Wachezaji 21 waitwa kikosini Tembo Warriors

Na Winfrida Mtoi

Jumla ya wachezaji  21 wameitwa kuunda  timu ya Taifa ya watu wenye ulemavu ‘Tembo Warriors’ kujiandaa na   mashindano ya Afrika  yatakayofanyika Aprili 14- 29,2024 nchini Misri

Akizungumza na waandishi wa habari leo Januari 22, 2024, Makamu Mwenyekiti wa Shirikisho la Soka kwa watu wenye ulemavu Tanzania (TAFF),  Athumani Lubandame, amesema tayari timu hiyo imeanza mazoezi.

” Sasa timu imeanza mazoezi rasmi ambayo yanafanyika Uwanja wa Uhuru, huku  tukiwa tunasubiri maelekezo ya Serikali kuingia kambi ya pamoja baadaye,” amesema Lubandame.

Kwa upande wake, Meneja wa timu hiyo, Zaharani Mwenyemti ,amesema lengo lao ni kufika fainali ya michuano hiyo.

Amesema wanataka kwenda   kutetea nafasi ya nne Afrika iliyowafanya  wafuzu Kombe la Dunia ambapo  waliishia hatua ya robo fainali.

Kocha Mkuu wa timu hiyo, Salvatory Edward , ametaja majina ya wachezaji walioitwa  kuwa ni  Bashara Alombile, Ally Juma Abdallah, Hassan Vuai Ameri, Abdulkarim Amin Khalifa, Shadrack  Hebron Sembele, Richard Fredy Swai, Ramadhan Ally Chomero.

Wengine ni Juma Mohamed Kidevu, Salimu Rashid Bakari, Steven Manumba Antony, Habibu Saidi, Salehe Mwipi, Khalfan Athumani,Emmanuel Nakala, Adamu Hassan, Lifati Anasi,Rojas Kadora, Julius Ngume, Kassimu Mohamed, Frank Ngairo na Wistin Sango.

spot_img

Latest articles

WATAHINIWA 1.16 MILIONI KUFANYA MTIHANI WA DARASA LA SABA

Na Tatu Mohamed JUMLA ya watahiniwa 1,168,649 kutoka shule 20,019 Tanzania Bara wanatarajiwa...

VETA DAR kuanzisha mafunzo ya Urejelezaji taka kuchochea ajira

Na Tatu Mohamed CHUO cha VETA Dar es Salaam kinatarajia kuanza kutoa mafunzo maalumu ya...

TANESCO YATUNUKIWA TUZO KUTAMBUA MCHANGO WA UBUNIFU NA MAENDELEO YA NISHATI

Na Mwandishi Wetu SHIRIKA la Umeme Tanzania (TANESCO) limekabidhiwa tuzo ya kwa kutambua mchango...

TANESCO YABORESHA MAISHA YA WAFANYAKAZI NYUMBA YA MUNGU

📌 Nyumba za wafanyakazi zakarabatiwa, kuboresha utendaji wa kazi 📌 Mtambo wa kisasa wa kuchakata...

More like this

WATAHINIWA 1.16 MILIONI KUFANYA MTIHANI WA DARASA LA SABA

Na Tatu Mohamed JUMLA ya watahiniwa 1,168,649 kutoka shule 20,019 Tanzania Bara wanatarajiwa...

VETA DAR kuanzisha mafunzo ya Urejelezaji taka kuchochea ajira

Na Tatu Mohamed CHUO cha VETA Dar es Salaam kinatarajia kuanza kutoa mafunzo maalumu ya...

TANESCO YATUNUKIWA TUZO KUTAMBUA MCHANGO WA UBUNIFU NA MAENDELEO YA NISHATI

Na Mwandishi Wetu SHIRIKA la Umeme Tanzania (TANESCO) limekabidhiwa tuzo ya kwa kutambua mchango...