Ramovic awaita mashabiki uwanjani, anapenda kuitwa Tanzanian Machine

Na Winfrida Mtoi

Kocha Mkuu wa Yanga,Sead Ramovic amesema mashabiki wanamuita ‘German Machine’ lakini yeye angependa kuitwa ‘Tanzanian Machine’, huku akiwaita mashabiki wa timu hiyo kesho kujitokeza uwanjani ili kukaribisha na kumsapoti ili kupata matokeo mazuri.

Yanga kesho Novemba 26,2024 inashuka dimbani kucheza na Al Hilal katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika  kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.  

“Mashabiki wananiita German Machine, lakini mimi ukiniuliza ningependa kuitwa Tanzanian Machine, nataka kufurahi pamoja na watu wa hapa na kuhakikisha klabu hii inapata mafanikio,” amesema Ramovic.

Aidha amesema Yanga ni timu bora lakini pia wanakwenda kucheza na timu bora, hivyo wanahitaji umakini kukabiliana na mchezo huo mgumu.

“Hii ni mara yangu ya kwanza kwenye Ligi ya Mabingwa. Ni jambo la kheri sana kwangu kushiriki mashindano haya makubwa nikiwa na timu kubwa. Falsafa yangu kubwa ni nidhamu na kujituma. Napenda kuona wachezaji wakicheza kama timu, haijalishi unatumia mfumo gani kama wachezaji wako hawana umoja ni ngumu kupata matokeo,” ameeleza.

Kocha huyo amesema katika timu yao hakuna mtu ambaye ni staa kwa sababu kila mtu ni staa ndani ya kikosi hicho.

Kwa upande wake nahodha wa timu hiyo Bakari Mwamnyeto amesema anajua kwamba mechi ya kesho itakuwa ngumu lakini wapinzani wao wajipange kwani wasipoangalia wanaweza kula hata goli tano.

spot_img

Latest articles

Waziri Mkuu atoa sababu yakutotaja idadi vifo vilivyotokea Oktoba 29

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amesema ni muhimu watanzania kutanguliza utu na...

Niffer arudishwa gerezani, 20 kesi ya uhaini waachiwa huru

Na Mwandishi Wetu Watuhumiwa 20 kati ya 22 waliokuwa wanashtakiwa kwa makosa ya uhaini wameachiwa...

Dk.Mwigulu aagiza Kanisa Gwajima lifunguliwe

Na Mwandishi Wetu Waziri Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba ameagiza kufunguliwa kwa Kanisa la Ufufuo na...

Ndejembi asisitiza ushirikiano kwa viongozi katika utekelezaji wa miradi yenye kipaumbele kwa wananchi

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi (Mb), ametoa wito kwa viongozi na...

More like this

Waziri Mkuu atoa sababu yakutotaja idadi vifo vilivyotokea Oktoba 29

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amesema ni muhimu watanzania kutanguliza utu na...

Niffer arudishwa gerezani, 20 kesi ya uhaini waachiwa huru

Na Mwandishi Wetu Watuhumiwa 20 kati ya 22 waliokuwa wanashtakiwa kwa makosa ya uhaini wameachiwa...

Dk.Mwigulu aagiza Kanisa Gwajima lifunguliwe

Na Mwandishi Wetu Waziri Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba ameagiza kufunguliwa kwa Kanisa la Ufufuo na...