AJALI YAAHIRISHA MCHEZO WA SIMBA, DODOMA JIJI

Na Mwandishi Wetu

Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB), imeahirisha   mchezo Ligi Kuu Tanzania Bara  kati ya  Simba na Dodoma Jiji uliopangwa kuchezwa  Februari 15, 2025 katika Uwanja wa KMC Complex, Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa taarifa ya bodi hiyo, kuahirisha mchezo huo kumetokana na hali ya kiafya ya maofisa na wachezaji wa Dodoma Jiji kutokuwa nzuri baada ya ajali ya basi waliyopata wakati wakisafiri kutokea Ruangwa mkoani Lindi.

“Ajali hiyo imesababisha athari hasi kwa klabu ya Dodoma Jiji kwa kuchelewesha safari yake ya kuelekea mkoani Dar es Salaam pamoja na kuathiri maandalizi ya kiufundi kwa kuwakosa wachezaji na maofisa wa ufundi ambao walipata majeraha katika ajali hiyo. Bodi itatangaza tarehe mpya ya mchezo huo hivi karibuni,” imesema taarifa hiyo.

Aidha kwa upande wa taarifa ya klabu ya Dodoma Jiji, kikosi hicho kimewasili salama jijini Dodoma na  ambapo taratibu za kitabibu zitaendelea kwa majeruhi wote katika Hosptali ya Benjamin Mkapa. 

Dodoma Jiji ilipata ajali Februari 10, 2025 baada ya basi walikuwa wakisafiria kutumbukia mtoni katikati ya Nangurukuru na Somanga.

spot_img

Latest articles

Sekta ya Viwanda na Biashara yazidi kutoa fursa kwa vijana

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Viwanda na Biashara, Judith Kapinga amesema sekta ya viwanda...

Polisi yachunguza tukio la kuchoma moto magari msibani

Na Mwandishi Wetu JESHI la Polisi Mkoa wa Morogoro limesema linachunguza tukio la kuchoma moto na...

Taifa Stars yakabidhiwa bendera tayari kwa AFCON 2025

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Prof. Palamagamba Kabudi, ameiaga na...

CRDB yashirikiana na Kids’ Holiday Festival kukuza elimu ya fedha kwa watoto

Na Mwandishi Wetu BENKI ya CRDB imeingia makubaliano ya ushirikiano na Kids’ Holiday Festival...

More like this

Sekta ya Viwanda na Biashara yazidi kutoa fursa kwa vijana

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Viwanda na Biashara, Judith Kapinga amesema sekta ya viwanda...

Polisi yachunguza tukio la kuchoma moto magari msibani

Na Mwandishi Wetu JESHI la Polisi Mkoa wa Morogoro limesema linachunguza tukio la kuchoma moto na...

Taifa Stars yakabidhiwa bendera tayari kwa AFCON 2025

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Prof. Palamagamba Kabudi, ameiaga na...