Ramovic awaita mashabiki uwanjani, anapenda kuitwa Tanzanian Machine

Na Winfrida Mtoi

Kocha Mkuu wa Yanga,Sead Ramovic amesema mashabiki wanamuita ‘German Machine’ lakini yeye angependa kuitwa ‘Tanzanian Machine’, huku akiwaita mashabiki wa timu hiyo kesho kujitokeza uwanjani ili kukaribisha na kumsapoti ili kupata matokeo mazuri.

Yanga kesho Novemba 26,2024 inashuka dimbani kucheza na Al Hilal katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika  kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.  

“Mashabiki wananiita German Machine, lakini mimi ukiniuliza ningependa kuitwa Tanzanian Machine, nataka kufurahi pamoja na watu wa hapa na kuhakikisha klabu hii inapata mafanikio,” amesema Ramovic.

Aidha amesema Yanga ni timu bora lakini pia wanakwenda kucheza na timu bora, hivyo wanahitaji umakini kukabiliana na mchezo huo mgumu.

“Hii ni mara yangu ya kwanza kwenye Ligi ya Mabingwa. Ni jambo la kheri sana kwangu kushiriki mashindano haya makubwa nikiwa na timu kubwa. Falsafa yangu kubwa ni nidhamu na kujituma. Napenda kuona wachezaji wakicheza kama timu, haijalishi unatumia mfumo gani kama wachezaji wako hawana umoja ni ngumu kupata matokeo,” ameeleza.

Kocha huyo amesema katika timu yao hakuna mtu ambaye ni staa kwa sababu kila mtu ni staa ndani ya kikosi hicho.

Kwa upande wake nahodha wa timu hiyo Bakari Mwamnyeto amesema anajua kwamba mechi ya kesho itakuwa ngumu lakini wapinzani wao wajipange kwani wasipoangalia wanaweza kula hata goli tano.

spot_img

Latest articles

Katibu Mkuu Maji aitaka DAWASA kufunga mkanda mapambano upotevu wa maji

Na Mwandishi wetu BARAZA kuu la Wafanyakazi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi...

Rais Samia aahidi kuunda chombo cha upelelezi kubaini wahusika wa matukio ya uhalifu Oktoba 29

Na Mwandishi Wetu RAIS Samia Suluhu Hassan, amesema kitaundwa chombo maalumu cha upelelezi kitakachoshughulikia masuala...

Jaji Chande: Katiba mpya, ugumu wa maisha vilichochea ghasia za uchaguzi 2025

Na Mwandishi Wetu Mwenyekiti wa Tume ya Uchunguzi wa Matukio ya vurugu yaliyotokea wakati na...

Tume yataja idadi waliopoteza maisha matukio ya Oktoba 29, Dar yaongoza

Na Mwandishi Wetu TUME ya Uchunguzi wa Matukio ya Uvunjifu wa Amani wakati na...

More like this

Katibu Mkuu Maji aitaka DAWASA kufunga mkanda mapambano upotevu wa maji

Na Mwandishi wetu BARAZA kuu la Wafanyakazi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi...

Rais Samia aahidi kuunda chombo cha upelelezi kubaini wahusika wa matukio ya uhalifu Oktoba 29

Na Mwandishi Wetu RAIS Samia Suluhu Hassan, amesema kitaundwa chombo maalumu cha upelelezi kitakachoshughulikia masuala...

Jaji Chande: Katiba mpya, ugumu wa maisha vilichochea ghasia za uchaguzi 2025

Na Mwandishi Wetu Mwenyekiti wa Tume ya Uchunguzi wa Matukio ya vurugu yaliyotokea wakati na...