Wasira: CCM kimbilio la wananchi, tujadili yanayowahusu

N Mwandishi Wetu, Bunda

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Stephen Wassira, amesema Chama ni kimbilio la wananchi hivyo lazima kijadili na kubeba shida za watu.

Ameagiza vikao vya Chama vizungumzie mambo yanayowahusu wananchi kwa lengo la kusikia changamoto zao na kuwa sehemu ya kupatiwa ufumbuzi.

Wasira ameyaeleza hayo mjini Bunda leo Januari 31, 2025 alipokutana na kuzungumza na wafanyabiashara na wajasiriamali wa Wilaya ya Bunda mkoani Mara.

Amesisitiza kuwa siyo sahihi vikao hivyo kujadili mambo yasiyo na maana wakati wananchi kjatika maeneo husika wanakabiliwa na changamoto ambazo endapo zitasikilizwa na kufikishwa mbele ya mamlaka husika zitapatiwa ufumbuzi.

“CCM ni lazima isikilize watu wanataka nini, sisi ni Chama cha watu na kwa kweli tunataka kiwe cha watu kwelikweli, vikao vyetu vya CCM vizungumze mambo ya watu, kama ni mambo ya wafanyabiashara wadogowadogo (machinga) tuzungumze kuhusu hilo, kama wana matatizo wakimbilie CCM kwa sababu wanajua huko ndiko kuna usalama,” amesema.

Ameongeza kuwa, ni vema vikao vianze kusikiliza machungu yanayowagusa wananchi ili kupata ufumbuzi wa changamoto zinazowakabili.

“Unajua vikao hivi wakati mwingine mnajikuta mnajizungumza wenyewe badala ya kuzungumza wafanyabiasha wana matatizo gani, mama lishe wana matatizo gani, wakulima wana matatizo gani,” amesema.

spot_img

Latest articles

Kamati ya Bunge Nishati na Madini yaridhishwa na hali ya uzalishaji umeme

📌Yasema jumla ya megawati 4,400 za umeme zinazalishwa kupitia vyanzo mbalimbali 📌Yaipongeza TANESCO...

Rais Samia atoa salamu za Rambirambi kwa kifo cha Kardinali Pengo

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, ametuma...

Kardinali Polycarp Pengo Afariki Dunia

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam,...

TIRDO yapongezwa, yaagizwa kujitangaza zaidi

Na Tatu Mohamed KATIBU Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Balozi Waziri Salum,...

More like this

Kamati ya Bunge Nishati na Madini yaridhishwa na hali ya uzalishaji umeme

📌Yasema jumla ya megawati 4,400 za umeme zinazalishwa kupitia vyanzo mbalimbali 📌Yaipongeza TANESCO...

Rais Samia atoa salamu za Rambirambi kwa kifo cha Kardinali Pengo

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, ametuma...

Kardinali Polycarp Pengo Afariki Dunia

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam,...