Biden: Tendo la ndoa siri ya furaha kwenye ndoa

Rais Joe Biden wa Marekani amewaasa wasaidizi wake kwamba siri ya ndoa ya muda mrefu na ya kudumu ni “tendo la ndoa.” Kitabu kipya kuhusu mke wa rais, Jill Biden ambacho kinaangazia ndoa yao iliyodumu kwa miaka 47 sasa, kinalitaja ‘Tendo la ndoa’ kuwa ndio kirutubisho muhimu zaidi katika ndoa.

Kitabu hicho “American Woman – The Transformation of the Modern First Lady, from Hillary Clinton to Jill Biden,” kimeandikwa na mwandishi wa New York Times katika Ikulu ya White House, Katie Rogers na kinatarajiwa kutoka wiki hii.

Sehemu inayohusu ngono inachukua vifungu vichache tu katika kitabu hicho chenye kurasa 276, lakini tayari maudhui hayo yameibua mjadala mkubwa mitandaoni na kugonga vichwa vya habari sehemu mbalimbali duniani.

Jill Tracy Jacobs Biden, mke wa pili na wa sasa wa Biden, alizaliwa Juni 3, 1951. Alikutana na Biden Machi 1975. Kitabu hiki pia kinaelezea uchungu wa Biden alioupata baada ya mke wake wa kwanza, Neilia, kufariki katika ajali ya gari mwaka wa 1972 pamoja na binti yao Naomi.

Je unakubaliana na kauli hii ya rais Biden?

spot_img

Latest articles

Neema Mchau ajitosa kugombea Udiwani Viti Maalum Ilala

Na Mwandishi Wetu MWENYEKITI wa Jukwaa la Wanawake Kata ya Gongolamboto Neema Mchau amechukua fomu...

Amanzi na Babu Tale uso kwa uso Jimboni

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Katibu wa Umoja wa Vijana wa CCM Tawi la Chuo...

VETA Pwani yabuni Mita ya Maji ya Kisasa, kutatua migogoro kwa wapangaji

Na Tatu Mohamed KATIKA hatua ya kuleta mageuzi katika usimamizi wa matumizi ya maji...

Ofisi ya Msajili Hazina yazitaka taasisi za umma kutumia maonesho ya Sabasaba kutangaza huduma

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili Hazina yazitaka taasisi za umma kutumia maonesho ...

More like this

Neema Mchau ajitosa kugombea Udiwani Viti Maalum Ilala

Na Mwandishi Wetu MWENYEKITI wa Jukwaa la Wanawake Kata ya Gongolamboto Neema Mchau amechukua fomu...

Amanzi na Babu Tale uso kwa uso Jimboni

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Katibu wa Umoja wa Vijana wa CCM Tawi la Chuo...

VETA Pwani yabuni Mita ya Maji ya Kisasa, kutatua migogoro kwa wapangaji

Na Tatu Mohamed KATIKA hatua ya kuleta mageuzi katika usimamizi wa matumizi ya maji...