Dk. Biteko asisitiza kupiga kura ni haki ya Kikatiba

Na Mwandishi Wetu

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko amewahimiza Watanzania kushiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika Novemba 27, 2024.

Dk. Biteko ametoa rai hiyo leo Novemba 25,2024 akiwa mkoani Geita ambapo amesema uchaguzi huo ni muhimu hususan kwa ukuzaji wa demokrasia nchini.

“Naomba Watanzania wote waliojiandikisha kwenye Daftari la Kupiga Kura katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa katika maeneo yao wajitokeze kupiga kura kwa ajili ya kuchagua viongozi wao,” amesema Dk. Biteko.

“Viongozi hawa ndio msingi katika nchi yetu, viongozi hawa ndio wanajua watu wanaishije, wana shida gani na watafanya nini kutatua shida hizo. Ni muhimu wote kushiriki kuchagua viongozi tunaowataka,” amesisitiza.

Aidha, Dk. Biteko amebainisha kuwa kupiga kura ni haki ya kila Mtanzania mwenye sifa hivyo watu wote wenye sifa wajitokeze kupiga kura ifikapo Novemba 27, 2024.

spot_img

Latest articles

WANANCHI WAENDELEA KUNUFAIKA NA HUDUMA ZA TPRB NANENANE DODOMA

Na Mwandishi Wetu Na Mwandishi Wetu WANANCHI na wadau mbalimbali wanaendelea kunufaika na huduma zinazotolewa...

CDICD YAONGEZA THAMANI YA BLACK GRANITE

🔸Uchakataji wa kisasa waongeza ushindani wa bidhaa za Tanzania katika soko la ndani na...

Taasisi za Umma 54 kuwasilisha taarifa za utendaji wa uwekezaji kwa Kamati za Bunge

Na Mwandishi Wetu JUMLA ya taasisi za umma 54 zinatarajiwa kuwasilisha taarifa za utendaji...

MKURUGENZI BOT AVUTIWA NA UFANISI WA UTUNZAJI KUMBUKUMBU KIDIJITALI WA PSSSF

Na Mwandishi Wetu MKURUGENZI wa Tafiti na Uchumi Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Dkt....

More like this

WANANCHI WAENDELEA KUNUFAIKA NA HUDUMA ZA TPRB NANENANE DODOMA

Na Mwandishi Wetu Na Mwandishi Wetu WANANCHI na wadau mbalimbali wanaendelea kunufaika na huduma zinazotolewa...

CDICD YAONGEZA THAMANI YA BLACK GRANITE

🔸Uchakataji wa kisasa waongeza ushindani wa bidhaa za Tanzania katika soko la ndani na...

Taasisi za Umma 54 kuwasilisha taarifa za utendaji wa uwekezaji kwa Kamati za Bunge

Na Mwandishi Wetu JUMLA ya taasisi za umma 54 zinatarajiwa kuwasilisha taarifa za utendaji...