Watanzania washinda milioni 234 za AGT, Rais Samia awapongeza


Na Mwandishi wetu

Wanasarakasi wawili watanzania ambao ni ndugu, Fadhil Ramadhani na Ibrahim Job, wameshinda kitita cha fedha cha dola za Kimarekani 250,000 sawa na sh 634 milioni baada ya kuibuka washindi wa American Got Talent (AGT) Fantasy League.

Watanzania hao wanaounda kikundi cha sarakasi kinachoitwa Ramadhani  Brothers, waliibuka washindi usiku wa jana Februari 19,2024 kwa kuwashinda wapinzani wao wengine tisa waliofika nao fainali.

Kupitia ukurasa wao wa Instagram baada ya kutangazwa washindi katika usiku huo, wamesema ni ushindi wa kushangaza kwao na kuwashukuru wote waliowapa sapoti.

Wamesema wanajivunia  kutangazwa wabingwa wa dunia wa mashindano, huku wakiwapokeza washindani wenzao  ambao wamewafanya wawe bora zaidi.

Katika hatua nyingine Rais Dk. Samia Suluhu Hassan amewapongeza washindi hao kutokana na kuitangaza vema Tanzania.

“Pongezi kwa vijana wetu Fadhil na Ibrahim (The Ramadhan Brothers) kwa kuibuka washindi katika mashindano ya sanaa na burudani ya AGT: Fantasy League, safari yenu inaendelea kudhihirisha kuwa juhudi, nidhamu, kujituma na kujiamini ni nguzo muhimu kufikia mafanikio. Mnaitangaza vyema nchi yetu na kuweka mfano bora kwa wengine,” amesema Rais Samia.

spot_img

Latest articles

Mkurugenzi Mkuu NIRC atoa pole kwa waandishi wa habari waliopata ajali Iringa

Na Mwandishi Wetu MKURUGENZI Mkuu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji (NIRC), Raymond Mndolwa,...

Baraza la wafanyakazi Siri ya utendaji bora

Na Mwandishi Wetu BARAZA la Wafanyakazi la Sita la TMDA limefanyika kwa ufanisi tarehe...

Baraza la sita la wafanyakazi lachagiza mafanikio ya TMDA

Na Mwandishi Wetu MKURUGENZI Mkuu wa TMDA, Dkt. Adam Fimbo, ametoa pongezi kwa wajumbe...

TMA yatoa mwelekeo wa mvua za Masika Machi hadi Mei 2026

Na Tatu Mohamed  MAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa mwelekeo wa mvua za...

More like this

Mkurugenzi Mkuu NIRC atoa pole kwa waandishi wa habari waliopata ajali Iringa

Na Mwandishi Wetu MKURUGENZI Mkuu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji (NIRC), Raymond Mndolwa,...

Baraza la wafanyakazi Siri ya utendaji bora

Na Mwandishi Wetu BARAZA la Wafanyakazi la Sita la TMDA limefanyika kwa ufanisi tarehe...

Baraza la sita la wafanyakazi lachagiza mafanikio ya TMDA

Na Mwandishi Wetu MKURUGENZI Mkuu wa TMDA, Dkt. Adam Fimbo, ametoa pongezi kwa wajumbe...