Wachezaji 21 waitwa kikosini Tembo Warriors

Na Winfrida Mtoi

Jumla ya wachezaji  21 wameitwa kuunda  timu ya Taifa ya watu wenye ulemavu ‘Tembo Warriors’ kujiandaa na   mashindano ya Afrika  yatakayofanyika Aprili 14- 29,2024 nchini Misri

Akizungumza na waandishi wa habari leo Januari 22, 2024, Makamu Mwenyekiti wa Shirikisho la Soka kwa watu wenye ulemavu Tanzania (TAFF),  Athumani Lubandame, amesema tayari timu hiyo imeanza mazoezi.

” Sasa timu imeanza mazoezi rasmi ambayo yanafanyika Uwanja wa Uhuru, huku  tukiwa tunasubiri maelekezo ya Serikali kuingia kambi ya pamoja baadaye,” amesema Lubandame.

Kwa upande wake, Meneja wa timu hiyo, Zaharani Mwenyemti ,amesema lengo lao ni kufika fainali ya michuano hiyo.

Amesema wanataka kwenda   kutetea nafasi ya nne Afrika iliyowafanya  wafuzu Kombe la Dunia ambapo  waliishia hatua ya robo fainali.

Kocha Mkuu wa timu hiyo, Salvatory Edward , ametaja majina ya wachezaji walioitwa  kuwa ni  Bashara Alombile, Ally Juma Abdallah, Hassan Vuai Ameri, Abdulkarim Amin Khalifa, Shadrack  Hebron Sembele, Richard Fredy Swai, Ramadhan Ally Chomero.

Wengine ni Juma Mohamed Kidevu, Salimu Rashid Bakari, Steven Manumba Antony, Habibu Saidi, Salehe Mwipi, Khalfan Athumani,Emmanuel Nakala, Adamu Hassan, Lifati Anasi,Rojas Kadora, Julius Ngume, Kassimu Mohamed, Frank Ngairo na Wistin Sango.

spot_img

Latest articles

Taifa Stars ya Gamondi amrejesha Kelvin John

Na Mwandishi Wetu Kaimu Kocha Mkuu wa timu ya Taifa, Taifa Stars Miguel Gamondi amemrudisha...

‘Hali ya huduma ya maji Dar, Pwani ni shwari’

Na Mwandishi Wetu WAKAZI mbalimbali wa Jiji la Dar es Salaam na Mkoa wa...

Mwanasheria Mkuu wa Serikali: Uchaguzi Mkuu wa 2025 ni halali

Na Mwandishi wetu MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza Johari amesema kuwa, Uchaguzi Mkuu wa...

Viongozi wa dini waendelea kihimiza amani uchaguzi mkuu

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam VIONGOZI wa dini nchini wameendelea kuhimiza umuhimu wa kudumisha...

More like this

Taifa Stars ya Gamondi amrejesha Kelvin John

Na Mwandishi Wetu Kaimu Kocha Mkuu wa timu ya Taifa, Taifa Stars Miguel Gamondi amemrudisha...

‘Hali ya huduma ya maji Dar, Pwani ni shwari’

Na Mwandishi Wetu WAKAZI mbalimbali wa Jiji la Dar es Salaam na Mkoa wa...

Mwanasheria Mkuu wa Serikali: Uchaguzi Mkuu wa 2025 ni halali

Na Mwandishi wetu MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza Johari amesema kuwa, Uchaguzi Mkuu wa...