Ramovic awaita mashabiki uwanjani, anapenda kuitwa Tanzanian Machine

Na Winfrida Mtoi

Kocha Mkuu wa Yanga,Sead Ramovic amesema mashabiki wanamuita ‘German Machine’ lakini yeye angependa kuitwa ‘Tanzanian Machine’, huku akiwaita mashabiki wa timu hiyo kesho kujitokeza uwanjani ili kukaribisha na kumsapoti ili kupata matokeo mazuri.

Yanga kesho Novemba 26,2024 inashuka dimbani kucheza na Al Hilal katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika  kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.  

“Mashabiki wananiita German Machine, lakini mimi ukiniuliza ningependa kuitwa Tanzanian Machine, nataka kufurahi pamoja na watu wa hapa na kuhakikisha klabu hii inapata mafanikio,” amesema Ramovic.

Aidha amesema Yanga ni timu bora lakini pia wanakwenda kucheza na timu bora, hivyo wanahitaji umakini kukabiliana na mchezo huo mgumu.

“Hii ni mara yangu ya kwanza kwenye Ligi ya Mabingwa. Ni jambo la kheri sana kwangu kushiriki mashindano haya makubwa nikiwa na timu kubwa. Falsafa yangu kubwa ni nidhamu na kujituma. Napenda kuona wachezaji wakicheza kama timu, haijalishi unatumia mfumo gani kama wachezaji wako hawana umoja ni ngumu kupata matokeo,” ameeleza.

Kocha huyo amesema katika timu yao hakuna mtu ambaye ni staa kwa sababu kila mtu ni staa ndani ya kikosi hicho.

Kwa upande wake nahodha wa timu hiyo Bakari Mwamnyeto amesema anajua kwamba mechi ya kesho itakuwa ngumu lakini wapinzani wao wajipange kwani wasipoangalia wanaweza kula hata goli tano.

spot_img

Latest articles

Naibu Waziri Nishati aitaka Tanesco kuimarisha huduma kwa wateja kupitia mifumo ya kidigitali

📌 Afungua Mkutano Mkuu wa Mwaka 2026 wa Maafisa Uhusiano na Huduma kwa Wateja...

Ofisi ya Msajili wa Hazina yafanya mazungumzo na Balozi wa China

Na Mwandishi wa OMH, Dar es Salaam OFISI ya Msajili wa Hazina imekutana na kufanya...

Rais Samia aunda Tume ya Uchunguzi wa Kijinai ghasia za Oktoba 29

Na Mwandishi Wetu RAIS Samia Suluhu Hassan, ameunda Tume ya Uchunguzi wa Kijinai wa matukio...

Tanesco yatakiwa kubuni teknolojia mpya kuboresha huduma kwa wateja

Na Mwandishi Wetu NAIBU Waziri wa Nishati, Salome Makamba, ameielekeza TANESCO kuendelea kufanya tafiti...

More like this

Naibu Waziri Nishati aitaka Tanesco kuimarisha huduma kwa wateja kupitia mifumo ya kidigitali

📌 Afungua Mkutano Mkuu wa Mwaka 2026 wa Maafisa Uhusiano na Huduma kwa Wateja...

Ofisi ya Msajili wa Hazina yafanya mazungumzo na Balozi wa China

Na Mwandishi wa OMH, Dar es Salaam OFISI ya Msajili wa Hazina imekutana na kufanya...

Rais Samia aunda Tume ya Uchunguzi wa Kijinai ghasia za Oktoba 29

Na Mwandishi Wetu RAIS Samia Suluhu Hassan, ameunda Tume ya Uchunguzi wa Kijinai wa matukio...