PSSSF yapewa siku 100 kukamilisha ujenzi kiwanda cha ngozi

Na Mwandishi Wetu, Kilimanjaro

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Mhandisi Cyprian Luhemeja ametoa siku 100 kwa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Wafanyakazi wa Umma (PSSSF) kuhakikisha awamu ya pili ya ujenzi wa kiwanda cha kuchakata bidhaa za ngozi Kilimanjaro unakamilika na kuanza kufanya kazi ifikapo Julai 2024.

Agizo hilo amelitoa leo Februari 22,2024 alipofanya ziara ya kukagua ujenzi katika kiwanda cha bidhaa za ngozi Kilimanjaro International Leather Industries Ltd (KLICL) ikiwa ni sehemu ya kukagua maendeleo ya miradi inayotekelezwa na serikali kupitia ofisi hiyo.

Mhandisi Luhemeja amesema kukamilika kwa kiwanda hicho kutaongeza thamani ya zao la ngozi ghafi, kufungua fursa za soko la uhakika la ngozi kutoka kwa wafugaji, kuongeza ajira kwa vijana na mapato ya fedha za ndani na za kigeni.

Aidha, amefurahishwa na ubora wa bidhaa zinazozalishwa kiwandani hapo na kutoa wito kwa Watanzania kuwa na tamaduni za kuthamini bidhaa zinazozalishwa nchini.

Awali Mkurugenzi Mkuu wa PSSSF, Abdul-Razaq Badru, amesema amepokea maagizo hayo na kuahidi kuwa watashirikiana na Jeshi la Magereza kuhakikisha wanafanya kazi kwa weledi kama ilivyoelekezwa ili Watanzania waanze kunufaika na mradi huo.

Naye, Mkurugenzi Mtendaji wa Kiwanda hicho, Mhandisi Saiba Edward, amesema mradi huo utaongeza kipato kwa wakazi wa Kilimanjaro na mikoa jirani kupitia fursa za uzabuni, uwakala na usambazaji wa bidhaa.

Kwa upande wake Kamishina Msaidizi wa Jeshi la Magereza, Frank Mwakijungu, amesema Magereza ni mbia wa utekelezaji mradi huo hivyo watasimamia ujenzi wa kiwanda hicho ili kikamilike kwa wakati kwa manufaa ya Watanzania.

spot_img

Latest articles

Mwanasheria Mkuu wa Serikali: Uchaguzi Mkuu wa 2025 ni halali

Na Mwandishi wetu MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza Johari amesema kuwa, Uchaguzi Mkuu wa...

Viongozi wa dini waendelea kihimiza amani uchaguzi mkuu

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam VIONGOZI wa dini nchini wameendelea kuhimiza umuhimu wa kudumisha...

Ujumbe wa viongozi wa dini kuelekea uchaguzi mkuu Oktoba 29, 2025 katika Kongamano la Kamati ya Amani Kitaifa Dar es Salaam

Na Mwandishi Wetu Askofu Mkuu Wapo Mission, Dk. Sylvester Gamanywa “Mungu ambaye tunamwakilisha ndiye anayweka watawala...

Watumishi wa umma waaswa kushiriki Uchaguzi wa Oktoba 29

Dar es Salaam. Ofisi ya Msajili wa Hazina (OMH) imetoa wito kwa watumishi wote...

More like this

Mwanasheria Mkuu wa Serikali: Uchaguzi Mkuu wa 2025 ni halali

Na Mwandishi wetu MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza Johari amesema kuwa, Uchaguzi Mkuu wa...

Viongozi wa dini waendelea kihimiza amani uchaguzi mkuu

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam VIONGOZI wa dini nchini wameendelea kuhimiza umuhimu wa kudumisha...

Ujumbe wa viongozi wa dini kuelekea uchaguzi mkuu Oktoba 29, 2025 katika Kongamano la Kamati ya Amani Kitaifa Dar es Salaam

Na Mwandishi Wetu Askofu Mkuu Wapo Mission, Dk. Sylvester Gamanywa “Mungu ambaye tunamwakilisha ndiye anayweka watawala...