Nyota Simba waungana kumuombea Inonga abebe kombe AFCON

Na Winfrida Mtoi

Wachezaji wa Simba wameungana na mchezaji mwenzao Henock Inonga kumuombea aweze kufika fainali ya Kombe la Mataifa Afrika (AFCON) hata kubeba ubingwa wa michuano hiyo inayoendelea nchini Ivory Coast.

Inonga ambaye ni beki wa Simba anaitumikia timu ya Taifa ya DR Congo ambayo keshokutwa Februari 7, 2024 itashuka dimbani kucheza na wenyeweji Ivory Coast katika mchezo wa nusu fainali.

Beki wa Wekundu wa Msimbazi hao, Hussein Kazi ndiye aliyeweka bayana kuwa wachezaji wa Simba wanamuombea mwenzao aweze kufika mbali na kuchukua ubingwa michuano hiyo mikubwa barani Afrika.

“Sisi kama Simba wachezaji kwa ujumla, tunamuombea mwenzetu Inonga mazuri aweze kufika mbali na kuchukua kombe,” amesema Kazi wakati akizungumzia maandalizi kuelekea mechi yao na Tabora United, utakaochezwa kesho Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi, mkoni Tabora.

spot_img

Latest articles

Waraka kwa Waziri Paul Christian Makonda

Katika dunia tunayoishi sasa michezo ni sekta inayoshikilia uchumi mkubwa. Wanamichezo wengi wamekuwa mabilionea...

ETDCO yaahidi kukamilisha Mradi wa Umeme katika vitongoji 372 Ruvuma kwa wakati

Na Mwandishi Wetu KAMPUNI ya Ujenzi na Ukarabati wa Miundombinu ya Usafirishaji na Usambazaji...

Wadau sekta ya Hali ya Hewa wajadili utabiri wa Masika 2026

Na Mwandishi Wetu WADAU kutoka sekta mbalimbali nchini wamekutana kujadili utabiri wa msimu wa...

WMA yafunga Mtambo wa kisasa unaohakiki Dira za Maji Dodoma

Na Mwandishi Wetu WAKALA wa Vipimo (WMA) umesimika mtambo wa kisasa wa kidijitali wa...

More like this

Waraka kwa Waziri Paul Christian Makonda

Katika dunia tunayoishi sasa michezo ni sekta inayoshikilia uchumi mkubwa. Wanamichezo wengi wamekuwa mabilionea...

ETDCO yaahidi kukamilisha Mradi wa Umeme katika vitongoji 372 Ruvuma kwa wakati

Na Mwandishi Wetu KAMPUNI ya Ujenzi na Ukarabati wa Miundombinu ya Usafirishaji na Usambazaji...

Wadau sekta ya Hali ya Hewa wajadili utabiri wa Masika 2026

Na Mwandishi Wetu WADAU kutoka sekta mbalimbali nchini wamekutana kujadili utabiri wa msimu wa...