Watanzania washinda milioni 234 za AGT, Rais Samia awapongeza


Na Mwandishi wetu

Wanasarakasi wawili watanzania ambao ni ndugu, Fadhil Ramadhani na Ibrahim Job, wameshinda kitita cha fedha cha dola za Kimarekani 250,000 sawa na sh 634 milioni baada ya kuibuka washindi wa American Got Talent (AGT) Fantasy League.

Watanzania hao wanaounda kikundi cha sarakasi kinachoitwa Ramadhani  Brothers, waliibuka washindi usiku wa jana Februari 19,2024 kwa kuwashinda wapinzani wao wengine tisa waliofika nao fainali.

Kupitia ukurasa wao wa Instagram baada ya kutangazwa washindi katika usiku huo, wamesema ni ushindi wa kushangaza kwao na kuwashukuru wote waliowapa sapoti.

Wamesema wanajivunia  kutangazwa wabingwa wa dunia wa mashindano, huku wakiwapokeza washindani wenzao  ambao wamewafanya wawe bora zaidi.

Katika hatua nyingine Rais Dk. Samia Suluhu Hassan amewapongeza washindi hao kutokana na kuitangaza vema Tanzania.

“Pongezi kwa vijana wetu Fadhil na Ibrahim (The Ramadhan Brothers) kwa kuibuka washindi katika mashindano ya sanaa na burudani ya AGT: Fantasy League, safari yenu inaendelea kudhihirisha kuwa juhudi, nidhamu, kujituma na kujiamini ni nguzo muhimu kufikia mafanikio. Mnaitangaza vyema nchi yetu na kuweka mfano bora kwa wengine,” amesema Rais Samia.

spot_img

Latest articles

Mwanasheria Mkuu wa Serikali: Uchaguzi Mkuu wa 2025 ni halali

Na Mwandishi wetu MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza Johari amesema kuwa, Uchaguzi Mkuu wa...

Viongozi wa dini waendelea kihimiza amani uchaguzi mkuu

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam VIONGOZI wa dini nchini wameendelea kuhimiza umuhimu wa kudumisha...

Ujumbe wa viongozi wa dini kuelekea uchaguzi mkuu Oktoba 29, 2025 katika Kongamano la Kamati ya Amani Kitaifa Dar es Salaam

Na Mwandishi Wetu Askofu Mkuu Wapo Mission, Dk. Sylvester Gamanywa “Mungu ambaye tunamwakilisha ndiye anayweka watawala...

Watumishi wa umma waaswa kushiriki Uchaguzi wa Oktoba 29

Dar es Salaam. Ofisi ya Msajili wa Hazina (OMH) imetoa wito kwa watumishi wote...

More like this

Mwanasheria Mkuu wa Serikali: Uchaguzi Mkuu wa 2025 ni halali

Na Mwandishi wetu MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza Johari amesema kuwa, Uchaguzi Mkuu wa...

Viongozi wa dini waendelea kihimiza amani uchaguzi mkuu

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam VIONGOZI wa dini nchini wameendelea kuhimiza umuhimu wa kudumisha...

Ujumbe wa viongozi wa dini kuelekea uchaguzi mkuu Oktoba 29, 2025 katika Kongamano la Kamati ya Amani Kitaifa Dar es Salaam

Na Mwandishi Wetu Askofu Mkuu Wapo Mission, Dk. Sylvester Gamanywa “Mungu ambaye tunamwakilisha ndiye anayweka watawala...