Wananchi Kipunguni kulipwa fidia mwezi ujao

Na Nora Damian

Waziri wa Fedha, Dk. Mwigulu Nchemba amesema fidia kwa wakazi wa Mtaa wa Kipunguni wanaotakiwa kuhama kupisha upanuzi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, zitaanza kulipwa Agosti mwaka huu.

Akizungumza leo Julai 8,2024 katika mkutano wa hadhara uliofanyika Jimbo la Segerea katika viwanja vya Shule ya Sekondari Liwiti, amesema imechelewa kwa sababu ya dharura iliyojitokeza katika mwaka wa fedha uliopita (2023/2024).

Dk. Nchemba alikuwa akizungumza kwa simu baada ya kupigiwa na Katibu Mwenezi wa CCM Taifa, Amos Makala, kutoa majibu ya suala hilo lililoulizwa na wananchi katika mkutano huo.

“Jambo la Kipunguni ninalifahamu vizuri na nilishafika Kipunguni kulielezea, tulitoa kauli ya serikali. Mheshimiwa mbunge (Bonnah) amelifuatilia mara nyingi, amelifikisha kwenye vikao kadhaa vya viongozi wakuu na vyote kauli ya serikali ilikuwa ni kuanza kulipa fidia mara moja.

“Tumechelewa tofauti na tulivyoahidi kwa sababu ya dharura iliyojitokeza katika mwaka wa fedha uliopita, tullikuwa na dharura kubwa ambazo zilikuwa zinalikata taifa vipande vipande yakiwemo mafuriko ya Kusini.

“Leo asubuhi nilikutana na ujumbe wa viongozi 10 kutoka Kipunguni, niliwapa majibu kwamba baada ya kuanza mwaka mpya wa fedha tunatarajia mwezi mmoja utatumika kuweka sawa mifumo mipya ya malipo…tunatarajia kuanzia mwezi wa nane tuanze kulipa wananchi wa Kipunguni,” amesema Dk. Nchemba.

Makala ambaye alikagua utekelezaji wa Ilani katika miradi mbalimbali ya maendeleo ukiwemo ujenzi wa shule za sekondari amempongeza Bonnah na kusema ni mchapakazi.

“Bonnah anafanya kazi, mambo ya kusema mnyonge mnyongeni haki yake mpeni…ukishamnyonga haki anaipata wapi…kwahiyo tunakupongeza sana kwa kazi nzuri unayoifanya. Ni kamanda mzuri, yuko na wananchi wake na anawatetea muda wote.

“Kila waziri atakayeteuliwa awe wa ujenzi au uchukuzi anajua kuna swali la Kipunguni, lazima amuulize. Ameliweka vizuri suala hili na sasa yamebaki malipo, mimi shahidi wenu mwezi wa nane wananchi watapata fidia zao,” amesema Makala.

Awali Mbunge wa Jimbo la Segerea, Bonnah Kamoli, amesema kwa muda mrefu wananchi wa Kipunguni wamekuwa wakiahidiwa kulipwa fidia bila mafanikio na kuiomba serikali kuharakisha malipo hayo.

spot_img

Latest articles

Wanafunzi watatu wafariki dunia baada ya kupigwa na radi Dar

Na Mwandishi wetu WANAFUNZI watatu wa Shule ya Msingi Msongola iliyopo eneo la Msongola,...

Serikali yawataka Wakurugenzi kuongeza thamani inayopimika katika uwekezaji wa hisa chache

Na Mwandishi wetu SERIKALI imewataka wakurugenzi wa bodi za kampuni ambazo ina umiliki wa...

Tanesco yazindua ndege nyuki (Drones) kuboresha miundombinu ya umeme nchini

📌Ni sehemu ya utekelezaji wa mikakati yake kuimarisha huduma kwa wateja kwa kutumia njia...

Senegal yavuliwa ubingwa wa AFCON 2025, wapewa Morocco

Na Mwandishi Wetu SENEGAL imevuliwa ubingwa  wa Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2025 baada...

More like this

Wanafunzi watatu wafariki dunia baada ya kupigwa na radi Dar

Na Mwandishi wetu WANAFUNZI watatu wa Shule ya Msingi Msongola iliyopo eneo la Msongola,...

Serikali yawataka Wakurugenzi kuongeza thamani inayopimika katika uwekezaji wa hisa chache

Na Mwandishi wetu SERIKALI imewataka wakurugenzi wa bodi za kampuni ambazo ina umiliki wa...

Tanesco yazindua ndege nyuki (Drones) kuboresha miundombinu ya umeme nchini

📌Ni sehemu ya utekelezaji wa mikakati yake kuimarisha huduma kwa wateja kwa kutumia njia...