TPLB yavuna mamilioni Yanga, Simba

Na Winfrida Mtoi

Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi ya Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB), imevuna mamilioni kutoka katika klabu za Yanga, Simba na nyingine za ligi hiyo kutokana na makosa mbalimbali waliyofanya kwenye michezo yao iliyopita.

Kwa mujibu wa taarifa ya kikao cha kamati hiyo cha Februari 14,2024 cha kupitia mwenendo na matukio ya michezo ya Ligi, klabu ya Yanga imetozwa faini ya sh 1,000,000 kwa kosa la mashabiki wake watatu kuonekana kwenye vyumba vya kuvalia wakati wa mechi yao na Tanzania Prisons.

Klabu hiyo imetozwa faini nyingine ya sh 1,000,000 pamoja na Dodoma Jiji kutokana wachezaji wao kuchelewa kurejea uwanjani kipindi cha pili wakati timu hizo zilipokutana na kusababisha mchezo kuchelewa kwa dakika saba.

Mshambuliaji wa timu hiyo Clement Mzize ametozwa faini ya sh 1,000,000 kwa kosa la kuondoa taulo la kipa wa Dodoma Jiji lililokuwa golini hali iliyoashiria imani za kishirikina, huku Shomari Kibwana naye alipigwa faini kama hiyo kwa kosa linalofanana na hilo wakati wa mechi dhidi ya Mashujaa FC.

Kwa upande wa Simba imepigwa faini ya 1,000,000 kwa kosa la mashabiki wake kuonekana katika video za mitandaoni wakimwaga vitu nyenye asili ya unga kitendo kilichoashiria ushirikina siku moja kabla ya mchezo wao na Tabora United kwenye Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi.

Klabu hiyo imepigwa faini nyingine kama hiyo kwa kosa la mashabiki wake kurusha chupa za maji wakati wa mechi yao na Azam FC.

Klabu nyingine zilizotozwa na faini kama hiyo ni Mashujaa FC, Tanzania Prisons.

spot_img

Latest articles

Mwakinyo kuilipia kisasi Taifa Stars dhidi ya Mnigeria kesho, Furahi apania rekodi

Na Winfrida Mtoi BONDIA wa kimataifa wa Tanzania, Hassan Mwakinyo, ameweka bayana kuwa pambano lake...

Serikali kuendelea kuwawezesha vijana kijamii, kiuchumi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Joel...

Kids Holiday Festival yawavuta mamia ya watoto, CRDB yatumia jukwaa kujenga uelewa wa fedha

Na Mwandishi Wetu BURUDANI na michezo mbalimbali vilitawala Tamasha la Kids Holiday Festival lililowakusanya...

Mambo: Demokrasia haijengwi kwa mashinikizo, vitisho

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Mgombea wa Bavicha Taifa, Masoud Mambo amesema kuwa demokrasia ya...

More like this

Mwakinyo kuilipia kisasi Taifa Stars dhidi ya Mnigeria kesho, Furahi apania rekodi

Na Winfrida Mtoi BONDIA wa kimataifa wa Tanzania, Hassan Mwakinyo, ameweka bayana kuwa pambano lake...

Serikali kuendelea kuwawezesha vijana kijamii, kiuchumi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Joel...

Kids Holiday Festival yawavuta mamia ya watoto, CRDB yatumia jukwaa kujenga uelewa wa fedha

Na Mwandishi Wetu BURUDANI na michezo mbalimbali vilitawala Tamasha la Kids Holiday Festival lililowakusanya...