Mashujaa wazitaka pointi tatu kwa Yanga

Na Winfrida Mtoi

Kueleke mchezo wao na Yanga, Kocha Mkuu wa Mashujaa FC, Mohammed Bares amesema wamejipanga kupata pointi tatu licha ya kwamba wanafahamu ugumu wa mechi hiyo.

Mchezo huo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, utarajia kupigwa kesho Februari 8, 2024 kwenye Uwanja wa Azam Complex, Dar es Salaam.

Katika mchezo uliopita timu hiyo ilifungwa na Simba bao 1-0 kwenye uwanja wao wa nyumbani Lake Tanganyika, Kigoma.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Februari 7,2024 jijini Dar es Salaam, Bares amesema wametoka kucheza mechi ngumu dhidi ya Simba wanaingia tena kwenye mechi ngumu lakini wamejipanga kuidhibiti Yanga.

“Ni mchezo mkubwa lakini kwenye mpira si mchezo mkubwa ni kujipanga tu na sisi tumejipanga kuidhibiti Yanga kwa sababu tunajua ina wachezaji wanaoweza kuamua matokeo,” amesema Bares.

Kwa upande wake mchezaji wa timu hiyo, Baraka Mtuwi amesema kwa kipindi hiki kila mchezo kwao wanacheza kama fainali na kuahidi kuwa hawatawaangusha mashabiki wao.

Mashujaa iliyoanza msimu huu kwa kasi hadi kukaa kwenye nafasi nne za juu mwanzoni mwa ligi hiyo, kwa sasa inashika nafasi ya 15 na alama tisa ikicheza michezo 13.

spot_img

Latest articles

Mavazi ya kitamaduni kivutio kingine AFCON 2025

Na Winfrida Mtoi SHAMRASHAMRA kuelekea Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON-2025), zimezidi kupamba moto, hasa baada...

Livembe: Mchakato wa Uchaguzi ulikuwa wa haki na halali

Na Mwandishi Wetu MWENYEKITI wa Jumuiya ya Wafanyabiashara Tanzania (JWT), Hamis Livembe, amesema mchakato wa...

Sekta ya Viwanda na Biashara yazidi kutoa fursa kwa vijana

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Viwanda na Biashara, Judith Kapinga amesema sekta ya viwanda...

Polisi yachunguza tukio la kuchoma moto magari msibani

Na Mwandishi Wetu JESHI la Polisi Mkoa wa Morogoro limesema linachunguza tukio la kuchoma moto na...

More like this

Mavazi ya kitamaduni kivutio kingine AFCON 2025

Na Winfrida Mtoi SHAMRASHAMRA kuelekea Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON-2025), zimezidi kupamba moto, hasa baada...

Livembe: Mchakato wa Uchaguzi ulikuwa wa haki na halali

Na Mwandishi Wetu MWENYEKITI wa Jumuiya ya Wafanyabiashara Tanzania (JWT), Hamis Livembe, amesema mchakato wa...

Sekta ya Viwanda na Biashara yazidi kutoa fursa kwa vijana

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Viwanda na Biashara, Judith Kapinga amesema sekta ya viwanda...