Wageni 300 kuwasili nchini kushiriki mkutano wa CISM

Ramadhan Hassan, Dodoma

Zaidi ya wageni 300 kutoka mataifa mbalimbali wanatarajiwa kuwasili nchini kushiriki mkutano Mkuu wa Baraza la Michezo ya Majeshi Duniani (CISM) utakaoanza Mei 12-19,2024 jijini Dar es Salaam.

Mkutano huo unakuwa wa pili kufanyika Tanzania ambapo mara ya mwisho ilikuwa 1991 jijini Arusha.

Akizungumza na Waandishi wa Habari leo Februari 20,2024 jijini hapa, Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya mkutano huo Meja Jenerali Francis Mbindi, amesema lengo la baraza hilo ni kutumia shughuli za michezo na utimamu wa mwili kama njia ya kueneza amani duniani.

“Ikiwa ni kuhamasisha mshikamano, urafiki, heshima, usawa, uadilifu na ushupavu,”amesema.

Amesema baraza hilo ni shirikisho la kimataifa lililoundwa Februari 18, 1945 baada ya vita kuu ya pili ya dunia na hadi sasa lina nchi wanachama 140 kutoka mabara yote duniani na Tanzania ilijiunga mwaka 1973.

“Tanzania tumepata dhamana ya kuwa wenyeji wa kuandaa mkutano huu wa 79 ambao utafanyika Dar es Salaam kuanzia May 12 hadi Mei 19, 2024,”amesema

Amesema mgeni rasmi siku ya ufunguzi Mei 13, 202 anatarajiwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Dk. Samia Suluhu Hassan.

Amesema siku ya kufunga Mei 17, 2024 mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.

“Sababu zilizopelekea kuteuliwa kwa Tanzania kuwa mwenyeji wa mkutano huu ni uwepo wa amani, ulinzi na usalama,”amesema Mwenyekiti huyo.

Aidha amesema kiswahili ikiwa ni lugha ya Taifa itakuwa miongoni mwa lugha tano zitakazotumika kwenye mkutano huo ambapo zingine ni Kiingereza, Kihispania, Kifaransa na Kiarabu.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Michezo JWTZ, Kanali Martin Msumari amesema watakuwa na michezo ya kipaumbele ambayo ni pamoja na riadha,ngumi na michezo mbalimbali.

spot_img

Latest articles

Mahakama yaipa uhuru Chadema, sasa ruksa kufanya siasa

Na Mwandishi Wetu MAHAKAMA ya Rufani Tanzania leo 15 Aprili 2026, imekiondolea kifungo cha kutofanya...

Rais Mwinyi akagua Mji wa AFCON Fumba

Na Mwandishi WetuRAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali...

Sowah apigwa faini nzito  kwa utovu wa nidhamu, ashushwa U-20

Na Winfrida Mtoi UONGOZI wa Klabu ya Simba umeweka wazi hatua kali za kinidhamu zilizochukuliwa...

Waziri Mavunde aelekeza kusimamishwa kwa shughuli za uchimbaji Busulwangili-Kahama – Kahama

Na Mwandishi wetu, Dodoma WAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde, ameagiza kusimamishwa mara moja kwa...

More like this

Mahakama yaipa uhuru Chadema, sasa ruksa kufanya siasa

Na Mwandishi Wetu MAHAKAMA ya Rufani Tanzania leo 15 Aprili 2026, imekiondolea kifungo cha kutofanya...

Rais Mwinyi akagua Mji wa AFCON Fumba

Na Mwandishi WetuRAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali...

Sowah apigwa faini nzito  kwa utovu wa nidhamu, ashushwa U-20

Na Winfrida Mtoi UONGOZI wa Klabu ya Simba umeweka wazi hatua kali za kinidhamu zilizochukuliwa...