SADC kukutana leo kujadili vita DRC

Na Mwandishi Wetu

VIONGOZI wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) wanatarajiwa kukutana leo huko Harare, Zimbabwe kwa mkutano maalum kujadili vita vinavyoendelea nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).

Mkutano huu unafanyika huku vikosi vya kijeshi vya kikanda, vinavyoshirikiana na vikosi vya ulinzi vya Congo, vikiripotiwa kupata majeruhi baada ya waasi kuchukua sehemu ya mji wa Goma mashariki mwa DRC.

Viongozi wanatarajiwa kujadili jinsi ya kumaliza mvutano katika eneo la mashariki mwa Congo, na mustakabali wa operesheni za kijeshi za SADC katika eneo hilo. Zimbabwe, kama mwenyeji wa mkutano, imeonyesha wasiwasi kwamba mzozo huu unaweza kuathiri nchi wanachama wa SADC.

Wanajeshi kutoka Afrika Kusini, Malawi, na Tanzania wameuawa katika mapigano dhidi ya waasi wa M23.

Hali ya mawasiliano inazidi kuwa tete, huku Umoja wa Mataifa ukishutumu Rwanda kwa kusaidia waasi wa mashariki mwa DRC, madai ambayo Rwanda imeyakanusha.

Chanzo: Dw

spot_img

Latest articles

CRDB yazindua msimu wa nne wa Zogo Mchongo, yasisitiza elimu ya fedha na matumizi ya teknolojia kukuza uchumi

Na Tatu Mohamed BENKI ya CRDB imezindua rasmi msimu wa nne wa kipindi cha Zogo...

WAZIRI NDEJEMBI ATOA ONYO KWA MKANDARASI ANAYETEKELEZA MRADI WA SONGEA–TUNDURU–MASASI

📌 Asema ucheleweshaji wa mradi hauendani na matarajio ya Serikali na wananchi. 📌 Amuagiza mkandarasi...

Taasisi za umma zatakiwa kuachana na utendaji wa mazoea ili kufanikisha Dira 2050

Na Mwandishi Wetu SERIKALI imezitaka Taasisi, Mashirika ya Umma na Wakala za Serikali kuachana...

NEWALA KUNUFAIKA NA UMEME WA UHAKIKA

📌*Ni baada ya kukamilika kwa njia ya kusafirisha umeme ya kilovoti 33 Masasi -...

More like this

CRDB yazindua msimu wa nne wa Zogo Mchongo, yasisitiza elimu ya fedha na matumizi ya teknolojia kukuza uchumi

Na Tatu Mohamed BENKI ya CRDB imezindua rasmi msimu wa nne wa kipindi cha Zogo...

WAZIRI NDEJEMBI ATOA ONYO KWA MKANDARASI ANAYETEKELEZA MRADI WA SONGEA–TUNDURU–MASASI

📌 Asema ucheleweshaji wa mradi hauendani na matarajio ya Serikali na wananchi. 📌 Amuagiza mkandarasi...

Taasisi za umma zatakiwa kuachana na utendaji wa mazoea ili kufanikisha Dira 2050

Na Mwandishi Wetu SERIKALI imezitaka Taasisi, Mashirika ya Umma na Wakala za Serikali kuachana...