Julio akabidhiwa Singida

Na Winfrida Mtoi

Siku chache baada ya kuvunja benchi lote la ufundi lililokuwa likiongozwa na Thabo Senong, uongozi wa Singida Fountain Gate umemtambulisha Jamhuri Kiwelu kuwa kocha mkuu wa kikosi hicho hadi mwisho wa msimu huu.

Timu hiyo imekuwa na matokeo yasiyoridhisha tangu baadhi ya wachezaji wake kutimkia Ihefu FC kipindi cha dirisha dogo kwa kupokea vichapo mfululizo.

Mchezo uliopita timu hiyo imepokea kichapo cha mabao 3-1 kutoka kwa Simba, Uwanja wa Azam Complex, kabla ya hapo ilitoka kufungwa na Mtibwa Sugar 2-0, CCM Kirumba, Mwanza.

Akizungumzia mabadiliko hayo, Rais wa Klabu ya Singida Fountain Gate, Japhet Makau, amesema mabadiliko hayo ni baada ya kubaini  upungufu kwenye benchi la ufundi, hivyo anaamini wanakwenda kuimarika sasa.

“Kocha mkuu anakuwa Julio akisaidiana na Ngawina Ngawina, pia tumemrudisha nyumbani Bartez (Ali Mustapha kocha wa makipa), tunaamini chini ya benchi hili tunakwenda kuimarika na tunaanza na mechi inayofuata dhidi ya Namungo, naamini mambo yatakuwa mazuri,” amesema Makau.

spot_img

Latest articles

Maboresho ya mitambo ya kufua umeme Mtera yaimarisha uzalishaji umeme

Na Mwandishi Wetu, Mtera NAIBU Waziri wa Nishati, Salome Makamba, Novemba 26, 2025, alitembelea na...

Ndejembi: Tanzania sasa ina umeme wa kutosha

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amesema Tanzania kwa sasa ina umeme...

Jeshi la Polisi lachunguza  taarifa ya OCD  Chunya

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi limesema limeona na linafanyia uchunguzi taarifa inayosambaa kwenye mitandao...

Uwanja wa Mkwakwani wafungiwa

Na Mwandishi Wetu SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF), limeufungia Uwanja wa Mkwakwani, Tanga kutumika kwa...

More like this

Maboresho ya mitambo ya kufua umeme Mtera yaimarisha uzalishaji umeme

Na Mwandishi Wetu, Mtera NAIBU Waziri wa Nishati, Salome Makamba, Novemba 26, 2025, alitembelea na...

Ndejembi: Tanzania sasa ina umeme wa kutosha

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amesema Tanzania kwa sasa ina umeme...

Jeshi la Polisi lachunguza  taarifa ya OCD  Chunya

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi limesema limeona na linafanyia uchunguzi taarifa inayosambaa kwenye mitandao...