CAG aipa tano PPAA

Na Mwandishi Wetu, Media Brains

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Charles Kichere ameipongeza Mamlaka ya Rufani ya Zabuni za Umma (PPAA) kwa kazi nzuri wanayoifanya ya kutoa elimu kwa umma kuhusu majukumu yake.

Bw. Kichere ametoa pongezi hizo wakati alipotembelea banda la PPAA katika Maonesho ya 48 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) yanayoendelea Jijini Dar es Salaam.

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Charles Kichere akimsikiliza Kaimu Mkuu wa Sehemu ya Huduma ya Sheria PPAA, Agnes Sayi wakati alipotembelea banda la Mamlaka ya Rufani ya Zabuni za Umma (PPAA) katika Maonesho ya 48 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) yanayoendelea Jijini Dar es Salaam.

Pamoja na mambo mengine, Kaimu Mkuu wa Sehemu ya Huduma ya Sheria PPAA, Agnes Sayi akiongea kwa niaba ya Katibu Mtendaji wa PPAA, James Sando amemueleza CAG kuwa Sheria mpya ya Ununuzi wa Umma ya Mwaka 2023 imeboresha masuala mbalimbali ikiwa ni pamoja kupunguzwa kwa muda wa kushughulikia malalamiko na rufaa zinazotokana na michakato ya Ununuzi wa Umma kutoka siku 45 hadi siku 40.

“Mabadiliko ya Sheria ya Ununuzi yamekuwa yakifanyika mara kwa mara kwa lengo la kupunguza muda, kuongeza uwazi na usawa katika shughuli za ununuzi wa umma, kuongeza ushindani,” alisema Sayi

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Charles Kichere akisaini kitabu cha wageni katika banda la Mamlaka ya Rufani ya Zabuni za Umma (PPAA) katika Maonesho ya 48 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) yanayoendelea Jijini Dar es Salaam.

Kadhalika, Sayi ameongeza kuwa PPAA imefanikiwa kuanzisha Moduli ya kushughulikia malalamiko na rufaa kwa njia kieletroniki ambapo moduli hiyo ipo katika mfumo wa ununuzi wa umma kieletroniki (NeST) ambapo kupitia moduli hiyo wazabuni wataawasilisha malalamiko yao kieletroniki jambo ambalo litasaidia kuokoa muda na gharama.

spot_img

Latest articles

Rais Samia: Walilenga kupindua dola

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa vurugu...

Serikali: Tuchukue hatua kuepuka madhara ya usugu wa vimelea vya magonjwa dhidi ya dawa (UVIDA)

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia kwa Mkurugenzi msaidizi, Kitengo cha Afya Moja, Ofisi ya...

Serikali yawaita wadau kujitokeza kusapoti ushiriki wa wanawake michezoni

Na Winfrida Mtoi Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamis Mwinjuma 'MwanaFA' amewaomba...

Ndejembi awahakikishia wakazi wa Kigamboni umeme wa uhakika

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amefanya ziara ya kikazi ndani ya...

More like this

Rais Samia: Walilenga kupindua dola

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa vurugu...

Serikali: Tuchukue hatua kuepuka madhara ya usugu wa vimelea vya magonjwa dhidi ya dawa (UVIDA)

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia kwa Mkurugenzi msaidizi, Kitengo cha Afya Moja, Ofisi ya...

Serikali yawaita wadau kujitokeza kusapoti ushiriki wa wanawake michezoni

Na Winfrida Mtoi Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamis Mwinjuma 'MwanaFA' amewaomba...