Ramovic awaita mashabiki uwanjani, anapenda kuitwa Tanzanian Machine

Na Winfrida Mtoi

Kocha Mkuu wa Yanga,Sead Ramovic amesema mashabiki wanamuita ‘German Machine’ lakini yeye angependa kuitwa ‘Tanzanian Machine’, huku akiwaita mashabiki wa timu hiyo kesho kujitokeza uwanjani ili kukaribisha na kumsapoti ili kupata matokeo mazuri.

Yanga kesho Novemba 26,2024 inashuka dimbani kucheza na Al Hilal katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika  kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.  

“Mashabiki wananiita German Machine, lakini mimi ukiniuliza ningependa kuitwa Tanzanian Machine, nataka kufurahi pamoja na watu wa hapa na kuhakikisha klabu hii inapata mafanikio,” amesema Ramovic.

Aidha amesema Yanga ni timu bora lakini pia wanakwenda kucheza na timu bora, hivyo wanahitaji umakini kukabiliana na mchezo huo mgumu.

“Hii ni mara yangu ya kwanza kwenye Ligi ya Mabingwa. Ni jambo la kheri sana kwangu kushiriki mashindano haya makubwa nikiwa na timu kubwa. Falsafa yangu kubwa ni nidhamu na kujituma. Napenda kuona wachezaji wakicheza kama timu, haijalishi unatumia mfumo gani kama wachezaji wako hawana umoja ni ngumu kupata matokeo,” ameeleza.

Kocha huyo amesema katika timu yao hakuna mtu ambaye ni staa kwa sababu kila mtu ni staa ndani ya kikosi hicho.

Kwa upande wake nahodha wa timu hiyo Bakari Mwamnyeto amesema anajua kwamba mechi ya kesho itakuwa ngumu lakini wapinzani wao wajipange kwani wasipoangalia wanaweza kula hata goli tano.

spot_img

Latest articles

Kamati ya kudumu ya Bunge ya Afya na Ukimwi yaipongeza TMDA

Na Mwandishi Wetu MWENYEKITI wa Kamati ya Kudumubya Bunge ya Afya na Masuala ya...

Serikali yatenga Bilioni 13 kuwezesha ujenzi wa ofisi za TMA

Na Mwandishi Wetu NAIBU Waziri wa Wizara ya Uchukuzi, David Kihenzile, ametembelea ujenzi wa...

Nishati ya umeme inachochea kasi ya Maendeleo mkoani Singida- Meya Singida

📌Afungua kikao kazi kati ya TANESCO na viongozi wa Serikali za Mitaa, Kata na...

Suluhisho la kusambaza taarifa za Hali ya Hewa kwa wakati kwa wakulima lajadiliwa

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), kwa kushirikiana na Norges...

More like this

Kamati ya kudumu ya Bunge ya Afya na Ukimwi yaipongeza TMDA

Na Mwandishi Wetu MWENYEKITI wa Kamati ya Kudumubya Bunge ya Afya na Masuala ya...

Serikali yatenga Bilioni 13 kuwezesha ujenzi wa ofisi za TMA

Na Mwandishi Wetu NAIBU Waziri wa Wizara ya Uchukuzi, David Kihenzile, ametembelea ujenzi wa...

Nishati ya umeme inachochea kasi ya Maendeleo mkoani Singida- Meya Singida

📌Afungua kikao kazi kati ya TANESCO na viongozi wa Serikali za Mitaa, Kata na...