Mashujaa wazitaka pointi tatu kwa Yanga

Na Winfrida Mtoi

Kueleke mchezo wao na Yanga, Kocha Mkuu wa Mashujaa FC, Mohammed Bares amesema wamejipanga kupata pointi tatu licha ya kwamba wanafahamu ugumu wa mechi hiyo.

Mchezo huo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, utarajia kupigwa kesho Februari 8, 2024 kwenye Uwanja wa Azam Complex, Dar es Salaam.

Katika mchezo uliopita timu hiyo ilifungwa na Simba bao 1-0 kwenye uwanja wao wa nyumbani Lake Tanganyika, Kigoma.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Februari 7,2024 jijini Dar es Salaam, Bares amesema wametoka kucheza mechi ngumu dhidi ya Simba wanaingia tena kwenye mechi ngumu lakini wamejipanga kuidhibiti Yanga.

“Ni mchezo mkubwa lakini kwenye mpira si mchezo mkubwa ni kujipanga tu na sisi tumejipanga kuidhibiti Yanga kwa sababu tunajua ina wachezaji wanaoweza kuamua matokeo,” amesema Bares.

Kwa upande wake mchezaji wa timu hiyo, Baraka Mtuwi amesema kwa kipindi hiki kila mchezo kwao wanacheza kama fainali na kuahidi kuwa hawatawaangusha mashabiki wao.

Mashujaa iliyoanza msimu huu kwa kasi hadi kukaa kwenye nafasi nne za juu mwanzoni mwa ligi hiyo, kwa sasa inashika nafasi ya 15 na alama tisa ikicheza michezo 13.

spot_img

Latest articles

Tanesco yaendelea kuwaelimisha wanaofanya shughuli za kiuchumi kwenye miundombinu ya umeme

📌Ni katika muendelezo wa ukaguzi wa miundombinu ya umeme Dar es salaam 📌Yatoa rai kwa...

‎DAWASA yapeleka agenda ya kudhibiti upotevu wa maji Pwani

Na Mwandishi Wetu MAPAMBANO dhidi ya upotevu wa maji yamepokelewa vyema na uongozi wa...

Msaidizi wa Lissu apatikana na pingu mkononi, aeleza kilichomkuta

Na Mwandishi Wetu NAIBU Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Bara, Amani...

Tanzania yataka ushirikiano imara na kuvuka mipaka kutokomeza maralia 

Na John Mapepele, Geneva, Uswisi  WAZIRI wa Afya wa Tanzania, Mohamed Mchengerwa, ametoa wito wa...

More like this

Tanesco yaendelea kuwaelimisha wanaofanya shughuli za kiuchumi kwenye miundombinu ya umeme

📌Ni katika muendelezo wa ukaguzi wa miundombinu ya umeme Dar es salaam 📌Yatoa rai kwa...

‎DAWASA yapeleka agenda ya kudhibiti upotevu wa maji Pwani

Na Mwandishi Wetu MAPAMBANO dhidi ya upotevu wa maji yamepokelewa vyema na uongozi wa...

Msaidizi wa Lissu apatikana na pingu mkononi, aeleza kilichomkuta

Na Mwandishi Wetu NAIBU Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Bara, Amani...