Mashujaa wazitaka pointi tatu kwa Yanga

Na Winfrida Mtoi

Kueleke mchezo wao na Yanga, Kocha Mkuu wa Mashujaa FC, Mohammed Bares amesema wamejipanga kupata pointi tatu licha ya kwamba wanafahamu ugumu wa mechi hiyo.

Mchezo huo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, utarajia kupigwa kesho Februari 8, 2024 kwenye Uwanja wa Azam Complex, Dar es Salaam.

Katika mchezo uliopita timu hiyo ilifungwa na Simba bao 1-0 kwenye uwanja wao wa nyumbani Lake Tanganyika, Kigoma.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Februari 7,2024 jijini Dar es Salaam, Bares amesema wametoka kucheza mechi ngumu dhidi ya Simba wanaingia tena kwenye mechi ngumu lakini wamejipanga kuidhibiti Yanga.

“Ni mchezo mkubwa lakini kwenye mpira si mchezo mkubwa ni kujipanga tu na sisi tumejipanga kuidhibiti Yanga kwa sababu tunajua ina wachezaji wanaoweza kuamua matokeo,” amesema Bares.

Kwa upande wake mchezaji wa timu hiyo, Baraka Mtuwi amesema kwa kipindi hiki kila mchezo kwao wanacheza kama fainali na kuahidi kuwa hawatawaangusha mashabiki wao.

Mashujaa iliyoanza msimu huu kwa kasi hadi kukaa kwenye nafasi nne za juu mwanzoni mwa ligi hiyo, kwa sasa inashika nafasi ya 15 na alama tisa ikicheza michezo 13.

spot_img

Latest articles

Serikali yazindua shindano la ‘Vijana Uchumi Challenge’ kuibua ubunifu wa vijana

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi ofisi ya Rais Maendeleo ya Vijana, Joel Nanauka,...

Vita ya kusaka tiketi ya China 2026 yanoga, Waogeleaji 200 wachuana vikali

Na Winfrida Mtoi IKIWA ni siku ya pili ya Mashindano ya Taifa ya mchezo wa...

Tanzania yang’ara Tuzo za Utalii Duniani, yaingiza vipengele 41

Na Tatu Mohamed TANZANIA imeendelea kung’ara katika anga la kimataifa baada ya kuingiza vipengele...

Okello awapa jeuri mashabiki wa Yanga

Na Mwandishi Wetu Nyota wa Yanga, Allan Okello amewahakikishia mashabiki wa timu hiyo kuwa watamaliza...

More like this

Serikali yazindua shindano la ‘Vijana Uchumi Challenge’ kuibua ubunifu wa vijana

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi ofisi ya Rais Maendeleo ya Vijana, Joel Nanauka,...

Vita ya kusaka tiketi ya China 2026 yanoga, Waogeleaji 200 wachuana vikali

Na Winfrida Mtoi IKIWA ni siku ya pili ya Mashindano ya Taifa ya mchezo wa...

Tanzania yang’ara Tuzo za Utalii Duniani, yaingiza vipengele 41

Na Tatu Mohamed TANZANIA imeendelea kung’ara katika anga la kimataifa baada ya kuingiza vipengele...