Wazabuni watatu kuchuana mradi wa mwendokasi Kibaha -Morogoro

Na Esther Mnyika, Media Brains

Serikali imepokea zabuni tatu za utekelezaji wa mradi wa barabara za mwendokasi kuanzia Kibaha hadi Morogoro ambapo awamu ya kwanza utaanzia Kibaha hadi Chalinze yenye urefu wa kilomita 78.9.

Akizungumza leo Februari 6,2024 jijini Dar es Salaam Mkurugenzi Mtendaji wa kituo cha Ubia Nchini (PPP), David Kafulila wakati akifungua tenda za wazabuni hao amesema jumla ya makampuni tisa yaliwasilisha nyaraka zao lakini anahitajika mmoja.

Amesema Serikali inajenga barabara ya Kibaha , Mlandizi, Chalinze na Morogoro ya kilomita 205 kwa ubia kati ya sekta ya umma na binafsi ambapo PPP imegawa barabara hiyo katika sehemu mbili.

“Sehemu hizi mbili, sehemu ya kwanza ni Kibaha , Mlandizi, na Chalinze kilomita 78.9 na sehemu ya pili Chalinze hadi Morogoro kilomita 126.1 na tayari upembuzi yakinifu sehemu ya kwanza ulifanywa na Kampuni ya kishauri ya Cheli Engineering Co.Ltd kutoka Korea.

” Kazi ya upembuzi yakinifu ilikamilika Februari mwaka jana na kazi ya upembuzi yakinifu kwa ajili ya kipande cha pili inaendelea, ” amesema Kafulila.

Amesema ujenzi huo utasaidia kupunguza muda wa kusafiri kutoka Dar es Salaam kwenda Morogoro, hivyo kukuza uchumi kutokana na watu kufika haraka wanapokwenda.

Amesema pia mradi huo utawezesha upatikanaji wa ujuzi, kiufundi, kifedha, kiteknolojia na kimenejimenti kutoka sekta binafsi.

Kwa upande wake Meneja wa Miradi ya Ubia Kati ya Serikali na Sekta Binafsi TANROAD, Mhandisi Kitainda Michael amesema serikali ilikaribisha wawekezaji waliokuwa na nia ya kujenga na kuendeleza sehemu ya Kibaha hadi Chalinze kilomita 78.9 kwa uratibu wa PPP.

“Kwa ajili ya kuwachambua na kuweza kuwatumia nyaraka za zabuni wale watakaokuwa wamekidhi vigezo ili waweze kuandaa zabuni zao na kuziwasilisha TANROAD kwa kufanya usanifu wa kina, kujenga, kugharamia ujenzi, kuendesha, kukarabati pamoja na kurejesha kwa Serikali,” amesema Mhandisi Michael.

Amesema muda wa ujenzi unakadiriwa kwa muda wa miaka mitatu na mwekezaji kuendesha mradi ni miaka 30 ambapo baada mda huo mradi utarudishwa kwa serikali.

spot_img

Latest articles

Serikali yazindua Jukwaa la Vijana, yataja vijana kuwa mhimili Mkuu wa Maendeleo ya Taifa

Na Tatu Mohamed SERIKALI imezindua rasmi jukwaa la kitaifa la vijana lijulikanalo kama ‘Vijana...

Mradi wa Umeme Jua uko mbioni kukamilika- Salome Makamba

Na Mwandishi Wetu NAIBU Waziri wa Nishati, Salome Makamba, amesema Mradi wa Umeme unaozalishwa...

Tuna deni la kusimamia miradi na kusikiloza kero za wananchi ili kuleta Maendeleo ya kweli: Salome

Na Mwandishi Wetu NAIBU Waziri wa Nishati, Salome Makamba, amesema viongozi wana deni kubwa...

2025 mwaka wa mageuzi na matokeo katika mashirika ya umma

Na Mwandishi Wetu MWAKA 2025 ulikuwa wa mafanikio makubwa kwa Ofisi ya Msajili wa...

More like this

Serikali yazindua Jukwaa la Vijana, yataja vijana kuwa mhimili Mkuu wa Maendeleo ya Taifa

Na Tatu Mohamed SERIKALI imezindua rasmi jukwaa la kitaifa la vijana lijulikanalo kama ‘Vijana...

Mradi wa Umeme Jua uko mbioni kukamilika- Salome Makamba

Na Mwandishi Wetu NAIBU Waziri wa Nishati, Salome Makamba, amesema Mradi wa Umeme unaozalishwa...

Tuna deni la kusimamia miradi na kusikiloza kero za wananchi ili kuleta Maendeleo ya kweli: Salome

Na Mwandishi Wetu NAIBU Waziri wa Nishati, Salome Makamba, amesema viongozi wana deni kubwa...