Julio akabidhiwa Singida

Na Winfrida Mtoi

Siku chache baada ya kuvunja benchi lote la ufundi lililokuwa likiongozwa na Thabo Senong, uongozi wa Singida Fountain Gate umemtambulisha Jamhuri Kiwelu kuwa kocha mkuu wa kikosi hicho hadi mwisho wa msimu huu.

Timu hiyo imekuwa na matokeo yasiyoridhisha tangu baadhi ya wachezaji wake kutimkia Ihefu FC kipindi cha dirisha dogo kwa kupokea vichapo mfululizo.

Mchezo uliopita timu hiyo imepokea kichapo cha mabao 3-1 kutoka kwa Simba, Uwanja wa Azam Complex, kabla ya hapo ilitoka kufungwa na Mtibwa Sugar 2-0, CCM Kirumba, Mwanza.

Akizungumzia mabadiliko hayo, Rais wa Klabu ya Singida Fountain Gate, Japhet Makau, amesema mabadiliko hayo ni baada ya kubaini  upungufu kwenye benchi la ufundi, hivyo anaamini wanakwenda kuimarika sasa.

“Kocha mkuu anakuwa Julio akisaidiana na Ngawina Ngawina, pia tumemrudisha nyumbani Bartez (Ali Mustapha kocha wa makipa), tunaamini chini ya benchi hili tunakwenda kuimarika na tunaanza na mechi inayofuata dhidi ya Namungo, naamini mambo yatakuwa mazuri,” amesema Makau.

spot_img

Latest articles

SMZ yapongeza udhamini mnono wa NMB Mapinduzi Cup

Na Mwandishi Wetu, Zanzibar SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ), imeipongeza Benki ya NMB kwa...

Mwakinyo ashinda kwa K.O, afichua siri

Na Winfrida Mtoi Bondia wa ngumi za kulipwa nchini, Hassan Mwakinyo ameibuka mshindi kwa K.O...

Mwakinyo kuilipia kisasi Taifa Stars dhidi ya Mnigeria kesho, Furahi apania rekodi

Na Winfrida Mtoi BONDIA wa kimataifa wa Tanzania, Hassan Mwakinyo, ameweka bayana kuwa pambano lake...

Serikali kuendelea kuwawezesha vijana kijamii, kiuchumi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Joel...

More like this

SMZ yapongeza udhamini mnono wa NMB Mapinduzi Cup

Na Mwandishi Wetu, Zanzibar SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ), imeipongeza Benki ya NMB kwa...

Mwakinyo ashinda kwa K.O, afichua siri

Na Winfrida Mtoi Bondia wa ngumi za kulipwa nchini, Hassan Mwakinyo ameibuka mshindi kwa K.O...

Mwakinyo kuilipia kisasi Taifa Stars dhidi ya Mnigeria kesho, Furahi apania rekodi

Na Winfrida Mtoi BONDIA wa kimataifa wa Tanzania, Hassan Mwakinyo, ameweka bayana kuwa pambano lake...