Mabadiliko ya sheria ya sukari yatawakomboa Watanzania-SBT

Mkurugenzi wa Bodi ya Sukari Tanzania, Profesa Kenneth Bengesi, akizungumza na Wahariri na Waandishi wa Habari.

Na Mwandishi Wetu, Media Brains

Kufuatia upotoshaji unaoendelea kutolewa na baadhi ya watu wasiokuwa na ufahamu juu ya sheria mpya ya sukari, Bodi ya Sukari Tanzania imetoa ufafanuzi kuhusu mabadiliko hayo.

Bodi imeeleza kuwa sheria hiyo mpya, iliyopitishwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, inalenga kudhibiti mfumuko wa bei ya sukari ili isimuumize mwananchi, kuhakikisha upatikanaji wa uhakika, uwazi katika usambazaji wake, pamoja na ufanisi kwenye viwanda vya sukari nchini.

Hayo yamesemwa Julai 5, 2024, na Mkurugenzi wa Bodi ya Sukari Tanzania, Profesa Kenneth Bengesi, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam. Ufafanuzi huo umekuja baada ya baadhi ya wadau wa sekta ya sukari kuelezea sakata hilo bila kuwa na taarifa za kutosha, hali iliyoibua sintofahamu kwenye sekta hiyo nyeti nchini.

“Baadhi ya watu wanaoelezea suala la sukari hawana taarifa za kutosha, hivyo ni jukumu letu kama Bodi kutoa picha kamili ya namna gani Watanzania watafaidika na mabadiliko haya katika sheria ya sukari,” amesema Profesa Bengesi.

Profesa Bengesi ameendelea kufafanua kuwa baadhi ya hoja zilizofafanuliwa na Bodi ya Sukari Tanzania ni pamoja na uhaba wa sukari, malalamiko ya utoaji wa vibali, na mbinu zinazotumika kuhakikisha uhaba wa sukari nchini unaisha.

“Serikali imefanya mabadiliko haya kwa nia ya kuleta ahueni kwa wananchi na kuleta ufanisi katika sekta ya sukari. Tunawahakikishia wananchi kuwa mabadiliko haya yatasaidia kupunguza changamoto zilizopo na kuleta maendeleo endelevu katika sekta hii muhimu,” ameongeza Profesa Bengesi.

Kwa mujibu wa Profesa Bengesi, Bodi ya Sukari Tanzania itaendelea kutoa elimu kwa umma kuhusu sheria mpya ya sukari na mafanikio yanayotarajiwa kutokana na utekelezaji wake. Amewataka wananchi na wadau wa sekta ya sukari kuwa na subira na kuunga mkono juhudi za serikali katika kuboresha sekta hiyo.

spot_img

Latest articles

Ndejembi: Ufanisi wa Tanesco katika utekelezaji na Usimamizi wa miradi umeleta mfumo madhubuti wa Nishati

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, amesema kuwa Shirika la Umeme...

Maboresho ya mitambo ya kufua umeme Mtera yaimarisha uzalishaji umeme

Na Mwandishi Wetu, Mtera NAIBU Waziri wa Nishati, Salome Makamba, Novemba 26, 2025, alitembelea na...

Ndejembi: Tanzania sasa ina umeme wa kutosha

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amesema Tanzania kwa sasa ina umeme...

Jeshi la Polisi lachunguza  taarifa ya OCD  Chunya

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi limesema limeona na linafanyia uchunguzi taarifa inayosambaa kwenye mitandao...

More like this

Ndejembi: Ufanisi wa Tanesco katika utekelezaji na Usimamizi wa miradi umeleta mfumo madhubuti wa Nishati

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, amesema kuwa Shirika la Umeme...

Maboresho ya mitambo ya kufua umeme Mtera yaimarisha uzalishaji umeme

Na Mwandishi Wetu, Mtera NAIBU Waziri wa Nishati, Salome Makamba, Novemba 26, 2025, alitembelea na...

Ndejembi: Tanzania sasa ina umeme wa kutosha

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amesema Tanzania kwa sasa ina umeme...