TPLB yavuna mamilioni Yanga, Simba

Na Winfrida Mtoi

Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi ya Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB), imevuna mamilioni kutoka katika klabu za Yanga, Simba na nyingine za ligi hiyo kutokana na makosa mbalimbali waliyofanya kwenye michezo yao iliyopita.

Kwa mujibu wa taarifa ya kikao cha kamati hiyo cha Februari 14,2024 cha kupitia mwenendo na matukio ya michezo ya Ligi, klabu ya Yanga imetozwa faini ya sh 1,000,000 kwa kosa la mashabiki wake watatu kuonekana kwenye vyumba vya kuvalia wakati wa mechi yao na Tanzania Prisons.

Klabu hiyo imetozwa faini nyingine ya sh 1,000,000 pamoja na Dodoma Jiji kutokana wachezaji wao kuchelewa kurejea uwanjani kipindi cha pili wakati timu hizo zilipokutana na kusababisha mchezo kuchelewa kwa dakika saba.

Mshambuliaji wa timu hiyo Clement Mzize ametozwa faini ya sh 1,000,000 kwa kosa la kuondoa taulo la kipa wa Dodoma Jiji lililokuwa golini hali iliyoashiria imani za kishirikina, huku Shomari Kibwana naye alipigwa faini kama hiyo kwa kosa linalofanana na hilo wakati wa mechi dhidi ya Mashujaa FC.

Kwa upande wa Simba imepigwa faini ya 1,000,000 kwa kosa la mashabiki wake kuonekana katika video za mitandaoni wakimwaga vitu nyenye asili ya unga kitendo kilichoashiria ushirikina siku moja kabla ya mchezo wao na Tabora United kwenye Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi.

Klabu hiyo imepigwa faini nyingine kama hiyo kwa kosa la mashabiki wake kurusha chupa za maji wakati wa mechi yao na Azam FC.

Klabu nyingine zilizotozwa na faini kama hiyo ni Mashujaa FC, Tanzania Prisons.

spot_img

Latest articles

Waziri wa Nishati Ndejembi azindua rasmi mita janja

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amezindua rasmi mita janja (smart meter)...

RC Kunenge: Mto Ruvu ubaki kwa matumizi ya binadamu tu, tusitishe shughuli nyingine kwa muda

Na Mwandishi Wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, ametoa wito kwa wakulima...

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...

Rais Samia: Walilenga kupindua dola

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa vurugu...

More like this

Waziri wa Nishati Ndejembi azindua rasmi mita janja

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amezindua rasmi mita janja (smart meter)...

RC Kunenge: Mto Ruvu ubaki kwa matumizi ya binadamu tu, tusitishe shughuli nyingine kwa muda

Na Mwandishi Wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, ametoa wito kwa wakulima...

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...