Dk. Biteko asisitiza kupiga kura ni haki ya Kikatiba

Na Mwandishi Wetu

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko amewahimiza Watanzania kushiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika Novemba 27, 2024.

Dk. Biteko ametoa rai hiyo leo Novemba 25,2024 akiwa mkoani Geita ambapo amesema uchaguzi huo ni muhimu hususan kwa ukuzaji wa demokrasia nchini.

“Naomba Watanzania wote waliojiandikisha kwenye Daftari la Kupiga Kura katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa katika maeneo yao wajitokeze kupiga kura kwa ajili ya kuchagua viongozi wao,” amesema Dk. Biteko.

“Viongozi hawa ndio msingi katika nchi yetu, viongozi hawa ndio wanajua watu wanaishije, wana shida gani na watafanya nini kutatua shida hizo. Ni muhimu wote kushiriki kuchagua viongozi tunaowataka,” amesisitiza.

Aidha, Dk. Biteko amebainisha kuwa kupiga kura ni haki ya kila Mtanzania mwenye sifa hivyo watu wote wenye sifa wajitokeze kupiga kura ifikapo Novemba 27, 2024.

spot_img

Latest articles

Tume kuundwa kuchunguza vurugu zilizotokea Oktoba 29, mwaka huu

Na Mwandishi Wetu  RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametangaza...

Mkakati wa Mawasiliano wa Nishati Safi ya kupikia: Dira ya Mafanikio ya Taifa

Na Mwandishi Wetu IMEELEZWA kuwa Mkakati wa Mawasiliano wa Nishati Safi ya Kupikia ni...

JKT Queens na matumaini nusu  fainali CAFWCL mbele ya TP Mazembe

Na Mwandishi Wetu Baada ya timu ya JKT Queens kutoa sare mbili mfululizo Ligi ya...

Rais Mwinyi ateua Mawaziri 20

Na Mwandishi Wetu Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali...

More like this

Tume kuundwa kuchunguza vurugu zilizotokea Oktoba 29, mwaka huu

Na Mwandishi Wetu  RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametangaza...

Mkakati wa Mawasiliano wa Nishati Safi ya kupikia: Dira ya Mafanikio ya Taifa

Na Mwandishi Wetu IMEELEZWA kuwa Mkakati wa Mawasiliano wa Nishati Safi ya Kupikia ni...

JKT Queens na matumaini nusu  fainali CAFWCL mbele ya TP Mazembe

Na Mwandishi Wetu Baada ya timu ya JKT Queens kutoa sare mbili mfululizo Ligi ya...