Mtu mmoja afariki katika ajali ya ndege ya shirika la ndege la Singapore kutoka London

Bangkok, Thailand

Mtu mmoja amefariki dunia na wengine kadhaa kujeruhiwa leo wakati ndege ya shirika la ndege la Singapore kutoka London Uingereza kuekea Singapore ilipokumbwa na msukosuko mkubwa, shirika hilo la ndege limethibitisha.

Ndege hiyo aina ya Boeing 777-300ER ilielekezwa kwenye Uwanja wa Ndege wa Suvarnabhumi huko Bangkok, Thailand, ambako ilitua kwa dharura saa 3:45pm (08:45 GMT) leo Jumanne.

Ndege ya SQ321 “ilikumbana na msukosuko mkubwa njiani,” Shirika la Ndege la Singapore limeeleza katika taarifa kwenye ukurasa wake wa Facebook.

“Tunaweza kuthibitisha kuwa kuna majeruhi na mtu mmoja aliyefariki kwenye ndege ya Boeing 777-300ER,” ilisema.

Saa nne baada ya kutua kwa dharura, watu 18 walisalia hospitalini huku wengine 12 wakitibiwa kwa msingi wa wagonjwa wa nje, imeeleza taarifa hiyo.

“Abiria na wafanyakazi waliosalia wanachunguzwa na kupewa matibabu, inapobidi,” iliongeza.

Ndege hiyo ilikuwa na abiria 211 na wahudumu 18.

Kittipong Kittikachorn, meneja mkuu wa Uwanja wa ndege wa Suvarnabhumi, aliambia mkutano wa wanahabari kwamba mwathiriwa alikuwa Muingereza ambaye alionekana kuwa na mshtuko wa moyo.

Kundi la Viwanja vya Ndege vya Thailand lilisema abiria waliojeruhiwa kidogo na ambao hawajajeruhiwa wanasaidiwa katika eneo maalum lililowekwa ndani ya kituo kwenye Uwanja wa Ndege wa Suvarnabhumi.

spot_img

Latest articles

Kuelekea Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani: TRA Yakabidhi Vifaa Tiba Vyenye Thamani ya Milioni 40

Na Tatu Mohamed KUELEKEA maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yanayoadhimishwa kila mwaka Machi 8,...

UWT Makangarawe watoa msaada kwa watoto wenye mahitaji maalum kuelekea Siku ya Wanawake Duniani

Na Tatu Mohamed KATIKA kuelekea maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, Umoja wa Wanawake...

‘Makomandoo’ wazitia hasara Simba na Yanga

Na Mwandishi Wetu KLABU za Simba na Yanga zimetozwa faini ta sh.5,000,000 kila moja kwa...

Mwamuzi aliyekataa bao la Simba Zanzibar afungiwa

Na Mwandishi Wetu MWAMUZI Kassim Mpanga Mpanga wa Dar es Salaam, amefungiwa miezi sita  kosa...

More like this

Kuelekea Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani: TRA Yakabidhi Vifaa Tiba Vyenye Thamani ya Milioni 40

Na Tatu Mohamed KUELEKEA maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yanayoadhimishwa kila mwaka Machi 8,...

UWT Makangarawe watoa msaada kwa watoto wenye mahitaji maalum kuelekea Siku ya Wanawake Duniani

Na Tatu Mohamed KATIKA kuelekea maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, Umoja wa Wanawake...

‘Makomandoo’ wazitia hasara Simba na Yanga

Na Mwandishi Wetu KLABU za Simba na Yanga zimetozwa faini ta sh.5,000,000 kila moja kwa...