Julio akabidhiwa Singida

Na Winfrida Mtoi

Siku chache baada ya kuvunja benchi lote la ufundi lililokuwa likiongozwa na Thabo Senong, uongozi wa Singida Fountain Gate umemtambulisha Jamhuri Kiwelu kuwa kocha mkuu wa kikosi hicho hadi mwisho wa msimu huu.

Timu hiyo imekuwa na matokeo yasiyoridhisha tangu baadhi ya wachezaji wake kutimkia Ihefu FC kipindi cha dirisha dogo kwa kupokea vichapo mfululizo.

Mchezo uliopita timu hiyo imepokea kichapo cha mabao 3-1 kutoka kwa Simba, Uwanja wa Azam Complex, kabla ya hapo ilitoka kufungwa na Mtibwa Sugar 2-0, CCM Kirumba, Mwanza.

Akizungumzia mabadiliko hayo, Rais wa Klabu ya Singida Fountain Gate, Japhet Makau, amesema mabadiliko hayo ni baada ya kubaini  upungufu kwenye benchi la ufundi, hivyo anaamini wanakwenda kuimarika sasa.

“Kocha mkuu anakuwa Julio akisaidiana na Ngawina Ngawina, pia tumemrudisha nyumbani Bartez (Ali Mustapha kocha wa makipa), tunaamini chini ya benchi hili tunakwenda kuimarika na tunaanza na mechi inayofuata dhidi ya Namungo, naamini mambo yatakuwa mazuri,” amesema Makau.

spot_img

Latest articles

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...

Rais Samia: Walilenga kupindua dola

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa vurugu...

Serikali: Tuchukue hatua kuepuka madhara ya usugu wa vimelea vya magonjwa dhidi ya dawa (UVIDA)

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia kwa Mkurugenzi msaidizi, Kitengo cha Afya Moja, Ofisi ya...

Serikali yawaita wadau kujitokeza kusapoti ushiriki wa wanawake michezoni

Na Winfrida Mtoi Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamis Mwinjuma 'MwanaFA' amewaomba...

More like this

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...

Rais Samia: Walilenga kupindua dola

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa vurugu...

Serikali: Tuchukue hatua kuepuka madhara ya usugu wa vimelea vya magonjwa dhidi ya dawa (UVIDA)

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia kwa Mkurugenzi msaidizi, Kitengo cha Afya Moja, Ofisi ya...