Watalii waongezeka Kilwa

Na Mwandishi wetu, Kilwa

Idadi ya watalii kutoka Mataifa mbalimbali duniani imezidi kuongezeka katika Hifadhi ya Urithi wa Dunia ya Magofu ya Kilwa Kisiwani na Songo Mnara kutokana na utalii wa kihistoria na kiutamaduni.

Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA ),taasisi yenye dhamana ya usimamizi wa hifadhi hiyo, Februari 15,2024 ilipokea kundi la tani la watalii 119 kutoka ikiwa ni mfululizo wa safari za watalii wa nje kutembelea hifadhi hiyo kwa shughuli za utalii.

Watalii waliowasili ni kutoka katika nchi za Uingereza, Ufaransa, Ujerumani, Italia, Ubelgiji, Hispania na Canada wakisafirishwa na meli iitwayo Le Bougainville.

Kwa mujibu wa TAWA, hayo ni matokeo ya hatua za makusudi zilizofanywa na Serikali ya Tanzania inayoongozwa na Dk.Samia Suluhu Hassan katika kuhakikisha sekta ya utalii nchini inakua kwa kasi baada ya kucheza filamu maarufu iitwayo Tanzania The Royal Tour.

Pia jitihada za dhati zilizofanywa na Wizara ya Maliasili na Utalii kupitia mamlaka hiyo kwa kuboresha miundombinu wezeshi ya utalii katika hifadhi hiyo.

spot_img

Latest articles

Yanga bingwa Mapinduzi Cup 2026

Na Mwandishi Wetu YANGA imetwaa ubingwa wa kombe la Mapinduzi ikiifunga Azam FC kwa mikwaju...

Yacouba atambulishwa Mbeya City

Na Mwandishi Wetu NYOTA wa zamani wa Yanga, raia wa Burkina Faso, Yacouba Songne, ametambulishwa ...

Waziri Ndejembi: Tanzania ina fursa kubwa ya kuendeleza nishati ya Jotoardhi

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi, amesema kutokana na uwepo wa vyanzo...

‘Guardians of the Peak’ kuinua utangazaji utalii wa Kilimanjaro kupitia filamu

Na Mwandishi Wetu MRADI wa Guardians of the Peak, unaoingia msimu wake wa pili,...

More like this

Yanga bingwa Mapinduzi Cup 2026

Na Mwandishi Wetu YANGA imetwaa ubingwa wa kombe la Mapinduzi ikiifunga Azam FC kwa mikwaju...

Yacouba atambulishwa Mbeya City

Na Mwandishi Wetu NYOTA wa zamani wa Yanga, raia wa Burkina Faso, Yacouba Songne, ametambulishwa ...

Waziri Ndejembi: Tanzania ina fursa kubwa ya kuendeleza nishati ya Jotoardhi

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi, amesema kutokana na uwepo wa vyanzo...