Mzee miaka 63 kizimbani kwa kumbaka binti yake

Na Malima Rubasha, Serengeti

Mahakama ya Wilaya ya Serengeti mkoani Mara, imempandisha kizimbani Marwa Masegwe(63) mkazi wa Kijiji cha Kibeyo Kata ya Kisangura kwa kosa la kumbaka binti yake wa kuzaa mwenye umri wa miaka 10 usiku Mei 15 na 16,2024 maeneo ya nyumbani kwake.

Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo, Joseph Mohere, akisoma hati ya mashtaka ameiambia mahakama hiyo kuwa katika kesi jinai namba 14565 ya mwaka 2024, mshtakiwa Marwa Mwita Masegwe mwenye umri wa miaka 63 mkazi wa kijiji cha kibeyo wilayani Serengeti alimbaka binti wa miaka 10 ambaye ni mtoto wake wa kuzaa, siku ya Mei 15 na 16 mwaka huu majira ya usiku nyumbani kwake katika kijiji cha kibeyo.

Hakimu Mohere aliendelea kuieleza mahakama kuwa hali hiyo ilipelekea binti huyo(jina limehifadhiwa) kutoa taarifa kwa majirani ili apate msaada kuhusu kitendo alichofanyiwa na baba yake kwa kuwa walikuwa wanaishi yeye na mdogo wake wa kiume na baba yao mzazi bila kuwepo kwa mzazi mwingine.

Upande wa mashtaka ukiongozwa na Nico Malekela pamoja na Paul Mlelwa umedai kuwa upande wa Jamhuri una mashahidi wanne na kati yao mashahidi watatu ni kutoka Ofisi ya Ustawi wa Jamii Wilaya ya Serengeti, Mganga kutoka hospitali ya Wilaya na Mhanga mwenyewe ambaye ni binti huyo na kwamba mashahidi wametoa ushahidi pasipo shaka yoyote.

Hata hivyo kwa upande wa mshtakiwa alipotakiwa kujitetea dhidi ya kesi hiyo inayomkabili alikana kuhusika kutenda kosa hilo.

Shauri hilo limeahairishwa hadi Juni 17, 2024 hadi kesi itakapotajwa tena na mshtakiwa amerudishwa rumande.

spot_img

Latest articles

VETA yajivunia mageuzi makubwa, yazidi kuwanufaisha Watanzania

Na Tatu Mohamed MAMLAKA ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) imesema inajivunia mafanikio...

TPDC yapata Tuzo ya Taasisi Bora Sabasaba kwa miaka mitano mfululizo

Na Tatu Mohamed SHIRIKA la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) limeandika historia kwa kutwaa tuzo...

Rais Mwinyi atembelea Banda la ETDCO Sabasaba

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein...

GF Trucks yaibuka mshindi wa jumla maonesho ya Sabasaba 2025

Na Mwandishi Wetu Kampuni ya Gf Trucks & Equipment imeibuka mshindi wa jumla katika Maonesho...

More like this

VETA yajivunia mageuzi makubwa, yazidi kuwanufaisha Watanzania

Na Tatu Mohamed MAMLAKA ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) imesema inajivunia mafanikio...

TPDC yapata Tuzo ya Taasisi Bora Sabasaba kwa miaka mitano mfululizo

Na Tatu Mohamed SHIRIKA la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) limeandika historia kwa kutwaa tuzo...

Rais Mwinyi atembelea Banda la ETDCO Sabasaba

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein...