Mzee miaka 63 kizimbani kwa kumbaka binti yake

Na Malima Rubasha, Serengeti

Mahakama ya Wilaya ya Serengeti mkoani Mara, imempandisha kizimbani Marwa Masegwe(63) mkazi wa Kijiji cha Kibeyo Kata ya Kisangura kwa kosa la kumbaka binti yake wa kuzaa mwenye umri wa miaka 10 usiku Mei 15 na 16,2024 maeneo ya nyumbani kwake.

Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo, Joseph Mohere, akisoma hati ya mashtaka ameiambia mahakama hiyo kuwa katika kesi jinai namba 14565 ya mwaka 2024, mshtakiwa Marwa Mwita Masegwe mwenye umri wa miaka 63 mkazi wa kijiji cha kibeyo wilayani Serengeti alimbaka binti wa miaka 10 ambaye ni mtoto wake wa kuzaa, siku ya Mei 15 na 16 mwaka huu majira ya usiku nyumbani kwake katika kijiji cha kibeyo.

Hakimu Mohere aliendelea kuieleza mahakama kuwa hali hiyo ilipelekea binti huyo(jina limehifadhiwa) kutoa taarifa kwa majirani ili apate msaada kuhusu kitendo alichofanyiwa na baba yake kwa kuwa walikuwa wanaishi yeye na mdogo wake wa kiume na baba yao mzazi bila kuwepo kwa mzazi mwingine.

Upande wa mashtaka ukiongozwa na Nico Malekela pamoja na Paul Mlelwa umedai kuwa upande wa Jamhuri una mashahidi wanne na kati yao mashahidi watatu ni kutoka Ofisi ya Ustawi wa Jamii Wilaya ya Serengeti, Mganga kutoka hospitali ya Wilaya na Mhanga mwenyewe ambaye ni binti huyo na kwamba mashahidi wametoa ushahidi pasipo shaka yoyote.

Hata hivyo kwa upande wa mshtakiwa alipotakiwa kujitetea dhidi ya kesi hiyo inayomkabili alikana kuhusika kutenda kosa hilo.

Shauri hilo limeahairishwa hadi Juni 17, 2024 hadi kesi itakapotajwa tena na mshtakiwa amerudishwa rumande.

spot_img

Latest articles

TUNATAMANI KUWA MABALOZI WA VIPIMO – WANAFUNZI MWANZA

Na WMA - Mwanza WANAFUNZI kutoka shule mbalimbali za Msingi na Sekondari jijini Mwanza wameomba...

Msajili wa Hazina ataka mageuzi makubwa TBC

Na Mwandishi wa OTR MSAJILI wa Hazina, Bw. Nehemiah Mchechu, ametaka kufanyika kwa mageuzi makubwa...

CRDB YAZINDUA UGHAIBUNI LOAN KUSAIDIA WATANZANIA WALIOPATA AJIRA NJE YA NCHI

Na Mwandishi Wetu BENKI ya CRDB imezindua rasmi huduma ya mkopo ya Ughaibuni yenye...

Ofisi ya Msajili wa Hazina kuimarisha ushirikiano na taasisi za umma za China

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina (OTR) iko katika hatua za mwisho za...

More like this

TUNATAMANI KUWA MABALOZI WA VIPIMO – WANAFUNZI MWANZA

Na WMA - Mwanza WANAFUNZI kutoka shule mbalimbali za Msingi na Sekondari jijini Mwanza wameomba...

Msajili wa Hazina ataka mageuzi makubwa TBC

Na Mwandishi wa OTR MSAJILI wa Hazina, Bw. Nehemiah Mchechu, ametaka kufanyika kwa mageuzi makubwa...

CRDB YAZINDUA UGHAIBUNI LOAN KUSAIDIA WATANZANIA WALIOPATA AJIRA NJE YA NCHI

Na Mwandishi Wetu BENKI ya CRDB imezindua rasmi huduma ya mkopo ya Ughaibuni yenye...