Media Brains,AGRA zapongezwa kwa kuwanoa wanahabari kuhusu mbegu bora

Na Winfrida Mtoi, Media Brains

MWENYEKITI wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Deodatus Balile, amezipongeza kampuni ya Media Brains na Shirika linalojihusisha na Kuendeleza Mifumo ya Chakula Afrika (AGRA) kwa kuandaa mafunzo kwa wanahabari yanayohusu mbegu bora za kilimo na mfumo wake wa uzalishaji.

Media Brains na AGRA zimeandaa mafunzo hayo ya siku mbili yaliyofanyika Novemba 3-4, 2023 katika hoteli ya Oceanic iliyopo Bagamoyo, yakihusisha wahariri wa vyombo vya habari na waandishi wa habari.

Balile ambaye ni kati ya washiriki, amesema mafunzo hayo ni ya kipekee ambayo ni tofauti na waliyozoea kufanya mengi yakilenga zaidi masuala ya siasa.

Dr. Emmarold Mneney akitoa mada kwa wahariri na waandishi wa habari wakati wa mafunzo hayo.

“Niwapongeze Media Brains na AGRA kwa kuandaa mafunzo haya ya kipeke, mikutano kama hii inayogusa wananchi moja kwa moja imekuwa haipewi kipaombele,” amesema Balile.

Wawezeshaji katika mafunzo hayo ni watafiti wabobezi katika masuala ya mbegu kutoka taasisi mbalimbali, akiwamo Dk. Emmarold Mneney ambaye amebainisha kuwa mbegu bora ina uwezo wa kukabiliana na tabianchi.

Ofisa Mtendaji Mkuu wa Media Brains, Jesse Kwayu akitoa neno katika mafunzo hayo.

Dk. Mneney amefafanua kuwa mabadiliko ya tabianchi hayawezi kukwepeka na njia ya kukabiliana nayo ni kuzalisha mbegu zilizoboreshwa ili kufikia lengo la kuilisha dunia.

“Elimu ya mbegu haipo ya kutosha, inatakiwa kutolewa kwa vitendo ili wananchi waweze kuhamasika na kuzalisha mbegu zenye ubora,” ameeleza Dk. Mneney.

Naye Dk. Geradine Mzena kutoka Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania TARI, amesema kutokana na ongezeko la idadi ya watu na wazalishaji wa mbegu wanatakiwa kuwa wengi ili kupata chakula kinachotosheleza.

“Ni kweli mbegu hazitoshi lakini Serikali imeanza kujenga maeneo mengine ya kuzalisha mbegu ili kulinda chakula,” amesema.

spot_img

Latest articles

DC Mpogolo: viongozi wa Serikali za Mitaa ni watu muhimu Katika Usimamizi wa Huduma za Umeme

Na Tatu Mohamed VIONGOZI wa Serikali za Mitaa wametajwa kuwa watu muhimu katika kusimamia miundo...

Rais Samia aagiza Tume kuchunguza, kujua haki wanayoidai vijana

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk.Samia Suluhu Hassan ameielekeza Tume...

Bado denial inasuta nafsi za wengi, hatuwezi kupona

LEO ni siku ya 23 tangu risasi ya kwanza ilipofyatuliwa na kuua vijana waliokuwa...

Watoto mapacha wajinyonga Zanzibar, kisa kazi za ndani

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba linachunguza tukio la kujinyonga kwa...

More like this

DC Mpogolo: viongozi wa Serikali za Mitaa ni watu muhimu Katika Usimamizi wa Huduma za Umeme

Na Tatu Mohamed VIONGOZI wa Serikali za Mitaa wametajwa kuwa watu muhimu katika kusimamia miundo...

Rais Samia aagiza Tume kuchunguza, kujua haki wanayoidai vijana

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk.Samia Suluhu Hassan ameielekeza Tume...

Bado denial inasuta nafsi za wengi, hatuwezi kupona

LEO ni siku ya 23 tangu risasi ya kwanza ilipofyatuliwa na kuua vijana waliokuwa...