Nyota Simba waungana kumuombea Inonga abebe kombe AFCON

Na Winfrida Mtoi

Wachezaji wa Simba wameungana na mchezaji mwenzao Henock Inonga kumuombea aweze kufika fainali ya Kombe la Mataifa Afrika (AFCON) hata kubeba ubingwa wa michuano hiyo inayoendelea nchini Ivory Coast.

Inonga ambaye ni beki wa Simba anaitumikia timu ya Taifa ya DR Congo ambayo keshokutwa Februari 7, 2024 itashuka dimbani kucheza na wenyeweji Ivory Coast katika mchezo wa nusu fainali.

Beki wa Wekundu wa Msimbazi hao, Hussein Kazi ndiye aliyeweka bayana kuwa wachezaji wa Simba wanamuombea mwenzao aweze kufika mbali na kuchukua ubingwa michuano hiyo mikubwa barani Afrika.

“Sisi kama Simba wachezaji kwa ujumla, tunamuombea mwenzetu Inonga mazuri aweze kufika mbali na kuchukua kombe,” amesema Kazi wakati akizungumzia maandalizi kuelekea mechi yao na Tabora United, utakaochezwa kesho Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi, mkoni Tabora.

spot_img

Latest articles

Tuna deni la kusimamia miradi na kusikiloza kero za wananchi ili kuleta Maendeleo ya kweli: Salome

Na Mwandishi Wetu NAIBU Waziri wa Nishati, Salome Makamba, amesema viongozi wana deni kubwa...

2025 mwaka wa mageuzi na matokeo katika mashirika ya umma

Na Mwandishi Wetu MWAKA 2025 ulikuwa wa mafanikio makubwa kwa Ofisi ya Msajili wa...

Wakatoliki feki wamechafua hali ya hewa, aibu hii anabeba nani?

TAHARUKI kubwa imeibuka nchini. Unaweza kuiona ukichungulia kwenye mitandao ya kijamii. Imesababishwa na akili...

Mukwala atua Zanzibar, Simba ikiivaa Azam kesho Mapinduzi Cup

Na Winfrida Mtoi WAKATI Simba kitarajia kukabiliana na Azam FC kesho katika mchezo wa nusu...

More like this

Tuna deni la kusimamia miradi na kusikiloza kero za wananchi ili kuleta Maendeleo ya kweli: Salome

Na Mwandishi Wetu NAIBU Waziri wa Nishati, Salome Makamba, amesema viongozi wana deni kubwa...

2025 mwaka wa mageuzi na matokeo katika mashirika ya umma

Na Mwandishi Wetu MWAKA 2025 ulikuwa wa mafanikio makubwa kwa Ofisi ya Msajili wa...

Wakatoliki feki wamechafua hali ya hewa, aibu hii anabeba nani?

TAHARUKI kubwa imeibuka nchini. Unaweza kuiona ukichungulia kwenye mitandao ya kijamii. Imesababishwa na akili...