Dk. Biteko asisitiza kupiga kura ni haki ya Kikatiba

Na Mwandishi Wetu

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko amewahimiza Watanzania kushiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika Novemba 27, 2024.

Dk. Biteko ametoa rai hiyo leo Novemba 25,2024 akiwa mkoani Geita ambapo amesema uchaguzi huo ni muhimu hususan kwa ukuzaji wa demokrasia nchini.

“Naomba Watanzania wote waliojiandikisha kwenye Daftari la Kupiga Kura katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa katika maeneo yao wajitokeze kupiga kura kwa ajili ya kuchagua viongozi wao,” amesema Dk. Biteko.

“Viongozi hawa ndio msingi katika nchi yetu, viongozi hawa ndio wanajua watu wanaishije, wana shida gani na watafanya nini kutatua shida hizo. Ni muhimu wote kushiriki kuchagua viongozi tunaowataka,” amesisitiza.

Aidha, Dk. Biteko amebainisha kuwa kupiga kura ni haki ya kila Mtanzania mwenye sifa hivyo watu wote wenye sifa wajitokeze kupiga kura ifikapo Novemba 27, 2024.

spot_img

Latest articles

Mfumo wa T-CAMS ni Mageuzi ya Kidijitali Yanayojenga Uwazi, Ufanisi na Ushindani katika Sekta ya Uwakala wa Forodha Tanzania

Na Mwandishi Wetu KATIKA dunia ya sasa, ushindani wa biashara haupimwi tena kwa ukubwa...

TBA yafungua fursa za uwekezaji katika miundombinu ya kilimo na biashara

Na Mwandishi Wetu, Dodoma WAKALA wa Majengo Tanzania (TBA) umewataka wawekezaji wa sekta binafsi kutumia...

UDOM yabuni mfumo wa kidijitali wa kupunguza upotevu wa mazao baada ya kuvuna

Na Mwandishi Wetu CHUO Kikuu cha Dodoma (UDOM) kimebuni mfumo wa kidijitali unaowezesha wakulima kufuatilia...

ZSTC yapongeza mchango wa TADB katika kukuza sekta ya karafuu Zanzibar

Na Mwandishi Wetu SHIRIKA la Biashara la Taifa Zanzibar (ZSTC) limesema ushirikiano wake na...

More like this

Mfumo wa T-CAMS ni Mageuzi ya Kidijitali Yanayojenga Uwazi, Ufanisi na Ushindani katika Sekta ya Uwakala wa Forodha Tanzania

Na Mwandishi Wetu KATIKA dunia ya sasa, ushindani wa biashara haupimwi tena kwa ukubwa...

TBA yafungua fursa za uwekezaji katika miundombinu ya kilimo na biashara

Na Mwandishi Wetu, Dodoma WAKALA wa Majengo Tanzania (TBA) umewataka wawekezaji wa sekta binafsi kutumia...

UDOM yabuni mfumo wa kidijitali wa kupunguza upotevu wa mazao baada ya kuvuna

Na Mwandishi Wetu CHUO Kikuu cha Dodoma (UDOM) kimebuni mfumo wa kidijitali unaowezesha wakulima kufuatilia...