Wanafunzi 250,000 elimu ya juu kukopeshwa Sh bilioni 787

Na Nora Damian

Wanafunzi 250,000 wa vyuo vya kati na elimu ya juu wanatarajia kunufaika na mikopo katika mwaka wa masomo 2024/2025 ambapo Sh bilioni 787 zimetengwa.

Idadi hiyo ya wanafunzi imeongezeka kutoka 224,056 wa mwaka 2023/2024 ambapo watakaonufaika ni wa shahada za awali, stashahada, stashahada ya umahiri katika mafunzo ya sheria kwa vitendo, shahada za umahiri na uzamivu na ruzuku za Samia.

Akizungumza leo Juni 6,2024 wakati wa uzinduzi wa msimu mpya wa uombaji mikopo Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB), Dk. Bill Kiwia, amesema dirisha la kuomba mikopo kwa njia ya mtandao litakuwa wazi kwa siku 90 hadi Agosti 31,2024 na kusisitiza kuwa hawataongeza muda.

“Kwa uzoefu wetu siku 90 zinatosha kwa kuwa mwombaji akiwa amejiandaa na nyaraka zote muhimu inamchukua muda wa dakika 40 kukamilisha maombi yake kwa njia ya mtandao. Hivyo, tunasisitiza waombaji wa mikopo kuzingatia muda uliotolewa kwa kuwa hatutarajii kuongeza baada ya Agosti 31,” amesema Dk. Kiwia.

Amesema pia mwombaji atapaswa kuwa na akaunti ya benki na kwamba kwa waombaji wenye namba za nida watapaswa kuziweka wakati wa kuomba mkopo na kama mwombaji hana anaweza kuendelea na maombi bila namba hiyo.

Mkurugenzi huyo amesisitiza wanafunzi wanaoomba mkopo kusoma na kuzingatia maelekezo yaliyomo katika miongozo ya utoaji mikopo na ruzuku ambayo tayari imewekwa kwenye tovuti ya bodi hiyo ikiwa katika lugha za Kiswahili na Kiingereza.

spot_img

Latest articles

VETA Kuongeza Vyuo Kutoka 80 hadi 152 Kufikia 2027

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) imetangaza mpango...

Mwanasheria Mkuu wa Serikali aongoza zoezi la kutoa huduma za kisheria kwa wananchi

Na Mwandishi Wetu MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza S. Johari amewaongoza Mawakili wa Serikali...

Kliniki ya Sheria yazinduliwa jijini Dar es Salaam

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu...

IST Festival yatumika kunadi mitaji nafuu kwa vijana

Na Mwandishi Wetu TAMASHA la IST Festival lililofanyika jana Februari 14, 2026 kwenye viwanja...

More like this

VETA Kuongeza Vyuo Kutoka 80 hadi 152 Kufikia 2027

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) imetangaza mpango...

Mwanasheria Mkuu wa Serikali aongoza zoezi la kutoa huduma za kisheria kwa wananchi

Na Mwandishi Wetu MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza S. Johari amewaongoza Mawakili wa Serikali...

Kliniki ya Sheria yazinduliwa jijini Dar es Salaam

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu...