Wasira: CCM kimbilio la wananchi, tujadili yanayowahusu

N Mwandishi Wetu, Bunda

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Stephen Wassira, amesema Chama ni kimbilio la wananchi hivyo lazima kijadili na kubeba shida za watu.

Ameagiza vikao vya Chama vizungumzie mambo yanayowahusu wananchi kwa lengo la kusikia changamoto zao na kuwa sehemu ya kupatiwa ufumbuzi.

Wasira ameyaeleza hayo mjini Bunda leo Januari 31, 2025 alipokutana na kuzungumza na wafanyabiashara na wajasiriamali wa Wilaya ya Bunda mkoani Mara.

Amesisitiza kuwa siyo sahihi vikao hivyo kujadili mambo yasiyo na maana wakati wananchi kjatika maeneo husika wanakabiliwa na changamoto ambazo endapo zitasikilizwa na kufikishwa mbele ya mamlaka husika zitapatiwa ufumbuzi.

“CCM ni lazima isikilize watu wanataka nini, sisi ni Chama cha watu na kwa kweli tunataka kiwe cha watu kwelikweli, vikao vyetu vya CCM vizungumze mambo ya watu, kama ni mambo ya wafanyabiashara wadogowadogo (machinga) tuzungumze kuhusu hilo, kama wana matatizo wakimbilie CCM kwa sababu wanajua huko ndiko kuna usalama,” amesema.

Ameongeza kuwa, ni vema vikao vianze kusikiliza machungu yanayowagusa wananchi ili kupata ufumbuzi wa changamoto zinazowakabili.

“Unajua vikao hivi wakati mwingine mnajikuta mnajizungumza wenyewe badala ya kuzungumza wafanyabiasha wana matatizo gani, mama lishe wana matatizo gani, wakulima wana matatizo gani,” amesema.

spot_img

Latest articles

Tusimamie sera ya kutofungamana, pia uwajibikaji matukio ya Oktoba 29

SIJAWAHI kuwa msemaji wa serikali, hivyo sina utaratibu wa kuizungumzia au kuisemea. Siyo jukumu...

DAWASA, Madiwani waja na suluhisho changamoto ya maji Ubungo

Na Mwandishi Wetu Madiwani wa Manispaa ya Ubungo wamekubaliana kwa kauli moja na Mamlaka ya...

Dawasa, madiwani Ubungo ziarani kutafuta suluhu ya maji

Na Mwandishi Wetu Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Mhe Albert Msando, ameongoza ziara maalum...

Mchezo wa kuogelea wazidi kupaa nchini, TSA  yafichua siri

Na Winfrida  Mtoi MCHEZO wa kuogelea umezidi kushika kasi nchini  kutokana na kuongezeka idadi ya...

More like this

Tusimamie sera ya kutofungamana, pia uwajibikaji matukio ya Oktoba 29

SIJAWAHI kuwa msemaji wa serikali, hivyo sina utaratibu wa kuizungumzia au kuisemea. Siyo jukumu...

DAWASA, Madiwani waja na suluhisho changamoto ya maji Ubungo

Na Mwandishi Wetu Madiwani wa Manispaa ya Ubungo wamekubaliana kwa kauli moja na Mamlaka ya...

Dawasa, madiwani Ubungo ziarani kutafuta suluhu ya maji

Na Mwandishi Wetu Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Mhe Albert Msando, ameongoza ziara maalum...