Ramovic awaita mashabiki uwanjani, anapenda kuitwa Tanzanian Machine

Na Winfrida Mtoi

Kocha Mkuu wa Yanga,Sead Ramovic amesema mashabiki wanamuita ‘German Machine’ lakini yeye angependa kuitwa ‘Tanzanian Machine’, huku akiwaita mashabiki wa timu hiyo kesho kujitokeza uwanjani ili kukaribisha na kumsapoti ili kupata matokeo mazuri.

Yanga kesho Novemba 26,2024 inashuka dimbani kucheza na Al Hilal katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika  kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.  

“Mashabiki wananiita German Machine, lakini mimi ukiniuliza ningependa kuitwa Tanzanian Machine, nataka kufurahi pamoja na watu wa hapa na kuhakikisha klabu hii inapata mafanikio,” amesema Ramovic.

Aidha amesema Yanga ni timu bora lakini pia wanakwenda kucheza na timu bora, hivyo wanahitaji umakini kukabiliana na mchezo huo mgumu.

“Hii ni mara yangu ya kwanza kwenye Ligi ya Mabingwa. Ni jambo la kheri sana kwangu kushiriki mashindano haya makubwa nikiwa na timu kubwa. Falsafa yangu kubwa ni nidhamu na kujituma. Napenda kuona wachezaji wakicheza kama timu, haijalishi unatumia mfumo gani kama wachezaji wako hawana umoja ni ngumu kupata matokeo,” ameeleza.

Kocha huyo amesema katika timu yao hakuna mtu ambaye ni staa kwa sababu kila mtu ni staa ndani ya kikosi hicho.

Kwa upande wake nahodha wa timu hiyo Bakari Mwamnyeto amesema anajua kwamba mechi ya kesho itakuwa ngumu lakini wapinzani wao wajipange kwani wasipoangalia wanaweza kula hata goli tano.

spot_img

Latest articles

Mwanasheria Mkuu wa Serikali: Uchaguzi Mkuu wa 2025 ni halali

Na Mwandishi wetu MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza Johari amesema kuwa, Uchaguzi Mkuu wa...

Viongozi wa dini waendelea kihimiza amani uchaguzi mkuu

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam VIONGOZI wa dini nchini wameendelea kuhimiza umuhimu wa kudumisha...

Ujumbe wa viongozi wa dini kuelekea uchaguzi mkuu Oktoba 29, 2025 katika Kongamano la Kamati ya Amani Kitaifa Dar es Salaam

Na Mwandishi Wetu Askofu Mkuu Wapo Mission, Dk. Sylvester Gamanywa “Mungu ambaye tunamwakilisha ndiye anayweka watawala...

Watumishi wa umma waaswa kushiriki Uchaguzi wa Oktoba 29

Dar es Salaam. Ofisi ya Msajili wa Hazina (OMH) imetoa wito kwa watumishi wote...

More like this

Mwanasheria Mkuu wa Serikali: Uchaguzi Mkuu wa 2025 ni halali

Na Mwandishi wetu MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza Johari amesema kuwa, Uchaguzi Mkuu wa...

Viongozi wa dini waendelea kihimiza amani uchaguzi mkuu

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam VIONGOZI wa dini nchini wameendelea kuhimiza umuhimu wa kudumisha...

Ujumbe wa viongozi wa dini kuelekea uchaguzi mkuu Oktoba 29, 2025 katika Kongamano la Kamati ya Amani Kitaifa Dar es Salaam

Na Mwandishi Wetu Askofu Mkuu Wapo Mission, Dk. Sylvester Gamanywa “Mungu ambaye tunamwakilisha ndiye anayweka watawala...