Mashujaa wazitaka pointi tatu kwa Yanga

Na Winfrida Mtoi

Kueleke mchezo wao na Yanga, Kocha Mkuu wa Mashujaa FC, Mohammed Bares amesema wamejipanga kupata pointi tatu licha ya kwamba wanafahamu ugumu wa mechi hiyo.

Mchezo huo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, utarajia kupigwa kesho Februari 8, 2024 kwenye Uwanja wa Azam Complex, Dar es Salaam.

Katika mchezo uliopita timu hiyo ilifungwa na Simba bao 1-0 kwenye uwanja wao wa nyumbani Lake Tanganyika, Kigoma.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Februari 7,2024 jijini Dar es Salaam, Bares amesema wametoka kucheza mechi ngumu dhidi ya Simba wanaingia tena kwenye mechi ngumu lakini wamejipanga kuidhibiti Yanga.

“Ni mchezo mkubwa lakini kwenye mpira si mchezo mkubwa ni kujipanga tu na sisi tumejipanga kuidhibiti Yanga kwa sababu tunajua ina wachezaji wanaoweza kuamua matokeo,” amesema Bares.

Kwa upande wake mchezaji wa timu hiyo, Baraka Mtuwi amesema kwa kipindi hiki kila mchezo kwao wanacheza kama fainali na kuahidi kuwa hawatawaangusha mashabiki wao.

Mashujaa iliyoanza msimu huu kwa kasi hadi kukaa kwenye nafasi nne za juu mwanzoni mwa ligi hiyo, kwa sasa inashika nafasi ya 15 na alama tisa ikicheza michezo 13.

spot_img

Latest articles

Mhitimu wa VETA abuni mashine za kuongeza thamani ya mazao, ajiajiri kupitia kampuni yake

Na Mwandishi Wetu MHITIMU wa mafunzo ya ufundi stadi kupitia VETA, Ernest Maranya, amebuni...

MHE.SALOME: WANANCHI WANAOPITIWA NA MIUNDOMBINU YA UMEME WAUNGANISHIWE HUDUMA KWA SH. 27,000

Na Mwandishi Wetu, Mara Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, amesema Serikali ya Awamu...

TTCL Yakabidhi Magari 6 ya Sh. Milioni 903 Kuimarisha Ufanisi wa Huduma

Na Mwandishi Wetu SHIRIKA la Mawasiliano Tanzania (TTCL) limeendelea kutekeleza mkakati wake wa kuboresha...

Ofisi ya Usuluhishi wa Kodi Yaahidi Kuimarisha Mazingira ya Biashara na Uwekezaji

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Usuluhishi wa Malalamiko na Taarifa za Kodi imesema, inaendelea...

More like this

Mhitimu wa VETA abuni mashine za kuongeza thamani ya mazao, ajiajiri kupitia kampuni yake

Na Mwandishi Wetu MHITIMU wa mafunzo ya ufundi stadi kupitia VETA, Ernest Maranya, amebuni...

MHE.SALOME: WANANCHI WANAOPITIWA NA MIUNDOMBINU YA UMEME WAUNGANISHIWE HUDUMA KWA SH. 27,000

Na Mwandishi Wetu, Mara Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, amesema Serikali ya Awamu...

TTCL Yakabidhi Magari 6 ya Sh. Milioni 903 Kuimarisha Ufanisi wa Huduma

Na Mwandishi Wetu SHIRIKA la Mawasiliano Tanzania (TTCL) limeendelea kutekeleza mkakati wake wa kuboresha...