Dk. Biteko asisitiza kupiga kura ni haki ya Kikatiba

Na Mwandishi Wetu

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko amewahimiza Watanzania kushiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika Novemba 27, 2024.

Dk. Biteko ametoa rai hiyo leo Novemba 25,2024 akiwa mkoani Geita ambapo amesema uchaguzi huo ni muhimu hususan kwa ukuzaji wa demokrasia nchini.

“Naomba Watanzania wote waliojiandikisha kwenye Daftari la Kupiga Kura katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa katika maeneo yao wajitokeze kupiga kura kwa ajili ya kuchagua viongozi wao,” amesema Dk. Biteko.

“Viongozi hawa ndio msingi katika nchi yetu, viongozi hawa ndio wanajua watu wanaishije, wana shida gani na watafanya nini kutatua shida hizo. Ni muhimu wote kushiriki kuchagua viongozi tunaowataka,” amesisitiza.

Aidha, Dk. Biteko amebainisha kuwa kupiga kura ni haki ya kila Mtanzania mwenye sifa hivyo watu wote wenye sifa wajitokeze kupiga kura ifikapo Novemba 27, 2024.

spot_img

Latest articles

Simba yaachia pointi tatu kwa Mkapa, Azam nayo mambo magumu

Na Winfrida Mtoi Simba imeshindwa kutamba nyumbani baada ya kufungwa na Petro de Luanda bao...

Serikali yaahidi kushirikiana na wadau kuendeleza mchezo wa kuogelea

Na Winfrida Mtoi WADAU wa mchezo wakuogelea Afrika Mashariki wamekutana kujadili maendeleo ya mchezo huo,...

Ndejembi: Tanesco mmefanya mageuzi makubwa katika huduma ya umeme kwa wananchi

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi, amesema kuwa Shirika la Umeme Tanzania...

Dube awapa raha wananchi

Na Winfrida Mtoi BAO pekee lililofungwa na Prince Dube dakika ya 58, limeipa Yanga alama...

More like this

Simba yaachia pointi tatu kwa Mkapa, Azam nayo mambo magumu

Na Winfrida Mtoi Simba imeshindwa kutamba nyumbani baada ya kufungwa na Petro de Luanda bao...

Serikali yaahidi kushirikiana na wadau kuendeleza mchezo wa kuogelea

Na Winfrida Mtoi WADAU wa mchezo wakuogelea Afrika Mashariki wamekutana kujadili maendeleo ya mchezo huo,...

Ndejembi: Tanesco mmefanya mageuzi makubwa katika huduma ya umeme kwa wananchi

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi, amesema kuwa Shirika la Umeme Tanzania...