Mtu mmoja afariki katika ajali ya ndege ya shirika la ndege la Singapore kutoka London

Bangkok, Thailand

Mtu mmoja amefariki dunia na wengine kadhaa kujeruhiwa leo wakati ndege ya shirika la ndege la Singapore kutoka London Uingereza kuekea Singapore ilipokumbwa na msukosuko mkubwa, shirika hilo la ndege limethibitisha.

Ndege hiyo aina ya Boeing 777-300ER ilielekezwa kwenye Uwanja wa Ndege wa Suvarnabhumi huko Bangkok, Thailand, ambako ilitua kwa dharura saa 3:45pm (08:45 GMT) leo Jumanne.

Ndege ya SQ321 “ilikumbana na msukosuko mkubwa njiani,” Shirika la Ndege la Singapore limeeleza katika taarifa kwenye ukurasa wake wa Facebook.

“Tunaweza kuthibitisha kuwa kuna majeruhi na mtu mmoja aliyefariki kwenye ndege ya Boeing 777-300ER,” ilisema.

Saa nne baada ya kutua kwa dharura, watu 18 walisalia hospitalini huku wengine 12 wakitibiwa kwa msingi wa wagonjwa wa nje, imeeleza taarifa hiyo.

“Abiria na wafanyakazi waliosalia wanachunguzwa na kupewa matibabu, inapobidi,” iliongeza.

Ndege hiyo ilikuwa na abiria 211 na wahudumu 18.

Kittipong Kittikachorn, meneja mkuu wa Uwanja wa ndege wa Suvarnabhumi, aliambia mkutano wa wanahabari kwamba mwathiriwa alikuwa Muingereza ambaye alionekana kuwa na mshtuko wa moyo.

Kundi la Viwanja vya Ndege vya Thailand lilisema abiria waliojeruhiwa kidogo na ambao hawajajeruhiwa wanasaidiwa katika eneo maalum lililowekwa ndani ya kituo kwenye Uwanja wa Ndege wa Suvarnabhumi.

spot_img

Latest articles

DC Mpogolo: viongozi wa Serikali za Mitaa ni watu muhimu Katika Usimamizi wa Huduma za Umeme

Na Tatu Mohamed VIONGOZI wa Serikali za Mitaa wametajwa kuwa watu muhimu katika kusimamia miundo...

Rais Samia aagiza Tume kuchunguza, kujua haki wanayoidai vijana

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk.Samia Suluhu Hassan ameielekeza Tume...

Bado denial inasuta nafsi za wengi, hatuwezi kupona

LEO ni siku ya 23 tangu risasi ya kwanza ilipofyatuliwa na kuua vijana waliokuwa...

Watoto mapacha wajinyonga Zanzibar, kisa kazi za ndani

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba linachunguza tukio la kujinyonga kwa...

More like this

DC Mpogolo: viongozi wa Serikali za Mitaa ni watu muhimu Katika Usimamizi wa Huduma za Umeme

Na Tatu Mohamed VIONGOZI wa Serikali za Mitaa wametajwa kuwa watu muhimu katika kusimamia miundo...

Rais Samia aagiza Tume kuchunguza, kujua haki wanayoidai vijana

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk.Samia Suluhu Hassan ameielekeza Tume...

Bado denial inasuta nafsi za wengi, hatuwezi kupona

LEO ni siku ya 23 tangu risasi ya kwanza ilipofyatuliwa na kuua vijana waliokuwa...