Wasira: CCM kimbilio la wananchi, tujadili yanayowahusu

N Mwandishi Wetu, Bunda

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Stephen Wassira, amesema Chama ni kimbilio la wananchi hivyo lazima kijadili na kubeba shida za watu.

Ameagiza vikao vya Chama vizungumzie mambo yanayowahusu wananchi kwa lengo la kusikia changamoto zao na kuwa sehemu ya kupatiwa ufumbuzi.

Wasira ameyaeleza hayo mjini Bunda leo Januari 31, 2025 alipokutana na kuzungumza na wafanyabiashara na wajasiriamali wa Wilaya ya Bunda mkoani Mara.

Amesisitiza kuwa siyo sahihi vikao hivyo kujadili mambo yasiyo na maana wakati wananchi kjatika maeneo husika wanakabiliwa na changamoto ambazo endapo zitasikilizwa na kufikishwa mbele ya mamlaka husika zitapatiwa ufumbuzi.

“CCM ni lazima isikilize watu wanataka nini, sisi ni Chama cha watu na kwa kweli tunataka kiwe cha watu kwelikweli, vikao vyetu vya CCM vizungumze mambo ya watu, kama ni mambo ya wafanyabiashara wadogowadogo (machinga) tuzungumze kuhusu hilo, kama wana matatizo wakimbilie CCM kwa sababu wanajua huko ndiko kuna usalama,” amesema.

Ameongeza kuwa, ni vema vikao vianze kusikiliza machungu yanayowagusa wananchi ili kupata ufumbuzi wa changamoto zinazowakabili.

“Unajua vikao hivi wakati mwingine mnajikuta mnajizungumza wenyewe badala ya kuzungumza wafanyabiasha wana matatizo gani, mama lishe wana matatizo gani, wakulima wana matatizo gani,” amesema.

spot_img

Latest articles

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu  ajiuzulu TEF

Na Mwandishi Wetu MKURUGENZI wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Bakari Machumu amejiuzulu nafasi ya makamu...

Wanariadha Wanawake 155 kukiwasha kwa Mkapa Nov 29

Na Winfrida Mtoi Jumla ya wanariadha wanawake 155, wanatarajiwa kushiriki katika msimu wa saba wa...

Waziri Mkuu atoa sababu yakutotaja idadi vifo vilivyotokea Oktoba 29

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amesema ni muhimu watanzania kutanguliza utu na...

Niffer arudishwa gerezani, 20 kesi ya uhaini waachiwa huru

Na Mwandishi Wetu Watuhumiwa 20 kati ya 22 waliokuwa wanashtakiwa kwa makosa ya uhaini wameachiwa...

More like this

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu  ajiuzulu TEF

Na Mwandishi Wetu MKURUGENZI wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Bakari Machumu amejiuzulu nafasi ya makamu...

Wanariadha Wanawake 155 kukiwasha kwa Mkapa Nov 29

Na Winfrida Mtoi Jumla ya wanariadha wanawake 155, wanatarajiwa kushiriki katika msimu wa saba wa...

Waziri Mkuu atoa sababu yakutotaja idadi vifo vilivyotokea Oktoba 29

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amesema ni muhimu watanzania kutanguliza utu na...