AJALI YAAHIRISHA MCHEZO WA SIMBA, DODOMA JIJI

Na Mwandishi Wetu

Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB), imeahirisha   mchezo Ligi Kuu Tanzania Bara  kati ya  Simba na Dodoma Jiji uliopangwa kuchezwa  Februari 15, 2025 katika Uwanja wa KMC Complex, Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa taarifa ya bodi hiyo, kuahirisha mchezo huo kumetokana na hali ya kiafya ya maofisa na wachezaji wa Dodoma Jiji kutokuwa nzuri baada ya ajali ya basi waliyopata wakati wakisafiri kutokea Ruangwa mkoani Lindi.

“Ajali hiyo imesababisha athari hasi kwa klabu ya Dodoma Jiji kwa kuchelewesha safari yake ya kuelekea mkoani Dar es Salaam pamoja na kuathiri maandalizi ya kiufundi kwa kuwakosa wachezaji na maofisa wa ufundi ambao walipata majeraha katika ajali hiyo. Bodi itatangaza tarehe mpya ya mchezo huo hivi karibuni,” imesema taarifa hiyo.

Aidha kwa upande wa taarifa ya klabu ya Dodoma Jiji, kikosi hicho kimewasili salama jijini Dodoma na  ambapo taratibu za kitabibu zitaendelea kwa majeruhi wote katika Hosptali ya Benjamin Mkapa. 

Dodoma Jiji ilipata ajali Februari 10, 2025 baada ya basi walikuwa wakisafiria kutumbukia mtoni katikati ya Nangurukuru na Somanga.

spot_img

Latest articles

Rais Samia: Serikali itachukua hatua yaliyopendekezwa na CAG

Na Mwandishi Wetu RAIS Samia Suluhu Hassan amesema Serikali itachukua hatua kama ilivyoelekezwa na sheria...

TAFF yajipanga kwa Ligi Kuu, Tabora yaanzisha timu

Na Mwandishi Wetu MKURUGENZI wa ufundi Shirikisho la Mpira wa Miguu kwa Watu wenye Ulemavu...

Bwege afariki dunia

Na Mwandishi Wetu MBUNGE wa zamani wa Jimbo la Kilwa Kusini, Mkoani Lindi, Selemani Bungara...

Ripoti ya CAG yaibua mazito ujenzi wa uwanja wa AFCON Arusha

Na Mwandishi Wetu RIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Charles...

More like this

Rais Samia: Serikali itachukua hatua yaliyopendekezwa na CAG

Na Mwandishi Wetu RAIS Samia Suluhu Hassan amesema Serikali itachukua hatua kama ilivyoelekezwa na sheria...

TAFF yajipanga kwa Ligi Kuu, Tabora yaanzisha timu

Na Mwandishi Wetu MKURUGENZI wa ufundi Shirikisho la Mpira wa Miguu kwa Watu wenye Ulemavu...

Bwege afariki dunia

Na Mwandishi Wetu MBUNGE wa zamani wa Jimbo la Kilwa Kusini, Mkoani Lindi, Selemani Bungara...