Mwanahabari Mkongwe Mambo Mbotela afariki dunia

Mwanahabari mkongwe nchini Kenya, Leonard Mambo Mbotela amefariki akiwa na umri wa miaka 85.

Mbotela aliyejulikana kwa kipindi chake maarufu cha Je, Huu Ni Uungwana? amefariki dunia leo Ijumaa saa 3:30 asubuhi.

Akithibitisha kifo cha Mbotela, mke wa mwanaye anayejulikana kwa jina la Anne Mbotela wa mujibu wa amesema kuwa alikuwa mgonjwa kwa muda kabla ya kuaga dunia.

Mbotela alijizolea umaarufu kwa kipindi hicho kilichokuwa kikirushwa na Shirika la Utangazaji la Kenya (KBC), ambapo alivuta hisia za watu wengi waliokuwa wakimfuatilia.

Kipindi hicho kilianza kuruka mwaka 1966, kikijikita kuhamasisha masuala mbalimbali ikiwemo maadili kimekuwa kikirushwa kupitia Televisheni ya KBC nchini humo.

Kati ya vipindi vyake vilivyopendwa ni Uhalifu Haulipi, Ongea Lugha Sanifu na Waliosifika.

spot_img

Latest articles

Rasmi Kocha Yanga afungashiwa virago usiku

Na Mwandishi Wetu Uongozi wa Klabu ya Yanga umevunja mkataba na Kocha Mkuu, Romain Folz. ...

Mwanamke ashikiliwa  Polisi kwa  kumuua mume wake na kumfukia ndani ya nyumba yao

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita linamshikilia mwanamke mmoja aliyefahamika kwa jina...

Padre aliyepotea apatikana akiwa hai

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi mkoani Ruvuma limefanikiwa kumpata Padre Camillus Nikata wa Jimbo...

More like this

Rasmi Kocha Yanga afungashiwa virago usiku

Na Mwandishi Wetu Uongozi wa Klabu ya Yanga umevunja mkataba na Kocha Mkuu, Romain Folz. ...

Mwanamke ashikiliwa  Polisi kwa  kumuua mume wake na kumfukia ndani ya nyumba yao

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita linamshikilia mwanamke mmoja aliyefahamika kwa jina...