Julio akabidhiwa Singida

Na Winfrida Mtoi

Siku chache baada ya kuvunja benchi lote la ufundi lililokuwa likiongozwa na Thabo Senong, uongozi wa Singida Fountain Gate umemtambulisha Jamhuri Kiwelu kuwa kocha mkuu wa kikosi hicho hadi mwisho wa msimu huu.

Timu hiyo imekuwa na matokeo yasiyoridhisha tangu baadhi ya wachezaji wake kutimkia Ihefu FC kipindi cha dirisha dogo kwa kupokea vichapo mfululizo.

Mchezo uliopita timu hiyo imepokea kichapo cha mabao 3-1 kutoka kwa Simba, Uwanja wa Azam Complex, kabla ya hapo ilitoka kufungwa na Mtibwa Sugar 2-0, CCM Kirumba, Mwanza.

Akizungumzia mabadiliko hayo, Rais wa Klabu ya Singida Fountain Gate, Japhet Makau, amesema mabadiliko hayo ni baada ya kubaini  upungufu kwenye benchi la ufundi, hivyo anaamini wanakwenda kuimarika sasa.

“Kocha mkuu anakuwa Julio akisaidiana na Ngawina Ngawina, pia tumemrudisha nyumbani Bartez (Ali Mustapha kocha wa makipa), tunaamini chini ya benchi hili tunakwenda kuimarika na tunaanza na mechi inayofuata dhidi ya Namungo, naamini mambo yatakuwa mazuri,” amesema Makau.

spot_img

Latest articles

Serikali yajipanga kuimarisha utumishi wa umma, kuendeleza mageuzi ya kidigitali

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa...

Bokya amtahadharisha mapema Tyson wa Bongo

Na Winfrida Mtoi Bondia Ismail Khalid maarufu Boyka ametamba kutoa kipigo kikali kwa mpinza wake...

Mwili wa Jenista Mhagama Kuzikwa Jumanne Mbinga, Ruvuma

Na Mwandishi Wetu MWILI wa aliyekuwa Mbunge wa Peramiho (CCM), Jenista Mhagama unatarajiwa kuzikwa...

Mradi wa upanuzi Kituo cha kupokea na kupoza umeme cha Kinyerezi I Extension umekamilika

Na Mwandishi Wetu NAIBU Waziri wa Nishati, Salome Makamba, amesema kuwa mradi wa upanuzi...

More like this

Serikali yajipanga kuimarisha utumishi wa umma, kuendeleza mageuzi ya kidigitali

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa...

Bokya amtahadharisha mapema Tyson wa Bongo

Na Winfrida Mtoi Bondia Ismail Khalid maarufu Boyka ametamba kutoa kipigo kikali kwa mpinza wake...

Mwili wa Jenista Mhagama Kuzikwa Jumanne Mbinga, Ruvuma

Na Mwandishi Wetu MWILI wa aliyekuwa Mbunge wa Peramiho (CCM), Jenista Mhagama unatarajiwa kuzikwa...