Dk. Biteko asisitiza kupiga kura ni haki ya Kikatiba

Na Mwandishi Wetu

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko amewahimiza Watanzania kushiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika Novemba 27, 2024.

Dk. Biteko ametoa rai hiyo leo Novemba 25,2024 akiwa mkoani Geita ambapo amesema uchaguzi huo ni muhimu hususan kwa ukuzaji wa demokrasia nchini.

“Naomba Watanzania wote waliojiandikisha kwenye Daftari la Kupiga Kura katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa katika maeneo yao wajitokeze kupiga kura kwa ajili ya kuchagua viongozi wao,” amesema Dk. Biteko.

“Viongozi hawa ndio msingi katika nchi yetu, viongozi hawa ndio wanajua watu wanaishije, wana shida gani na watafanya nini kutatua shida hizo. Ni muhimu wote kushiriki kuchagua viongozi tunaowataka,” amesisitiza.

Aidha, Dk. Biteko amebainisha kuwa kupiga kura ni haki ya kila Mtanzania mwenye sifa hivyo watu wote wenye sifa wajitokeze kupiga kura ifikapo Novemba 27, 2024.

spot_img

Latest articles

Tume juu ya Tume, tunavuka au tunatumbukia zaidi?

MSINGI ni neno linalobeba maana kubwa katika mambo mengi. Katika ujenzi iwe wa barabara...

Tanzania kujifunza kutoka China kuhusu mageuzi ya mashirika ya umma

Na Mwandishi wa OMH, Dar es Salaam TANZANIA imeonesha nia ya kutumia uzoefu wa China...

Naibu Waziri Nishati aitaka Tanesco kuimarisha huduma kwa wateja kupitia mifumo ya kidigitali

📌 Afungua Mkutano Mkuu wa Mwaka 2026 wa Maafisa Uhusiano na Huduma kwa Wateja...

Ofisi ya Msajili wa Hazina yafanya mazungumzo na Balozi wa China

Na Mwandishi wa OMH, Dar es Salaam OFISI ya Msajili wa Hazina imekutana na kufanya...

More like this

Tume juu ya Tume, tunavuka au tunatumbukia zaidi?

MSINGI ni neno linalobeba maana kubwa katika mambo mengi. Katika ujenzi iwe wa barabara...

Tanzania kujifunza kutoka China kuhusu mageuzi ya mashirika ya umma

Na Mwandishi wa OMH, Dar es Salaam TANZANIA imeonesha nia ya kutumia uzoefu wa China...

Naibu Waziri Nishati aitaka Tanesco kuimarisha huduma kwa wateja kupitia mifumo ya kidigitali

📌 Afungua Mkutano Mkuu wa Mwaka 2026 wa Maafisa Uhusiano na Huduma kwa Wateja...