MAJALIWA- RAIS SAMIA AAGIZA FEDHA ZA MAADHIMISHO YA UHURU ZIELEKEZWE KUTOA HUDUMA ZA KIJAMII

Na Mwandishi Wetu

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema kuwa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan ameelekeza Maadhimisho ya Miaka 63 ya Uhuru wa Tanzania Bara kwa mwaka 2024 yafanyike katika ngazi ya mikoa na Fedha zilizotengwa katika kila taasisi kwa ajili ya maadhimisho hayo zielekezwe katika kutoa huduma za kijamii.

Amesema kuwa kila mkoa uhakikishe wilaya zake zinafanya shughuli za kijamii ikiwemo upandaji miti, usafi wa mazingira katika maeneo ya kijamii kama vile kwenye Masoko, Hospitali, Kambi za wazee na wenye mahitaji maalum, mashindano ya michezo mbalimbali pamoja na makongamano na midahalo ya kujadili maendeleo endelevu ambayo nchi yetu imefikia katika kipindi cha miaka 63 ya Uhuru.

Amesema hayo leo Jumatano Desemba 04,2024 katika kikao kazi cha Mawaziri kilichofanyika katika ukumbi wa Hazina Jijini Dodoma. “Sherehe za Mwaka huu hazitakuwa na Gwaride na Shughuli nyingine za Kitaifa”.

Amesema kuwa Serikali inatoa wito kwa wananchi kushiriki katika shughuli hizo ili kujivunia sifa za kipekee ambazo zimetokana na Uhuru wetu. “Ninatoa rai kwa Wakuu wote wa Mikoa ya Tanzania Bara, kuzingatia na kufuata ipasavyo maelekezo Mahsusi yaliyotolewa na Serikali ili kuhakikisha maadhimisho hayo yanafanyika kwa ufanisi.

Ameongeza kuwa shughuli za Maadhimisho ya Miaka 63 ya Uhuru wa Tanzania Bara ya Mwaka 2024 zilishaanza tangu Desemba 02 na zitafanyika mpaka 09 Desemba, 2024 Siku ya kilele.

“Katika maadhimisho haya, Taasisi zote za Serikali na Vyombo vyote vya Ulinzi na Usalama zinaelekezwa kuhakikisha Majengo yote ya Serikali Tanzania Bara yanapambwa kwa vitambaa vya rangi ya Bendera ya Taifa, picha rasmi ya Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ambaye ni Muasisi wa Uhuru wetu pamoja na picha ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,” amesema.

Kauli Mbiu inayosema, Miaka 63 ya Uhuru wa Tanzania Bara: “UONGOZI MADHUBUTI NA USHIRIKISHWAJI WA WANANCHI NI MSINGI WA MAENDELEO YETU.”

spot_img

Latest articles

IST Festival yatumika kunadi mitaji nafuu kwa vijana

Na Mwandishi Wetu TAMASHA la IST Festival lililofanyika jana Februari 14, 2026 kwenye viwanja...

Taliss – IST Swimming Championships yawavuta wenye mahitaji maalumu

Na Winfrida Mtoi MASHINDANO ya mchezo wa kuogelea 'Taliss -IST Championship' yameanza leo Februari 14,...

CRDB na Costech watenga Sh. Bilioni 4.6 kuwezesha mitaji kwa vijana wabunifu

Na Mwandishi Wetu WIZARA ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kupitia TUME ya Sayansi na...

Wanahabari watakiwa kuweka usawa katika uandishi wa mabadiliko ya tabianchi

Na Tatu Mohamed MWAKILISHI wa kimataifa kutoka ActionAid International, Teresa Anderson, amesema ipo haja...

More like this

IST Festival yatumika kunadi mitaji nafuu kwa vijana

Na Mwandishi Wetu TAMASHA la IST Festival lililofanyika jana Februari 14, 2026 kwenye viwanja...

Taliss – IST Swimming Championships yawavuta wenye mahitaji maalumu

Na Winfrida Mtoi MASHINDANO ya mchezo wa kuogelea 'Taliss -IST Championship' yameanza leo Februari 14,...

CRDB na Costech watenga Sh. Bilioni 4.6 kuwezesha mitaji kwa vijana wabunifu

Na Mwandishi Wetu WIZARA ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kupitia TUME ya Sayansi na...