Mwanahabari Mkongwe Mambo Mbotela afariki dunia

Mwanahabari mkongwe nchini Kenya, Leonard Mambo Mbotela amefariki akiwa na umri wa miaka 85.

Mbotela aliyejulikana kwa kipindi chake maarufu cha Je, Huu Ni Uungwana? amefariki dunia leo Ijumaa saa 3:30 asubuhi.

Akithibitisha kifo cha Mbotela, mke wa mwanaye anayejulikana kwa jina la Anne Mbotela wa mujibu wa amesema kuwa alikuwa mgonjwa kwa muda kabla ya kuaga dunia.

Mbotela alijizolea umaarufu kwa kipindi hicho kilichokuwa kikirushwa na Shirika la Utangazaji la Kenya (KBC), ambapo alivuta hisia za watu wengi waliokuwa wakimfuatilia.

Kipindi hicho kilianza kuruka mwaka 1966, kikijikita kuhamasisha masuala mbalimbali ikiwemo maadili kimekuwa kikirushwa kupitia Televisheni ya KBC nchini humo.

Kati ya vipindi vyake vilivyopendwa ni Uhalifu Haulipi, Ongea Lugha Sanifu na Waliosifika.

spot_img

Latest articles

Serikali yaahidi kushirikiana na wadau kuendeleza mchezo wa kuogelea

Na Winfrida Mtoi WADAU wa mchezo wakuogelea Afrika Mashariki wamekutana kujadili maendeleo ya mchezo huo,...

Ndejembi: Tanesco mmefanya mageuzi makubwa katika huduma ya umeme kwa wananchi

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi, amesema kuwa Shirika la Umeme Tanzania...

Dube awapa raha wananchi

Na Winfrida Mtoi BAO pekee lililofungwa na Prince Dube dakika ya 58, limeipa Yanga alama...

Mexico yatwaa taji la Miss Universe 2025, Ivory Coast namba tano

Na Mwandishi Wetu Mexico imeibuka mshindi wa taji la Miss Universe 2025 kupitia mrembo wake...

More like this

Serikali yaahidi kushirikiana na wadau kuendeleza mchezo wa kuogelea

Na Winfrida Mtoi WADAU wa mchezo wakuogelea Afrika Mashariki wamekutana kujadili maendeleo ya mchezo huo,...

Ndejembi: Tanesco mmefanya mageuzi makubwa katika huduma ya umeme kwa wananchi

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi, amesema kuwa Shirika la Umeme Tanzania...

Dube awapa raha wananchi

Na Winfrida Mtoi BAO pekee lililofungwa na Prince Dube dakika ya 58, limeipa Yanga alama...