AJALI YAAHIRISHA MCHEZO WA SIMBA, DODOMA JIJI

Na Mwandishi Wetu

Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB), imeahirisha   mchezo Ligi Kuu Tanzania Bara  kati ya  Simba na Dodoma Jiji uliopangwa kuchezwa  Februari 15, 2025 katika Uwanja wa KMC Complex, Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa taarifa ya bodi hiyo, kuahirisha mchezo huo kumetokana na hali ya kiafya ya maofisa na wachezaji wa Dodoma Jiji kutokuwa nzuri baada ya ajali ya basi waliyopata wakati wakisafiri kutokea Ruangwa mkoani Lindi.

“Ajali hiyo imesababisha athari hasi kwa klabu ya Dodoma Jiji kwa kuchelewesha safari yake ya kuelekea mkoani Dar es Salaam pamoja na kuathiri maandalizi ya kiufundi kwa kuwakosa wachezaji na maofisa wa ufundi ambao walipata majeraha katika ajali hiyo. Bodi itatangaza tarehe mpya ya mchezo huo hivi karibuni,” imesema taarifa hiyo.

Aidha kwa upande wa taarifa ya klabu ya Dodoma Jiji, kikosi hicho kimewasili salama jijini Dodoma na  ambapo taratibu za kitabibu zitaendelea kwa majeruhi wote katika Hosptali ya Benjamin Mkapa. 

Dodoma Jiji ilipata ajali Februari 10, 2025 baada ya basi walikuwa wakisafiria kutumbukia mtoni katikati ya Nangurukuru na Somanga.

spot_img

Latest articles

TANZANIA YAZIDI KUIMARISHA NAFASI YAKE KATIKA BIASHARA YA UMEME KIKANDA

Na Mwandishi Wetu, Zanzibar TANZANIA imeendelea kuimarisha nafasi yake katika biashara ya umeme kikanda, huku...

MRADI WA NJIA YA KUSAFIRISHA UMEME WA KV 220 IGANJO–SAZA KUIMARISHA UPATIKANAJI WA UMEME NA KUCHOCHEA UCHIMBAJI WA MADINI – MHE. SALOME

📌 Ashuhudia utiaji saini mkataba wa utekelezaji wa mradi kutoka Iganjo, Mbeya hadi Saza,...

Salome Ashuhudia utiaji saini mkataba wa sh. bilioni 198 kuimarisha umeme Songwe, Chunya

📌Ataka kasi ya utekelezaji wa mradi na wazawa kupewa kipaumbele 📌Wachimbaji wapongeza Na Mwandishi Wetu NAIBU...

ZARA TANZANIA ADVENTURES YAZINDUA RASMI KAMPENI YA TWENZETU KILELENI MSIMU WA TANO

KAMPUNI ya Zara Tanzania Adventures imezindua rasmi kampeni ya Twenzetu Kileleni – Msimu wa...

More like this

TANZANIA YAZIDI KUIMARISHA NAFASI YAKE KATIKA BIASHARA YA UMEME KIKANDA

Na Mwandishi Wetu, Zanzibar TANZANIA imeendelea kuimarisha nafasi yake katika biashara ya umeme kikanda, huku...

MRADI WA NJIA YA KUSAFIRISHA UMEME WA KV 220 IGANJO–SAZA KUIMARISHA UPATIKANAJI WA UMEME NA KUCHOCHEA UCHIMBAJI WA MADINI – MHE. SALOME

📌 Ashuhudia utiaji saini mkataba wa utekelezaji wa mradi kutoka Iganjo, Mbeya hadi Saza,...

Salome Ashuhudia utiaji saini mkataba wa sh. bilioni 198 kuimarisha umeme Songwe, Chunya

📌Ataka kasi ya utekelezaji wa mradi na wazawa kupewa kipaumbele 📌Wachimbaji wapongeza Na Mwandishi Wetu NAIBU...