PSSSF yapewa siku 100 kukamilisha ujenzi kiwanda cha ngozi

Na Mwandishi Wetu, Kilimanjaro

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Mhandisi Cyprian Luhemeja ametoa siku 100 kwa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Wafanyakazi wa Umma (PSSSF) kuhakikisha awamu ya pili ya ujenzi wa kiwanda cha kuchakata bidhaa za ngozi Kilimanjaro unakamilika na kuanza kufanya kazi ifikapo Julai 2024.

Agizo hilo amelitoa leo Februari 22,2024 alipofanya ziara ya kukagua ujenzi katika kiwanda cha bidhaa za ngozi Kilimanjaro International Leather Industries Ltd (KLICL) ikiwa ni sehemu ya kukagua maendeleo ya miradi inayotekelezwa na serikali kupitia ofisi hiyo.

Mhandisi Luhemeja amesema kukamilika kwa kiwanda hicho kutaongeza thamani ya zao la ngozi ghafi, kufungua fursa za soko la uhakika la ngozi kutoka kwa wafugaji, kuongeza ajira kwa vijana na mapato ya fedha za ndani na za kigeni.

Aidha, amefurahishwa na ubora wa bidhaa zinazozalishwa kiwandani hapo na kutoa wito kwa Watanzania kuwa na tamaduni za kuthamini bidhaa zinazozalishwa nchini.

Awali Mkurugenzi Mkuu wa PSSSF, Abdul-Razaq Badru, amesema amepokea maagizo hayo na kuahidi kuwa watashirikiana na Jeshi la Magereza kuhakikisha wanafanya kazi kwa weledi kama ilivyoelekezwa ili Watanzania waanze kunufaika na mradi huo.

Naye, Mkurugenzi Mtendaji wa Kiwanda hicho, Mhandisi Saiba Edward, amesema mradi huo utaongeza kipato kwa wakazi wa Kilimanjaro na mikoa jirani kupitia fursa za uzabuni, uwakala na usambazaji wa bidhaa.

Kwa upande wake Kamishina Msaidizi wa Jeshi la Magereza, Frank Mwakijungu, amesema Magereza ni mbia wa utekelezaji mradi huo hivyo watasimamia ujenzi wa kiwanda hicho ili kikamilike kwa wakati kwa manufaa ya Watanzania.

spot_img

Latest articles

Ridhiwani:Niko tayari kuhojiwa kuhusu tuhuma za Lake Oil

Na Mwandishi Wetu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na...

Ndejembi: Ufanisi wa Tanesco katika utekelezaji na Usimamizi wa miradi umeleta mfumo madhubuti wa Nishati

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, amesema kuwa Shirika la Umeme...

Maboresho ya mitambo ya kufua umeme Mtera yaimarisha uzalishaji umeme

Na Mwandishi Wetu, Mtera NAIBU Waziri wa Nishati, Salome Makamba, Novemba 26, 2025, alitembelea na...

Ndejembi: Tanzania sasa ina umeme wa kutosha

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amesema Tanzania kwa sasa ina umeme...

More like this

Ridhiwani:Niko tayari kuhojiwa kuhusu tuhuma za Lake Oil

Na Mwandishi Wetu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na...

Ndejembi: Ufanisi wa Tanesco katika utekelezaji na Usimamizi wa miradi umeleta mfumo madhubuti wa Nishati

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, amesema kuwa Shirika la Umeme...

Maboresho ya mitambo ya kufua umeme Mtera yaimarisha uzalishaji umeme

Na Mwandishi Wetu, Mtera NAIBU Waziri wa Nishati, Salome Makamba, Novemba 26, 2025, alitembelea na...