Dk. Biteko asisitiza kupiga kura ni haki ya Kikatiba

Na Mwandishi Wetu

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko amewahimiza Watanzania kushiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika Novemba 27, 2024.

Dk. Biteko ametoa rai hiyo leo Novemba 25,2024 akiwa mkoani Geita ambapo amesema uchaguzi huo ni muhimu hususan kwa ukuzaji wa demokrasia nchini.

“Naomba Watanzania wote waliojiandikisha kwenye Daftari la Kupiga Kura katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa katika maeneo yao wajitokeze kupiga kura kwa ajili ya kuchagua viongozi wao,” amesema Dk. Biteko.

“Viongozi hawa ndio msingi katika nchi yetu, viongozi hawa ndio wanajua watu wanaishije, wana shida gani na watafanya nini kutatua shida hizo. Ni muhimu wote kushiriki kuchagua viongozi tunaowataka,” amesisitiza.

Aidha, Dk. Biteko amebainisha kuwa kupiga kura ni haki ya kila Mtanzania mwenye sifa hivyo watu wote wenye sifa wajitokeze kupiga kura ifikapo Novemba 27, 2024.

spot_img

Latest articles

ELIMU YA VIPIMO YAWAVUTIA WANANCHI, WAAHIDI KUWA MABALOZI WA KUJITOLEA

Na Mwandishi Wetu Dodoma – “Sasa najua ni nini ninapaswa kuangalia ninapojaza mafuta, kununua...

Bodi ya DAWASA yasisitiza kukamilika kwa wakati ufungaji pampu mpya za maji

Na Mwandishi Wetu BODI ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira...

JAB YASOGEZA HUDUMA ZA ITHIBATI KARIBU NA WAANDISHI DODOMA

Na Mwandishi Wetu BODI ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeanza kutoa huduma...

Wadau wavutiwa elimu ya vipimo maadhimisho wiki ya utumishi wa umma

Na Mwandishi Wetu WADAU mbalimbali waliotembelea Banda la Wakala wa Vipimo (WMA) katika siku ya...

More like this

ELIMU YA VIPIMO YAWAVUTIA WANANCHI, WAAHIDI KUWA MABALOZI WA KUJITOLEA

Na Mwandishi Wetu Dodoma – “Sasa najua ni nini ninapaswa kuangalia ninapojaza mafuta, kununua...

Bodi ya DAWASA yasisitiza kukamilika kwa wakati ufungaji pampu mpya za maji

Na Mwandishi Wetu BODI ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira...

JAB YASOGEZA HUDUMA ZA ITHIBATI KARIBU NA WAANDISHI DODOMA

Na Mwandishi Wetu BODI ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeanza kutoa huduma...