TANZANIA NA SOMALIA KUBADILISHANA WAFUNGWA

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

SERIKALI ya Tanzania na Somalia zimesaini mikataba miwili ya makubaliano ya kushirikiana katika masuala ya ulinzi na usalama na kubadilishana wafungwa.

Mikataba hiyo imesainiwa leo Januari 29, 2025 jijini Dar es Salaam na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa kwa upande wa Tanzania na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Ahmed Moalim Fiqi kwa upande wa Somalia.

Akizungumza baada ya kusaini mikataba hiyo, Bashungwa amesema mkataba wa kubadilishana wafungwa utaziwezesha nchi hizo mbili kuruhusu wafungwa waweze kutumikia adhabu katika nchi zao na kusaidia kupunguza gharama za kifedha za kuwahudumia wafungwa hao.

“Inapotokea kuna Watanzania wenzetu wameingia katika hali ya kuwa wafungwa wakiwa kule Somalia, kupitia mkataba tuliosaini utatuwezesha kuwachukuwa Watanzania kuwaleta kwenye magereza yetu, vile vile kwa wafungwa wa Somalia watarudishwa kuendelea na vifungo vyao nchini kwao,” ameeleza.

Aidha, Bashungwa amesema mkataba wa ushirikiano kuhusu ulinzi na usalama, unalenga kuimarisha uwezo vyombo vya usalama kwa kutoa mafunzo kwa Askari wa pande zote mbili, kutekeleza operesheni za pamoja, kubadilishana utaalam katika masuala ya usalama na ulinzi pamoja na kubadilishana taarifa za kiintelijensia.

Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Said Mussa amesema utiaji saini wa mikataba hiyo ni utekelezaji wa maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan na Rais wa Jamhuri ya Shirikisho ya Somali, Hassan Sheikh Mohamud ili kuendelea kuimarisha ushirikiano.

spot_img

Latest articles

Mwanasheria Mkuu wa Serikali: Uchaguzi Mkuu wa 2025 ni halali

Na Mwandishi wetu MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza Johari amesema kuwa, Uchaguzi Mkuu wa...

Viongozi wa dini waendelea kihimiza amani uchaguzi mkuu

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam VIONGOZI wa dini nchini wameendelea kuhimiza umuhimu wa kudumisha...

Ujumbe wa viongozi wa dini kuelekea uchaguzi mkuu Oktoba 29, 2025 katika Kongamano la Kamati ya Amani Kitaifa Dar es Salaam

Na Mwandishi Wetu Askofu Mkuu Wapo Mission, Dk. Sylvester Gamanywa “Mungu ambaye tunamwakilisha ndiye anayweka watawala...

Watumishi wa umma waaswa kushiriki Uchaguzi wa Oktoba 29

Dar es Salaam. Ofisi ya Msajili wa Hazina (OMH) imetoa wito kwa watumishi wote...

More like this

Mwanasheria Mkuu wa Serikali: Uchaguzi Mkuu wa 2025 ni halali

Na Mwandishi wetu MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza Johari amesema kuwa, Uchaguzi Mkuu wa...

Viongozi wa dini waendelea kihimiza amani uchaguzi mkuu

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam VIONGOZI wa dini nchini wameendelea kuhimiza umuhimu wa kudumisha...

Ujumbe wa viongozi wa dini kuelekea uchaguzi mkuu Oktoba 29, 2025 katika Kongamano la Kamati ya Amani Kitaifa Dar es Salaam

Na Mwandishi Wetu Askofu Mkuu Wapo Mission, Dk. Sylvester Gamanywa “Mungu ambaye tunamwakilisha ndiye anayweka watawala...