Tanzania Bara  kati ya  Simba na Dodoma Jiji uliopangwa kuchezwa  Februari 15, 2025 katika Uwanja wa KMC Complex, Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa taarifa ya bodi hiyo, kuahirisha mchezo huo kumetokana na hali ya kiafya ya maofisa na wachezaji wa Dodoma Jiji kutokuwa nzuri baada ya ajali ya basi waliyopata wakati wakisafiri kutokea Ruangwa mkoani Lindi.

“Ajali hiyo imesababisha athari hasi kwa klabu ya Dodoma Jiji kwa kuchelewesha safari yake ya kuelekea mkoani Dar es Salaam pamoja na kuathiri maandalizi ya kiufundi kwa kuwakosa wachezaji na maofisa wa ufundi ambao walipata majeraha katika ajali hiyo. Bodi itatangaza tarehe mpya ya mchezo huo hivi karibuni,” imesema taarifa hiyo.

Aidha kwa upande wa taarifa ya klabu ya Dodoma Jiji, kikosi hicho kimewasili salama jijini Dodoma na  ambapo taratibu za kitabibu zitaendelea kwa majeruhi wote katika Hosptali ya Benjamin Mkapa. 

Dodoma Jiji ilipata ajali Februari 10, 2025 baada ya basi walikuwa wakisafiria kutumbukia mtoni katikati ya Nangurukuru na Somanga.

spot_img

Latest articles

Wachezaji volleyball nchini watakiwa kujituma kuwavutia mawakala wa kimataifa

Na Mwandishi Wetu WACHEZAJI wa mpira wa wavu 'volleyball' wanaoshiriki Ligi ya Mkoa wa Dar...

TANESCO YAFUNGUA UKURASA MPYA WA MATUMIZI YA UMEME NCHINI

📍Yazindua vituo vya kuchajia vyombo vya usafiri vinavyotumia umeme 📍Wananchi kunufaika na mpango wa ukopeshaji...

Tusimamie sera ya kutofungamana, pia uwajibikaji matukio ya Oktoba 29

SIJAWAHI kuwa msemaji wa serikali, hivyo sina utaratibu wa kuizungumzia au kuisemea. Siyo jukumu...

DAWASA, Madiwani waja na suluhisho changamoto ya maji Ubungo

Na Mwandishi Wetu Madiwani wa Manispaa ya Ubungo wamekubaliana kwa kauli moja na Mamlaka ya...

More like this

Wachezaji volleyball nchini watakiwa kujituma kuwavutia mawakala wa kimataifa

Na Mwandishi Wetu WACHEZAJI wa mpira wa wavu 'volleyball' wanaoshiriki Ligi ya Mkoa wa Dar...

TANESCO YAFUNGUA UKURASA MPYA WA MATUMIZI YA UMEME NCHINI

📍Yazindua vituo vya kuchajia vyombo vya usafiri vinavyotumia umeme 📍Wananchi kunufaika na mpango wa ukopeshaji...

Tusimamie sera ya kutofungamana, pia uwajibikaji matukio ya Oktoba 29

SIJAWAHI kuwa msemaji wa serikali, hivyo sina utaratibu wa kuizungumzia au kuisemea. Siyo jukumu...