Wageni 300 kuwasili nchini kushiriki mkutano wa CISM

Ramadhan Hassan, Dodoma

Zaidi ya wageni 300 kutoka mataifa mbalimbali wanatarajiwa kuwasili nchini kushiriki mkutano Mkuu wa Baraza la Michezo ya Majeshi Duniani (CISM) utakaoanza Mei 12-19,2024 jijini Dar es Salaam.

Mkutano huo unakuwa wa pili kufanyika Tanzania ambapo mara ya mwisho ilikuwa 1991 jijini Arusha.

Akizungumza na Waandishi wa Habari leo Februari 20,2024 jijini hapa, Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya mkutano huo Meja Jenerali Francis Mbindi, amesema lengo la baraza hilo ni kutumia shughuli za michezo na utimamu wa mwili kama njia ya kueneza amani duniani.

“Ikiwa ni kuhamasisha mshikamano, urafiki, heshima, usawa, uadilifu na ushupavu,”amesema.

Amesema baraza hilo ni shirikisho la kimataifa lililoundwa Februari 18, 1945 baada ya vita kuu ya pili ya dunia na hadi sasa lina nchi wanachama 140 kutoka mabara yote duniani na Tanzania ilijiunga mwaka 1973.

“Tanzania tumepata dhamana ya kuwa wenyeji wa kuandaa mkutano huu wa 79 ambao utafanyika Dar es Salaam kuanzia May 12 hadi Mei 19, 2024,”amesema

Amesema mgeni rasmi siku ya ufunguzi Mei 13, 202 anatarajiwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Dk. Samia Suluhu Hassan.

Amesema siku ya kufunga Mei 17, 2024 mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.

“Sababu zilizopelekea kuteuliwa kwa Tanzania kuwa mwenyeji wa mkutano huu ni uwepo wa amani, ulinzi na usalama,”amesema Mwenyekiti huyo.

Aidha amesema kiswahili ikiwa ni lugha ya Taifa itakuwa miongoni mwa lugha tano zitakazotumika kwenye mkutano huo ambapo zingine ni Kiingereza, Kihispania, Kifaransa na Kiarabu.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Michezo JWTZ, Kanali Martin Msumari amesema watakuwa na michezo ya kipaumbele ambayo ni pamoja na riadha,ngumi na michezo mbalimbali.

spot_img

Latest articles

Yacouba atambulishwa Mbeya City

Na Mwandishi Wetu NYOTA wa zamani wa Yanga, raia wa Burkina Faso, Yacouba Songne, ametambulishwa ...

Waziri Ndejembi: Tanzania ina fursa kubwa ya kuendeleza nishati ya Jotoardhi

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi, amesema kutokana na uwepo wa vyanzo...

‘Guardians of the Peak’ kuinua utangazaji utalii wa Kilimanjaro kupitia filamu

Na Mwandishi Wetu MRADI wa Guardians of the Peak, unaoingia msimu wake wa pili,...

Serikali yazindua Jukwaa la Vijana, yataja vijana kuwa mhimili Mkuu wa Maendeleo ya Taifa

Na Tatu Mohamed SERIKALI imezindua rasmi jukwaa la kitaifa la vijana lijulikanalo kama ‘Vijana...

More like this

Yacouba atambulishwa Mbeya City

Na Mwandishi Wetu NYOTA wa zamani wa Yanga, raia wa Burkina Faso, Yacouba Songne, ametambulishwa ...

Waziri Ndejembi: Tanzania ina fursa kubwa ya kuendeleza nishati ya Jotoardhi

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi, amesema kutokana na uwepo wa vyanzo...

‘Guardians of the Peak’ kuinua utangazaji utalii wa Kilimanjaro kupitia filamu

Na Mwandishi Wetu MRADI wa Guardians of the Peak, unaoingia msimu wake wa pili,...