AJALI YAAHIRISHA MCHEZO WA SIMBA, DODOMA JIJI

Na Mwandishi Wetu

Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB), imeahirisha   mchezo Ligi Kuu Tanzania Bara  kati ya  Simba na Dodoma Jiji uliopangwa kuchezwa  Februari 15, 2025 katika Uwanja wa KMC Complex, Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa taarifa ya bodi hiyo, kuahirisha mchezo huo kumetokana na hali ya kiafya ya maofisa na wachezaji wa Dodoma Jiji kutokuwa nzuri baada ya ajali ya basi waliyopata wakati wakisafiri kutokea Ruangwa mkoani Lindi.

“Ajali hiyo imesababisha athari hasi kwa klabu ya Dodoma Jiji kwa kuchelewesha safari yake ya kuelekea mkoani Dar es Salaam pamoja na kuathiri maandalizi ya kiufundi kwa kuwakosa wachezaji na maofisa wa ufundi ambao walipata majeraha katika ajali hiyo. Bodi itatangaza tarehe mpya ya mchezo huo hivi karibuni,” imesema taarifa hiyo.

Aidha kwa upande wa taarifa ya klabu ya Dodoma Jiji, kikosi hicho kimewasili salama jijini Dodoma na  ambapo taratibu za kitabibu zitaendelea kwa majeruhi wote katika Hosptali ya Benjamin Mkapa. 

Dodoma Jiji ilipata ajali Februari 10, 2025 baada ya basi walikuwa wakisafiria kutumbukia mtoni katikati ya Nangurukuru na Somanga.

spot_img

Latest articles

Waziri wa Nishati Ndejembi azindua rasmi mita janja

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amezindua rasmi mita janja (smart meter)...

RC Kunenge: Mto Ruvu ubaki kwa matumizi ya binadamu tu, tusitishe shughuli nyingine kwa muda

Na Mwandishi Wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, ametoa wito kwa wakulima...

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...

Rais Samia: Walilenga kupindua dola

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa vurugu...

More like this

Waziri wa Nishati Ndejembi azindua rasmi mita janja

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amezindua rasmi mita janja (smart meter)...

RC Kunenge: Mto Ruvu ubaki kwa matumizi ya binadamu tu, tusitishe shughuli nyingine kwa muda

Na Mwandishi Wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, ametoa wito kwa wakulima...

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...