Biden: Tendo la ndoa siri ya furaha kwenye ndoa

Rais Joe Biden wa Marekani amewaasa wasaidizi wake kwamba siri ya ndoa ya muda mrefu na ya kudumu ni “tendo la ndoa.” Kitabu kipya kuhusu mke wa rais, Jill Biden ambacho kinaangazia ndoa yao iliyodumu kwa miaka 47 sasa, kinalitaja ‘Tendo la ndoa’ kuwa ndio kirutubisho muhimu zaidi katika ndoa.

Kitabu hicho “American Woman – The Transformation of the Modern First Lady, from Hillary Clinton to Jill Biden,” kimeandikwa na mwandishi wa New York Times katika Ikulu ya White House, Katie Rogers na kinatarajiwa kutoka wiki hii.

Sehemu inayohusu ngono inachukua vifungu vichache tu katika kitabu hicho chenye kurasa 276, lakini tayari maudhui hayo yameibua mjadala mkubwa mitandaoni na kugonga vichwa vya habari sehemu mbalimbali duniani.

Jill Tracy Jacobs Biden, mke wa pili na wa sasa wa Biden, alizaliwa Juni 3, 1951. Alikutana na Biden Machi 1975. Kitabu hiki pia kinaelezea uchungu wa Biden alioupata baada ya mke wake wa kwanza, Neilia, kufariki katika ajali ya gari mwaka wa 1972 pamoja na binti yao Naomi.

Je unakubaliana na kauli hii ya rais Biden?

spot_img

Latest articles

Waziri wa Nishati Ndejembi azindua rasmi mita janja

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amezindua rasmi mita janja (smart meter)...

RC Kunenge: Mto Ruvu ubaki kwa matumizi ya binadamu tu, tusitishe shughuli nyingine kwa muda

Na Mwandishi Wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, ametoa wito kwa wakulima...

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...

Rais Samia: Walilenga kupindua dola

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa vurugu...

More like this

Waziri wa Nishati Ndejembi azindua rasmi mita janja

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amezindua rasmi mita janja (smart meter)...

RC Kunenge: Mto Ruvu ubaki kwa matumizi ya binadamu tu, tusitishe shughuli nyingine kwa muda

Na Mwandishi Wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, ametoa wito kwa wakulima...

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...