Wachezaji 21 waitwa kikosini Tembo Warriors

Na Winfrida Mtoi

Jumla ya wachezaji  21 wameitwa kuunda  timu ya Taifa ya watu wenye ulemavu ‘Tembo Warriors’ kujiandaa na   mashindano ya Afrika  yatakayofanyika Aprili 14- 29,2024 nchini Misri

Akizungumza na waandishi wa habari leo Januari 22, 2024, Makamu Mwenyekiti wa Shirikisho la Soka kwa watu wenye ulemavu Tanzania (TAFF),  Athumani Lubandame, amesema tayari timu hiyo imeanza mazoezi.

” Sasa timu imeanza mazoezi rasmi ambayo yanafanyika Uwanja wa Uhuru, huku  tukiwa tunasubiri maelekezo ya Serikali kuingia kambi ya pamoja baadaye,” amesema Lubandame.

Kwa upande wake, Meneja wa timu hiyo, Zaharani Mwenyemti ,amesema lengo lao ni kufika fainali ya michuano hiyo.

Amesema wanataka kwenda   kutetea nafasi ya nne Afrika iliyowafanya  wafuzu Kombe la Dunia ambapo  waliishia hatua ya robo fainali.

Kocha Mkuu wa timu hiyo, Salvatory Edward , ametaja majina ya wachezaji walioitwa  kuwa ni  Bashara Alombile, Ally Juma Abdallah, Hassan Vuai Ameri, Abdulkarim Amin Khalifa, Shadrack  Hebron Sembele, Richard Fredy Swai, Ramadhan Ally Chomero.

Wengine ni Juma Mohamed Kidevu, Salimu Rashid Bakari, Steven Manumba Antony, Habibu Saidi, Salehe Mwipi, Khalfan Athumani,Emmanuel Nakala, Adamu Hassan, Lifati Anasi,Rojas Kadora, Julius Ngume, Kassimu Mohamed, Frank Ngairo na Wistin Sango.

spot_img

Latest articles

GST: Taarifa sahihi za kijiolojia ni msingi wa uchimbaji wenye tija

Na Mwandishi Wetu TAASISI ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) imewataka wachimbaji,...

NIC: Waandishi wa habari vinara wa kuhamasisha matumizi ya bima

Na Mwandishi Wetu SHIRIKA la Bima la Taifa (NIC Insurance) limewapongeza waandishi wa habari...

TAIC: Bima ya kilimo ni kinga ya mtaji wa wakulima na wafugaji

Na Mwandishi Wetu UMOJA wa Makampuni ya Bima za Kilimo Tanzania (TAIC) umewahimiza wakulima...

TIRA yatumia Nanenane kuhamasisha wakulima kujiunga na bima ya kilimo

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA) imetumia Maonesho ya Kimataifa ya...

More like this

GST: Taarifa sahihi za kijiolojia ni msingi wa uchimbaji wenye tija

Na Mwandishi Wetu TAASISI ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) imewataka wachimbaji,...

NIC: Waandishi wa habari vinara wa kuhamasisha matumizi ya bima

Na Mwandishi Wetu SHIRIKA la Bima la Taifa (NIC Insurance) limewapongeza waandishi wa habari...

TAIC: Bima ya kilimo ni kinga ya mtaji wa wakulima na wafugaji

Na Mwandishi Wetu UMOJA wa Makampuni ya Bima za Kilimo Tanzania (TAIC) umewahimiza wakulima...