King Kikii afariki, Rais Samia amlilia

Na Mwandishi Wetu

Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ametuma salamu za pole kutokana na kifo cha mkongwe wa muziki wa dansi,  Boniface Kikumbi ‘King Kikii’ na kusema nguli huyo atakumbukwa na kuenziwa   kwa kazi zake nyingi nzuri ikiwamo wimbo wa kitambaa cheupe.

Amesema King Kikii ametoa burudani kwa mamilioni ya Watanzania na amekuwa mlezi na mwalimu wa wengi katika tasnia ya muziki.

“Ninatoa salamu za pole kwa familia, ndugu, jamaa, marafiki, wasanii na wapenzi wote wa muziki nchini kufuatia kifo cha mwanamuziki nguli Boniface Kikumbi Mwanza Mpango ‘King Kikii’.

Kwa zaidi ya miaka 50 King Kikii. Tutamkumbuka na kumuenzi kwa kazi zake nyingi na nzuri ikiwemo wimbo wake maarufu wa ‘Kitambaa Cheupe’ ambao umeendelea kuwa sehemu ya burudani kwenye maeneo na shughuli mbalimbali za burudani nchini.

“Mwenyezi Mungu ailaze roho yake mahali pema”

King Kikii amefariki usiku wa kuamkia leo Novemba 15, 2024 nyumbani kwake Mtoni kwa Aziz Ally, jijini Dar es Salaam.

spot_img

Latest articles

Katibu Mkuu Kiongozi awataka maofisa habari serikalini kujiimarisha kiutendaji kukabiliana na teknolojia

Na Winfrida Mtoi KATIBU Mkuu Kiongozi, Balozi Dk. Moses Kusiluka amewataka Maofisa Habari wa Serikali...

Rais Mwinyi: SMZ kuendelea kushirikiana na TRA kuimarisha ukusanyaji wa mapato

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein...

Tanzania yajumuishwa kwenye orodha ya Nchi zenye vikwazo vya kuingia Marekani

Na Mwandishi Wetu SERIKALI ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imethibitisha kuwa Serikali ya...

More like this

Katibu Mkuu Kiongozi awataka maofisa habari serikalini kujiimarisha kiutendaji kukabiliana na teknolojia

Na Winfrida Mtoi KATIBU Mkuu Kiongozi, Balozi Dk. Moses Kusiluka amewataka Maofisa Habari wa Serikali...

Rais Mwinyi: SMZ kuendelea kushirikiana na TRA kuimarisha ukusanyaji wa mapato

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein...