TPLB yavuna mamilioni Yanga, Simba

Na Winfrida Mtoi

Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi ya Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB), imevuna mamilioni kutoka katika klabu za Yanga, Simba na nyingine za ligi hiyo kutokana na makosa mbalimbali waliyofanya kwenye michezo yao iliyopita.

Kwa mujibu wa taarifa ya kikao cha kamati hiyo cha Februari 14,2024 cha kupitia mwenendo na matukio ya michezo ya Ligi, klabu ya Yanga imetozwa faini ya sh 1,000,000 kwa kosa la mashabiki wake watatu kuonekana kwenye vyumba vya kuvalia wakati wa mechi yao na Tanzania Prisons.

Klabu hiyo imetozwa faini nyingine ya sh 1,000,000 pamoja na Dodoma Jiji kutokana wachezaji wao kuchelewa kurejea uwanjani kipindi cha pili wakati timu hizo zilipokutana na kusababisha mchezo kuchelewa kwa dakika saba.

Mshambuliaji wa timu hiyo Clement Mzize ametozwa faini ya sh 1,000,000 kwa kosa la kuondoa taulo la kipa wa Dodoma Jiji lililokuwa golini hali iliyoashiria imani za kishirikina, huku Shomari Kibwana naye alipigwa faini kama hiyo kwa kosa linalofanana na hilo wakati wa mechi dhidi ya Mashujaa FC.

Kwa upande wa Simba imepigwa faini ya 1,000,000 kwa kosa la mashabiki wake kuonekana katika video za mitandaoni wakimwaga vitu nyenye asili ya unga kitendo kilichoashiria ushirikina siku moja kabla ya mchezo wao na Tabora United kwenye Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi.

Klabu hiyo imepigwa faini nyingine kama hiyo kwa kosa la mashabiki wake kurusha chupa za maji wakati wa mechi yao na Azam FC.

Klabu nyingine zilizotozwa na faini kama hiyo ni Mashujaa FC, Tanzania Prisons.

spot_img

Latest articles

TTCL yaahidi kuimarisha huduma za kidijitali nchini

Na Tatu Mohamed SHIRIKA la Mawasiliano Tanzania (TTCL) limesema litaendelea kuimarisha huduma za mawasiliano nchini...

TANZANIA NA URUSI ZAIMARISHA USHIRIKIANO WA UTALII KUPITIA MAKUBALIANO MAPYA

Na Mwandishi Wetu TANZANIA na Urusi zimesaini Hati ya Makubaliano (MoU) ya ushirikiano katika...

GASCO yaahidi kuendelea kuimarisha usalama na upatikanaji wa huduma ya gesi asilia

Na Tatu Mohamed KAMPUNI ya GASCO, kampuni tanzu ya Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania...

Mhitimu wa VETA abuni mashine za kuongeza thamani ya mazao, ajiajiri kupitia kampuni yake

Na Mwandishi Wetu MHITIMU wa mafunzo ya ufundi stadi kupitia VETA, Ernest Maranya, amebuni...

More like this

TTCL yaahidi kuimarisha huduma za kidijitali nchini

Na Tatu Mohamed SHIRIKA la Mawasiliano Tanzania (TTCL) limesema litaendelea kuimarisha huduma za mawasiliano nchini...

TANZANIA NA URUSI ZAIMARISHA USHIRIKIANO WA UTALII KUPITIA MAKUBALIANO MAPYA

Na Mwandishi Wetu TANZANIA na Urusi zimesaini Hati ya Makubaliano (MoU) ya ushirikiano katika...

GASCO yaahidi kuendelea kuimarisha usalama na upatikanaji wa huduma ya gesi asilia

Na Tatu Mohamed KAMPUNI ya GASCO, kampuni tanzu ya Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania...