TANZANIA NA SOMALIA KUBADILISHANA WAFUNGWA

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

SERIKALI ya Tanzania na Somalia zimesaini mikataba miwili ya makubaliano ya kushirikiana katika masuala ya ulinzi na usalama na kubadilishana wafungwa.

Mikataba hiyo imesainiwa leo Januari 29, 2025 jijini Dar es Salaam na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa kwa upande wa Tanzania na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Ahmed Moalim Fiqi kwa upande wa Somalia.

Akizungumza baada ya kusaini mikataba hiyo, Bashungwa amesema mkataba wa kubadilishana wafungwa utaziwezesha nchi hizo mbili kuruhusu wafungwa waweze kutumikia adhabu katika nchi zao na kusaidia kupunguza gharama za kifedha za kuwahudumia wafungwa hao.

“Inapotokea kuna Watanzania wenzetu wameingia katika hali ya kuwa wafungwa wakiwa kule Somalia, kupitia mkataba tuliosaini utatuwezesha kuwachukuwa Watanzania kuwaleta kwenye magereza yetu, vile vile kwa wafungwa wa Somalia watarudishwa kuendelea na vifungo vyao nchini kwao,” ameeleza.

Aidha, Bashungwa amesema mkataba wa ushirikiano kuhusu ulinzi na usalama, unalenga kuimarisha uwezo vyombo vya usalama kwa kutoa mafunzo kwa Askari wa pande zote mbili, kutekeleza operesheni za pamoja, kubadilishana utaalam katika masuala ya usalama na ulinzi pamoja na kubadilishana taarifa za kiintelijensia.

Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Said Mussa amesema utiaji saini wa mikataba hiyo ni utekelezaji wa maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan na Rais wa Jamhuri ya Shirikisho ya Somali, Hassan Sheikh Mohamud ili kuendelea kuimarisha ushirikiano.

spot_img

Latest articles

MADIWANI WA MPANDA NA NSIMBO WAIPONGEZA SERIKALI KWA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA KITUO CHA KUFUA UMEME CHA JULIUS NYERERE

Na Mwandishi wetu Rufiji - Pwani MADIWANI wa Halmashauri za Wilaya za Mpanda na Nsimbo mkoani...

WANANCHI MSIHOFU KUTUMIA NISHATI YA UMEME KATIKA VYOMBO VYA USAFIRI -MD TWANGE

📌Asema TANESCO inajenga vituo vya kuchajia vyombo hivyo nchi nzima 📌Aeleza mpango wa kusambaza majiko...

Aibu: Ukaburu waibuka Baraza la Wawakilishi

MSIMU wa siasa za masimango na kubaguana umerejea tena na kushika kasi. Safari hii...

More like this

MADIWANI WA MPANDA NA NSIMBO WAIPONGEZA SERIKALI KWA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA KITUO CHA KUFUA UMEME CHA JULIUS NYERERE

Na Mwandishi wetu Rufiji - Pwani MADIWANI wa Halmashauri za Wilaya za Mpanda na Nsimbo mkoani...

WANANCHI MSIHOFU KUTUMIA NISHATI YA UMEME KATIKA VYOMBO VYA USAFIRI -MD TWANGE

📌Asema TANESCO inajenga vituo vya kuchajia vyombo hivyo nchi nzima 📌Aeleza mpango wa kusambaza majiko...

Aibu: Ukaburu waibuka Baraza la Wawakilishi

MSIMU wa siasa za masimango na kubaguana umerejea tena na kushika kasi. Safari hii...