Saba wapofuka wakitibu macho (red eyes) kienyeji

UNGUJA.
Watu saba wamepofuka macho Visiwani Zanzibar, kutokana na kutumia dawa za kienyeji kutibu ugonjwa wa macho mekundu (red eyes). Zaidi ya watu 12,860 wameugua ugonjwa huo, wengine wakiwa wamepona na baadhi wanaendelea na matibabu. Mratibu wa huduma za afya msingi ya matibabu ya macho, Dk Rajab Muhammed Hilali amesema dawa za kienyeji zimewasababishia upofu watu hao na kwamba miongoni mwa wagonjwa waliopata upofu yupo mtoto wa miaka 11.

Dk. Hilal amesma jicho la kulia la mtoto huyo limeathirika na kwamba walimpeleka Hospitali ya CCBRT lakini ilionekana haliwezi kurejea katika hali ya kawaida. Dk. Hilali amesema watu wengi wanaoenda hospitalini wanakuwa wameshazidiwa baada ya kutumia dawa ambazo si sahihi kwa ajili ya tiba. “Kwa wagonjwa hao wana jicho ambalo limepata upofu, ukiuliza unaambiwa alikuwa anatumia dawa za kienyeji, chumvi na vitu vingine kwa hiyo vimeleta athari kwenye jicho,” amesema.

Meneja wa kitengo cha elimu ya afya cha Wizara ya Afya (Zanzibar), Dk Bakar Hamad Madarawa amesema kuna wagonjwa wengi waliougua ugonjwa wa macho lakini hawajaenda kupata matibabu. Amesema takwimu za wagonjwa hao ni takribani asilimia 20, lakini kwa mazingira ya kawaida asilimia 80 ya wagonjwa hao bado hawajafika katika vituo vya afya.

“Takwimu hizi ni asilimia 20 ambazo tunazo sisi Serikali, lakini asilimia 80 wapo wagonjwa wengi, kila familia kwa sasa kuna angalu mgonjwa mmoja, kwa hiyo tuendelee kutoa elimu,” amesema Dk. Madarawa.

Mwishoni wa Januari, 2024 wataalamu wa afya na madaktari bingwa wa macho walinukuliwa na Mwananchi Digital wakisema wamekuwa wanapokea idadi kubwa ya wagonjwa wakiwa katika hali ya ugonjwa mkali, kutokana na matumizi ya njia mbadala kutibu macho, ikiwamo matumizi ya mkojo, chumvi na vitunguu saumu.

Wataalamu walisema wagonjwa wanaotumia vitu tajwa macho yao huvimba na kuuma zaidi pamoja na kupatwa homa, huku hasi zinazotajwa zaidi ni kusababisha vidonda kwenye kioo cha jicho. Tiba hizo mbadala zinaelezwa kuwa zinaweza kusababisha kovu kwenye jicho litakalomfanya mgonjwa apate uoni hafifu au kupoteze uwezo wa kuona kabisa.

Ugonjwa huo ujulikanao viral keratoconjunctivitis (red eyes), mbali ya Zanzibar, pia umesambaa maeneo mbalimbali ya Tanzania Bara.

Chanzo: Mwananchi

spot_img

Latest articles

Mukwala atua Zanzibar, Simba ikiivaa Azam kesho Mapinduzi Cup

Na Winfrida Mtoi WAKATI Simba kitarajia kukabiliana na Azam FC kesho katika mchezo wa nusu...

Serikali yawekeza zaidi ya Sh. Bilioni 280 kuimarisha upatikanaji umeme Dar es Salaam

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amesema Serikali ya Jamhuri ya Muungano...

Chongolo akutana na wawekezaji  kutoka China

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Kilimo, Daniel Chongolo, amekutana na wawekezaji kutoka nchini China  na...

Familia yaondoa vitu nyumbani kwa Polepole

Na Mwandishi Wetu FAMILIA ya aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Cuba, Humphrey Polepole, leo Jumanne,...

More like this

Mukwala atua Zanzibar, Simba ikiivaa Azam kesho Mapinduzi Cup

Na Winfrida Mtoi WAKATI Simba kitarajia kukabiliana na Azam FC kesho katika mchezo wa nusu...

Serikali yawekeza zaidi ya Sh. Bilioni 280 kuimarisha upatikanaji umeme Dar es Salaam

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amesema Serikali ya Jamhuri ya Muungano...

Chongolo akutana na wawekezaji  kutoka China

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Kilimo, Daniel Chongolo, amekutana na wawekezaji kutoka nchini China  na...