Wachezaji 21 waitwa kikosini Tembo Warriors

Na Winfrida Mtoi

Jumla ya wachezaji  21 wameitwa kuunda  timu ya Taifa ya watu wenye ulemavu ‘Tembo Warriors’ kujiandaa na   mashindano ya Afrika  yatakayofanyika Aprili 14- 29,2024 nchini Misri

Akizungumza na waandishi wa habari leo Januari 22, 2024, Makamu Mwenyekiti wa Shirikisho la Soka kwa watu wenye ulemavu Tanzania (TAFF),  Athumani Lubandame, amesema tayari timu hiyo imeanza mazoezi.

” Sasa timu imeanza mazoezi rasmi ambayo yanafanyika Uwanja wa Uhuru, huku  tukiwa tunasubiri maelekezo ya Serikali kuingia kambi ya pamoja baadaye,” amesema Lubandame.

Kwa upande wake, Meneja wa timu hiyo, Zaharani Mwenyemti ,amesema lengo lao ni kufika fainali ya michuano hiyo.

Amesema wanataka kwenda   kutetea nafasi ya nne Afrika iliyowafanya  wafuzu Kombe la Dunia ambapo  waliishia hatua ya robo fainali.

Kocha Mkuu wa timu hiyo, Salvatory Edward , ametaja majina ya wachezaji walioitwa  kuwa ni  Bashara Alombile, Ally Juma Abdallah, Hassan Vuai Ameri, Abdulkarim Amin Khalifa, Shadrack  Hebron Sembele, Richard Fredy Swai, Ramadhan Ally Chomero.

Wengine ni Juma Mohamed Kidevu, Salimu Rashid Bakari, Steven Manumba Antony, Habibu Saidi, Salehe Mwipi, Khalfan Athumani,Emmanuel Nakala, Adamu Hassan, Lifati Anasi,Rojas Kadora, Julius Ngume, Kassimu Mohamed, Frank Ngairo na Wistin Sango.

spot_img

Latest articles

Mwamuzi Mtanzania kuchezesha Kombe la Dunia

Na Mwandishi Wetu MWAMUZI wa Tanzania wa mpira wa miguu kwa watu wenye ulemavu, Shaban...

Dawasa yatoa elimu Uhifadhi wa maji katika wiki ya mazingira

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)...

Kampuni ya Media Brains yawapa mbinu za kidigitali waandishi wa habari Iringa

Na Mwandishi Wetu, Iringa KAMPUNI ya Media Brains kwa kushirikiana na Taasisi ya Konrad Adenauer...

Kibabage aimpa mzuka Serengeti Boys kuelekea fainali ya AFCON

Na Winfrida Mtoi BEKI wa timu ya Taifa (Taifa Stars), Nickson Kibabage amesema kitendo cha...

More like this

Mwamuzi Mtanzania kuchezesha Kombe la Dunia

Na Mwandishi Wetu MWAMUZI wa Tanzania wa mpira wa miguu kwa watu wenye ulemavu, Shaban...

Dawasa yatoa elimu Uhifadhi wa maji katika wiki ya mazingira

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)...

Kampuni ya Media Brains yawapa mbinu za kidigitali waandishi wa habari Iringa

Na Mwandishi Wetu, Iringa KAMPUNI ya Media Brains kwa kushirikiana na Taasisi ya Konrad Adenauer...