King Kikii afariki, Rais Samia amlilia

Na Mwandishi Wetu

Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ametuma salamu za pole kutokana na kifo cha mkongwe wa muziki wa dansi,  Boniface Kikumbi ‘King Kikii’ na kusema nguli huyo atakumbukwa na kuenziwa   kwa kazi zake nyingi nzuri ikiwamo wimbo wa kitambaa cheupe.

Amesema King Kikii ametoa burudani kwa mamilioni ya Watanzania na amekuwa mlezi na mwalimu wa wengi katika tasnia ya muziki.

“Ninatoa salamu za pole kwa familia, ndugu, jamaa, marafiki, wasanii na wapenzi wote wa muziki nchini kufuatia kifo cha mwanamuziki nguli Boniface Kikumbi Mwanza Mpango ‘King Kikii’.

Kwa zaidi ya miaka 50 King Kikii. Tutamkumbuka na kumuenzi kwa kazi zake nyingi na nzuri ikiwemo wimbo wake maarufu wa ‘Kitambaa Cheupe’ ambao umeendelea kuwa sehemu ya burudani kwenye maeneo na shughuli mbalimbali za burudani nchini.

“Mwenyezi Mungu ailaze roho yake mahali pema”

King Kikii amefariki usiku wa kuamkia leo Novemba 15, 2024 nyumbani kwake Mtoni kwa Aziz Ally, jijini Dar es Salaam.

spot_img

Latest articles

RC Chalamila tafuta dozi ya Tume Keenja

KATIKA juhudi za kurejesha utawala wa sheria (orderly administration) katika jiji la Dar es...

DAWASA YAANZA MSAKO KWA WANAOJIUNGANISHIA MAJI KINYEMELA

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es salaam (DAWASA)...

Vipengele 63 Kuing’arisha The Serengeti Awards 2026

Na Mwandishi Wetu JUMLA ya vipengele 63 vitaingia katika kinyang’anyiro cha The Serengeti Awards...

PSSSF yawajengea uwezo waandishi wa habari kuhusu masuala ya Hifadhi ya Jamii

Dar es Salaam- Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) umeendesha...

More like this

RC Chalamila tafuta dozi ya Tume Keenja

KATIKA juhudi za kurejesha utawala wa sheria (orderly administration) katika jiji la Dar es...

DAWASA YAANZA MSAKO KWA WANAOJIUNGANISHIA MAJI KINYEMELA

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es salaam (DAWASA)...

Vipengele 63 Kuing’arisha The Serengeti Awards 2026

Na Mwandishi Wetu JUMLA ya vipengele 63 vitaingia katika kinyang’anyiro cha The Serengeti Awards...