Wasira: CCM kimbilio la wananchi, tujadili yanayowahusu

N Mwandishi Wetu, Bunda

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Stephen Wassira, amesema Chama ni kimbilio la wananchi hivyo lazima kijadili na kubeba shida za watu.

Ameagiza vikao vya Chama vizungumzie mambo yanayowahusu wananchi kwa lengo la kusikia changamoto zao na kuwa sehemu ya kupatiwa ufumbuzi.

Wasira ameyaeleza hayo mjini Bunda leo Januari 31, 2025 alipokutana na kuzungumza na wafanyabiashara na wajasiriamali wa Wilaya ya Bunda mkoani Mara.

Amesisitiza kuwa siyo sahihi vikao hivyo kujadili mambo yasiyo na maana wakati wananchi kjatika maeneo husika wanakabiliwa na changamoto ambazo endapo zitasikilizwa na kufikishwa mbele ya mamlaka husika zitapatiwa ufumbuzi.

“CCM ni lazima isikilize watu wanataka nini, sisi ni Chama cha watu na kwa kweli tunataka kiwe cha watu kwelikweli, vikao vyetu vya CCM vizungumze mambo ya watu, kama ni mambo ya wafanyabiashara wadogowadogo (machinga) tuzungumze kuhusu hilo, kama wana matatizo wakimbilie CCM kwa sababu wanajua huko ndiko kuna usalama,” amesema.

Ameongeza kuwa, ni vema vikao vianze kusikiliza machungu yanayowagusa wananchi ili kupata ufumbuzi wa changamoto zinazowakabili.

“Unajua vikao hivi wakati mwingine mnajikuta mnajizungumza wenyewe badala ya kuzungumza wafanyabiasha wana matatizo gani, mama lishe wana matatizo gani, wakulima wana matatizo gani,” amesema.

spot_img

Latest articles

Jeshi la Polisi latoa onyo wanaondelea kuhamasisha maandamano

Na Mwandishi Wetu JESHI la Polisi nchini limesema  kwa kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi...

Watanzania waaswa kudumisha amani, Umoja na mshikamano

Na Mwandishi Wetu KATIKA kuadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Tanganyika, Watanzania wametakiwa kukumbuka...

Serikali kuanzisha Kituo Maalum cha Wawekezaji Vijana

Na Tatu Mohamed SERIKALI inatarajia kuanzisha kituo Maalum cha kuhudumia na kuwezesha wawekezaji vijana(Youth Investors...

Mnyama Simba afia kwa Mkapa, Yanga, Azam kicheko

Na Winfrida Mtoi LIGI Kuu Tanzania Bara imeendelea leo Novemba 7, 2025 kwa michezo miwili...

More like this

Jeshi la Polisi latoa onyo wanaondelea kuhamasisha maandamano

Na Mwandishi Wetu JESHI la Polisi nchini limesema  kwa kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi...

Watanzania waaswa kudumisha amani, Umoja na mshikamano

Na Mwandishi Wetu KATIKA kuadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Tanganyika, Watanzania wametakiwa kukumbuka...

Serikali kuanzisha Kituo Maalum cha Wawekezaji Vijana

Na Tatu Mohamed SERIKALI inatarajia kuanzisha kituo Maalum cha kuhudumia na kuwezesha wawekezaji vijana(Youth Investors...